12.04.2023 Views

Kupinga ya Kiprotestanti

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />

Mkufuru akafaulu katika kujionyesha mwenyewe “juu <strong>ya</strong> yote <strong>ya</strong>nayoitwa Mungu, ao<br />

kuabudiwa.” 2 Watesalonika 2:4. Alisubutu kugeuza amri moja tu <strong>ya</strong> sheria <strong>ya</strong> Mungu<br />

inayoonyesha Mungu wa kweli na wa uhai. Katika amri <strong>ya</strong> ine, Mungu hufunuliwa kama<br />

Muumba. Kama ukumbusho wa kazi <strong>ya</strong> kuumba, siku <strong>ya</strong> saba ikatakaswa kama siku <strong>ya</strong><br />

pumziko la mtu, iliyokusudiwa kulinda Mungu wa uhai siku zote mbele <strong>ya</strong> akili za watu kama<br />

kitu cha ibada. Shetani hujitaidi kugeuza watu kwa utii wa sheria <strong>ya</strong> Mungu; kwa hivyo<br />

huelekeza nguvu zake zaidi sana juu <strong>ya</strong> amri ile inayoonyesha Mungu kama Muumba.<br />

Waprotestanti sasa wanalazimisha kwamba ufufuo wa Kristo Siku <strong>ya</strong> Kwanza (Dimanche)<br />

uliifan<strong>ya</strong> kuwa Sabato <strong>ya</strong> Kikristo. Lakini hapana heshima <strong>ya</strong> namna hiyo iliyotolewa kwa<br />

siku ile na Kristo au mitume wake. Kawaida <strong>ya</strong> Siku <strong>ya</strong> Kwanza (Dimanche) ilikuwa na asili<br />

<strong>ya</strong>ke katika ile “siri <strong>ya</strong> uasi” (2 Watesalonika 2:7), ambayo, hata katika siku <strong>ya</strong> Paulo, ilianza<br />

kazi <strong>ya</strong>ke. Sababu gani inayoweza kutolewa kwa mageuzi ambayo Maandiko ha<strong>ya</strong>kuruhusu?<br />

Katika karne <strong>ya</strong> sita, askofu wa Roma alitangazwa kuwa kichwa cha kanisa yote nzima.<br />

Dini <strong>ya</strong> kipagani ikatoa nafasi kwa kanisa la Roma. Joka akamupa n<strong>ya</strong>ma “nguvu zake”, na<br />

kiti chake cha ufalme na mamlaka nyingi”. Ufunuo 13:2 (Tazama Nyongezo).<br />

Sasa ikaanza miaka 1260 <strong>ya</strong> mateso <strong>ya</strong> Papa iliyotabiriwa katika mambo <strong>ya</strong> unabii wa<br />

Danieli na Ufunuo. Danieli 7:25; Ufunuo 13:5-7. Wakristo walilazimishwa kuchagua au<br />

kuacha uaminifu wao na kukubali huduma na ibada za Papa, au kutoa maisha <strong>ya</strong>o katika<br />

gereza, au kuuawa. Sasa maneno <strong>ya</strong> Yesu <strong>ya</strong>litimilika: “Nanyi mutatolewa hata na wazazi<br />

wenu, na ndugu, na jamaa, na rafiki, na wengine wenu watawaua. Na mutachukiwa na watu<br />

wote kwa ajili <strong>ya</strong> jina langu” Luka 21:16, 17.<br />

Ulimwengu ukawa shamba kubwa sana la vita. Kwa mamia <strong>ya</strong> miaka kanisa la Kristo<br />

lilipaswa kuishi katika maficho na giza. “Yule mwanamuke akakimbia hata pori; kule ana<br />

pahali palipotengenezwa na Mungu ili wamulishe kule siku elfu moja mia mbili na makumi<br />

sita” Ufunuo 12:6.<br />

Kutawazwa kwa utawala wa Kanisa la Roma kulionyesha mwanzo wa miaka <strong>ya</strong> giza.<br />

Imani ikahamishwa kutoka kwa Kristo na kwenda kwa Papa wa Roma. Badala <strong>ya</strong> kutumainia<br />

Mwana wa Mungu kwa ajili <strong>ya</strong> musamaha wa zambi na wokovu wa milele, watu wakatazamia<br />

Papa, na mapadri ambao aliwatolea mamlaka <strong>ya</strong>ke. Papa alikuwa mpatanishi wao wa kidunia.<br />

Alisimama kwa mahali pa Mungu kwa ajili <strong>ya</strong>o. Kwenda pembeni <strong>ya</strong> mapenzi <strong>ya</strong>ke ilikuwa<br />

sababu <strong>ya</strong> kutosha kwa azabu kali. Kwa hiyo akili za watu zikatoka kwa Mungu zikageukia<br />

watu wapotevu, waba<strong>ya</strong>, niseme nini tena, kwa mfalme wa giza anayetumia uwezo wake<br />

kupita wao. Wakati Maandiko <strong>ya</strong>napokomeshwa na mtu anapojiona mwenyewe kuwa kama<br />

mkubwa kabisa, kitu kitakacho tazamiwa tu ni hila, madanganyo, na upunguo wa tabia njema.<br />

Siku za Hatari kwa Kanisa<br />

Wachukuzi wa bendera waaminifu walikuwa wachache sana. Hapo hapo ilionekana<br />

kwamba makosa ingekuwa karibu kushinda kabisa, na dini <strong>ya</strong> kweli kuondolewa duniani.<br />

18

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!