Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Mkufuru akafaulu katika kujionyesha mwenyewe “juu <strong>ya</strong> yote <strong>ya</strong>nayoitwa Mungu, ao<br />
kuabudiwa.” 2 Watesalonika 2:4. Alisubutu kugeuza amri moja tu <strong>ya</strong> sheria <strong>ya</strong> Mungu<br />
inayoonyesha Mungu wa kweli na wa uhai. Katika amri <strong>ya</strong> ine, Mungu hufunuliwa kama<br />
Muumba. Kama ukumbusho wa kazi <strong>ya</strong> kuumba, siku <strong>ya</strong> saba ikatakaswa kama siku <strong>ya</strong><br />
pumziko la mtu, iliyokusudiwa kulinda Mungu wa uhai siku zote mbele <strong>ya</strong> akili za watu kama<br />
kitu cha ibada. Shetani hujitaidi kugeuza watu kwa utii wa sheria <strong>ya</strong> Mungu; kwa hivyo<br />
huelekeza nguvu zake zaidi sana juu <strong>ya</strong> amri ile inayoonyesha Mungu kama Muumba.<br />
Waprotestanti sasa wanalazimisha kwamba ufufuo wa Kristo Siku <strong>ya</strong> Kwanza (Dimanche)<br />
uliifan<strong>ya</strong> kuwa Sabato <strong>ya</strong> Kikristo. Lakini hapana heshima <strong>ya</strong> namna hiyo iliyotolewa kwa<br />
siku ile na Kristo au mitume wake. Kawaida <strong>ya</strong> Siku <strong>ya</strong> Kwanza (Dimanche) ilikuwa na asili<br />
<strong>ya</strong>ke katika ile “siri <strong>ya</strong> uasi” (2 Watesalonika 2:7), ambayo, hata katika siku <strong>ya</strong> Paulo, ilianza<br />
kazi <strong>ya</strong>ke. Sababu gani inayoweza kutolewa kwa mageuzi ambayo Maandiko ha<strong>ya</strong>kuruhusu?<br />
Katika karne <strong>ya</strong> sita, askofu wa Roma alitangazwa kuwa kichwa cha kanisa yote nzima.<br />
Dini <strong>ya</strong> kipagani ikatoa nafasi kwa kanisa la Roma. Joka akamupa n<strong>ya</strong>ma “nguvu zake”, na<br />
kiti chake cha ufalme na mamlaka nyingi”. Ufunuo 13:2 (Tazama Nyongezo).<br />
Sasa ikaanza miaka 1260 <strong>ya</strong> mateso <strong>ya</strong> Papa iliyotabiriwa katika mambo <strong>ya</strong> unabii wa<br />
Danieli na Ufunuo. Danieli 7:25; Ufunuo 13:5-7. Wakristo walilazimishwa kuchagua au<br />
kuacha uaminifu wao na kukubali huduma na ibada za Papa, au kutoa maisha <strong>ya</strong>o katika<br />
gereza, au kuuawa. Sasa maneno <strong>ya</strong> Yesu <strong>ya</strong>litimilika: “Nanyi mutatolewa hata na wazazi<br />
wenu, na ndugu, na jamaa, na rafiki, na wengine wenu watawaua. Na mutachukiwa na watu<br />
wote kwa ajili <strong>ya</strong> jina langu” Luka 21:16, 17.<br />
Ulimwengu ukawa shamba kubwa sana la vita. Kwa mamia <strong>ya</strong> miaka kanisa la Kristo<br />
lilipaswa kuishi katika maficho na giza. “Yule mwanamuke akakimbia hata pori; kule ana<br />
pahali palipotengenezwa na Mungu ili wamulishe kule siku elfu moja mia mbili na makumi<br />
sita” Ufunuo 12:6.<br />
Kutawazwa kwa utawala wa Kanisa la Roma kulionyesha mwanzo wa miaka <strong>ya</strong> giza.<br />
Imani ikahamishwa kutoka kwa Kristo na kwenda kwa Papa wa Roma. Badala <strong>ya</strong> kutumainia<br />
Mwana wa Mungu kwa ajili <strong>ya</strong> musamaha wa zambi na wokovu wa milele, watu wakatazamia<br />
Papa, na mapadri ambao aliwatolea mamlaka <strong>ya</strong>ke. Papa alikuwa mpatanishi wao wa kidunia.<br />
Alisimama kwa mahali pa Mungu kwa ajili <strong>ya</strong>o. Kwenda pembeni <strong>ya</strong> mapenzi <strong>ya</strong>ke ilikuwa<br />
sababu <strong>ya</strong> kutosha kwa azabu kali. Kwa hiyo akili za watu zikatoka kwa Mungu zikageukia<br />
watu wapotevu, waba<strong>ya</strong>, niseme nini tena, kwa mfalme wa giza anayetumia uwezo wake<br />
kupita wao. Wakati Maandiko <strong>ya</strong>napokomeshwa na mtu anapojiona mwenyewe kuwa kama<br />
mkubwa kabisa, kitu kitakacho tazamiwa tu ni hila, madanganyo, na upunguo wa tabia njema.<br />
Siku za Hatari kwa Kanisa<br />
Wachukuzi wa bendera waaminifu walikuwa wachache sana. Hapo hapo ilionekana<br />
kwamba makosa ingekuwa karibu kushinda kabisa, na dini <strong>ya</strong> kweli kuondolewa duniani.<br />
18