Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
na ugomvi; lakini kwa namna matisho <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong>lizidi, ndipo furaha <strong>ya</strong>ngu iliongezeka...<br />
Wamekwisha kuharibu heshima (sifa) <strong>ya</strong>ngu na mwenendo wangu. ... Kuhusu roho <strong>ya</strong>ngu,<br />
hawawezi kuikamata. Yeye anayetaka kutangaza neno la Kristo ulimwenguni, inampasa<br />
kutazamia kifo wakati wowote.”<br />
Akari <strong>ya</strong> kufika kwa Luther huko Augsburg kukaleta kushelewa kukubwa kwa mjumbe<br />
wa Papa. Mpinga mafundisho <strong>ya</strong> dini anayeamsha ulimwengu akaonekana sasa kuwa chini<br />
<strong>ya</strong> uwezo wa Roma; hakupaswa kuponyoka. Mjumbe alikusudia kulazimisha Luther kukana,<br />
ao isipowezekana alazimishe kwenda Roma kufuata n<strong>ya</strong>yo <strong>ya</strong> Huss na Jerome. Mjumbe wa<br />
Papa akatuma watu wake kumwambia Lutter afike bila ahadi <strong>ya</strong> ulinzi salama wa mfalme na<br />
matumaini <strong>ya</strong>ke mwenyewe wema wake. Kwa hiyo mtengenezaji akakataa. Hata wakati<br />
alipopata ahadi <strong>ya</strong> ulinzi wa mfalme mkuu ndipo akakubali kuonekana mbele <strong>ya</strong> mjumbe wa<br />
Papa. Kama mpango wa busara, watu wa Roma wakakusudia kumpata Luther kwa njia <strong>ya</strong><br />
kujioyesha kama wapole.<br />
Mjumbe akajionyesha kawa rafiki mkubwaa, lakini akaomba kwamba Luther ajitoe kabisa<br />
kwa kanisa na kukubali kila kitu bila mabishano wala swali. Luther, kwa kujibu, akaonyesha<br />
heshima <strong>ya</strong>ke kwa ajili <strong>ya</strong> kanisa, mapenzi <strong>ya</strong>ke kwa ajili <strong>ya</strong> ukweli, kuwa ta<strong>ya</strong>ri kwa kujibu<br />
makatazo yote kuhusu <strong>ya</strong>le aliyo<strong>ya</strong>fundishwa, na kuweka mafundisho <strong>ya</strong>ke chini <strong>ya</strong> uamuzi<br />
wa vyuo vikubwa (universites). Lakini alikataa juu <strong>ya</strong> mwendo wa askofu katika<br />
kummulazimisha kukana bila kuonyesha na kuhakikisha kosa lake.<br />
Jibu moja tu lilikuwa, “uKane, ukane”! Mtengenezaji akaonyesha kwamba msiimamo<br />
wake unakubaliwa na Maandiko. Hakuweza kukana ukweli. Mjumbe, aliposhindwa kujibu<br />
kwa mabishano <strong>ya</strong> Luther, akamulemeza na zoruba <strong>ya</strong> laumu, zarau, sifa <strong>ya</strong> uongo maneno<br />
kutoka kwa kiasili (traditions), na mezali (maneno) <strong>ya</strong> Wababa, akikatalia Mtengenezaji<br />
nafasi <strong>ya</strong> kusema. Luther mwishowe, bila kupenda, akamupa ruhusa <strong>ya</strong> kutoa jibu lake kwa<br />
maandiko.<br />
Akasema,akiandika kwa rafiki, “Mambo <strong>ya</strong>liyoandikwa ingeweza kutolewa kwa mawazo<br />
<strong>ya</strong> wengine; na jambo la pili, mtu anakuwa na bahati nzuri sana <strong>ya</strong> kutumika kwa hofu nyingi,<br />
kama si kwa zamiri, <strong>ya</strong> bwana wa kiburi na wa kusema ovyo ovyo ambaye njia ingine<br />
angeshinda kwa kutumia maneno <strong>ya</strong>ke makali.” Kwa mkutano uliofuata, Luther akaonyesha<br />
maelezo mafupi na <strong>ya</strong> nguvu <strong>ya</strong> mawazo <strong>ya</strong>ke, <strong>ya</strong>nayoshuhudiwa na Maandiko. Kartasi hii,<br />
baada <strong>ya</strong> kusoma kwa sauti nguvu, akaitoa kwa askofu, naye akaitupa kando kwa zarau,<br />
kuitangaza kuwa mchanganyiko wa maneno <strong>ya</strong> bure na mateuzi <strong>ya</strong>siyofaa. Sasa Luther<br />
akakutana na askofu wa kiburi kwa uwanja wake mwenyewe--mambo <strong>ya</strong> asili na mafundisho<br />
<strong>ya</strong> kanisa--na kuangusha kabisa majivuno <strong>ya</strong>ke.<br />
Askofu akapoteza kujitawala kote na katika hasira akapandisha sauti, “ukane! ao<br />
nitakutuma Roma”. Na mwishowe akatangaza, katika sauti <strong>ya</strong> kiburi na hasira, “uKane, ao<br />
usirudi tena.” Mtengenezaji kwa upesi akaondoka pamoja na rafiki zake, hivyo kutangaza<br />
wazi kwamba asingoje kwake kwamba atakana. Hili si jambo ambalo askofu alilokusudia.<br />
52