12.04.2023 Views

Kupinga ya Kiprotestanti

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />

Sura 41. Dunia katika Uharibifu<br />

Wakati sauti <strong>ya</strong> Mungu inapogeuza utumwa wa watu wake, pale panakuwa na muamko<br />

wa kutisha wa wale waliopoteza vyote katika vita kubwa <strong>ya</strong> maisha. Kupofushwa na<br />

madanganyo <strong>ya</strong> Shetani watajiri wakajisifu wenyewe kwa ukuu wao kwa wale wasiofanikiwa<br />

sana. Lakini hawakujali kulisha wenye njaa, kuvika wale waliokuwa unchi, kufan<strong>ya</strong> kwa haki,<br />

na kupenda rehema. Sasa wameondolewa vyote vilivyowafan<strong>ya</strong> kuwa wakubwa na<br />

wameachwa ukiwa (maskini). Wanatazama kwa hofu juu <strong>ya</strong> kuangamia kwa sanamu zao.<br />

Wameuzisha nafsi zao kwa ajili <strong>ya</strong> anasa <strong>ya</strong> dunia na hawakuwa watajiri kwa Mungu. Maisha<br />

<strong>ya</strong>o ni <strong>ya</strong> kushindwa, anasa zao zimegeuka kuwa uchungu. Faida <strong>ya</strong> maisha <strong>ya</strong>o yote imepotea<br />

kwa wakati moja. Watajiri wanalilia kuangamia kwa nyumba zao kubwa, kutawanyika kwa<br />

zahabu <strong>ya</strong>o na feza, na hofu <strong>ya</strong> kwamba wao wenyewe wanapashwa kuangamia pamoja na<br />

sanamu zao. Waovu wanaomboleza <strong>ya</strong> kwamba matokeo ni vile inavyokuwa, lakini hawatubu<br />

kwa maovu <strong>ya</strong>o.<br />

Mhubiri aliyefan<strong>ya</strong> ukweli kwa kafara makusudi <strong>ya</strong> kupata upendeleo wa watu sasa<br />

anatambua mvuto wa mafundisho <strong>ya</strong>ke. Kila mustari ulioandikwa, kila neno lililotamkwa<br />

lililoongoza watu kudumu katika kimbilio la uwongo limetawan<strong>ya</strong> mbegu: na sasa anatazama<br />

mavuno. Bwana anasema: “Ole wao wachungaji, wanaoharibu na kutawan<strong>ya</strong> kondoo za<br />

malisho <strong>ya</strong>ngu! ... Angalieni, nitaleta juu yenu uovu wa matendo yenu”. “kwa uwongo<br />

mumehuzunisha moyo wao walio haki, nisiowahuzunisha; nakutia nguvu mikono <strong>ya</strong> mwovu,<br />

hata asigeuke toka njia <strong>ya</strong>ke <strong>ya</strong> uovu, na kuponyeshwa hai”. Yeremia 23:1,2; Ezekieli 13:22.<br />

Wahubiri na watu wanaona <strong>ya</strong> kuwa wameasi juu <strong>ya</strong> Muumba wa sheria yote <strong>ya</strong> haki.<br />

Kuweka pembeni maagizo <strong>ya</strong> Mungu kulitoa mwinuko kwa maelfu <strong>ya</strong> nguvu za uovu, hata<br />

dunia ikawa mfereji moja mkubwa wa zambi. Hakuna lugha inayoweza kueleza tamaa <strong>ya</strong><br />

wasiowaaminifu wanapotazama wale walivyopoteza milele--uzima wa milele.<br />

Watu wanashitakiana wao kwa wao kwa ajili <strong>ya</strong> kuwaongoza kwa uharibifu, lakini wote<br />

wanaunganika kwa kukusan<strong>ya</strong> hukumu <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong> uchungu mkubwa juu <strong>ya</strong> wachungaji<br />

wasiokuwa waaminifu waliotabiri “maneno <strong>ya</strong> laini” (Isa<strong>ya</strong> 30:10), walioongoza wasikilizaji<br />

wao kufan<strong>ya</strong> ukiwa sheria <strong>ya</strong> Mungu na kutesa wale wangeishika kama takatifu.<br />

“Tumepotea”! wameomboleza, “na ninyi ndio munaokuwa sababu yenyewe”. Mikono<br />

iliyowatawaza zamani kwa heshima itan<strong>ya</strong>nyuliwa kwa ajili <strong>ya</strong> uharibifu wao. Po pote<br />

kunakuwa vita na umwangaji wa damu.<br />

Mwana wa Mungu na wajumbe wa mbinguni wamekuwa katika vita pamoja na muovu,<br />

kwa kuon<strong>ya</strong>, kuangazia, na kuokoa wana wa watu. Sasa wote wamefan<strong>ya</strong> mipango<br />

(makusudi) <strong>ya</strong>o; waovu wameungana kabisa na Shetani katika vita kupigana na Mungu.<br />

Mabishano si <strong>ya</strong> Shetani peke <strong>ya</strong>ke, lakini pamoja na watu. “Bwana ana mashindano na<br />

mataifa”. Yeremia 25:31.<br />

Malaika wa Mauti<br />

267

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!