You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Kwa wakati huu, wageni wawili kutoka Uingereza, watu wa elimu, walipokea nuru na<br />
wakaja kuieneza katika Prague. Kwa upesi wakan<strong>ya</strong>mazishwa, lakini kwa sababu hawakutaka<br />
kuacha kusudi lao, wakatafuta mashauri mengine. Walipokuwa wafundi pia wahubiri, katika<br />
mahali wazi mbele <strong>ya</strong> watu wakachora picha mbili. Moja ikaonyesha kuingia kwa Kristo<br />
katika Yerusalema, “Mpole, naye amepanda mwana punda” (Matayo 21:5) na akafuatwa na<br />
wanafunzi wake katika mavazi <strong>ya</strong> kuzeeka juu <strong>ya</strong> safari na miguu wazi. Picha ingine ilieleza<br />
mwandamano wa askofu-papa katika kanzu zake za utajiri na taji tatu, mwenye akapanda<br />
farasi ambaye amepambwa vizuri sana, ametanguliwa na wapiga tarumbeta na kufuatwa na<br />
wakuu wa baraza <strong>ya</strong> papa (cardinals) na maaskofu katika mavazi <strong>ya</strong> kifalme.<br />
Makutano <strong>ya</strong>kaja kutazama mapicha. Hapana mtu aliweza kushindwa kusoma maana.<br />
Kukawa makelele mengi katika Prague, na wageni wakaona kwamba inafaa kuondoka. Lakini<br />
picha ikaleta wazo kubwa kwa Huss na ikamwongoza karibu sana na uchunguzi wa Biblia na<br />
wa maandiko <strong>ya</strong> Wycliffe. Ingawa alikuwa hakujita<strong>ya</strong>risha bado kukubali matengenezo yote<br />
<strong>ya</strong>liyotetewa na Wycliffe, aliona tabia <strong>ya</strong> kweli <strong>ya</strong> kanisa la Roma, na akalaumu kiburi, tamaa<br />
<strong>ya</strong> nguvu, na makosa <strong>ya</strong> mamlaka <strong>ya</strong> dini.<br />
Prague Ikawekwa Chini <strong>ya</strong> Makatazo<br />
Habari zikapelekwa Roma, na Huss akaitwa kwa kuonekana mbele <strong>ya</strong> Papa. Kutii<br />
kungalileta kifo cha kweli. Mfalme na malkia wa Bohemia, chuo kikuu, washiriki wa chuo<br />
kikuu, na wakuu wa serkali, wakajiunga katika mwito kwa askofu kwamba Huss aruhusiwe<br />
kubaki huko Prague na kujibu kwa njia <strong>ya</strong> ujumbe. Baadaye, Papa akaendelea kuhukumu<br />
nakulaumu Huss, na akatangaza mji wa Prague kuwa chini <strong>ya</strong> makatazo.<br />
Katika mwaka ule hukumu hii ikatia kofu. Watu walimuzania Papa kama mjumbe wa<br />
Mungu, wa kushika funguo za mbingu na jehanamu na kuwa na uwezo kuita hukumu.<br />
Iliaminiwa kwamba mpaka ilipaswa kupendeza Papa kutosha laana, wafu wangefungiwa<br />
kutoka kwa makao <strong>ya</strong> heri. Kazi zote za dini zikakatazwa. Makanisa <strong>ya</strong>kafungwa. Ndoa<br />
zikaazumishwa katika uwanja wa kanisa. Wafu wakazikwa bila kanuni ndani <strong>ya</strong> mifereji ao<br />
mashambani.<br />
Prague ikajaa na msukosuko. Kundi kubwa <strong>ya</strong> watu wakalaumu Huss na wakadai kwamba<br />
alazimiswe kwenda Roma. Kwa kutuliza makelele, Mtengenezaji akapelekwa kwa mda katika<br />
kijiji chake cha kuzaliwa. Hakuacha kazi zake, bali alisafiri katika inchi na kuhubiri makutano<br />
<strong>ya</strong> hamu kubwa. Wakati mwamsho katika Prague ulipotulia, Huss akarudi kuendelea kuhubiri<br />
Neno la Mungu. Adui zake walikuwa hodari, lakini malkia na wenye cheo kikuu wengi<br />
walikuwa rafiki zake, na watu katika hesabu kubwa wakamfuata.<br />
Huss alisimama peke <strong>ya</strong>ke katika kazi <strong>ya</strong>ke. Sasa Jerome akajiunga katika matengenezo.<br />
Wawili hawa baadaye wakajiunga katika maisha <strong>ya</strong>o, na katika mauti hawakuweza kuachana.<br />
Katika watu bora hawa ambao huleta nguvu <strong>ya</strong> kweli <strong>ya</strong> tabia, Huss alikuwa mkubwa zaidi.<br />
37