You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Sura 31. Pepo Wachafu<br />
Malaika wa Bwana na pepo wachafu wanaonyeshwa wazi katika Maandiko na wanaingia<br />
katika historia <strong>ya</strong> wanadamu. Malaika watakatifu wale “wanaotumikia watakaoriti wokovu”<br />
(Waebrania 1:14) wanazaniwa kwa wengi kama pepo za waliokufa. Lakini Maandiko<br />
inaonyesha hakika kwamba hawa si pepo inayoachana na mwili wa waliokufa.<br />
Mbele <strong>ya</strong> kuumbwa kwa mtu, malaika walikuwa wakiishi, kwani wakati misingi <strong>ya</strong> dunia<br />
ilipowekwa, ‘’nyota za asubui waliimba pamoja, na wana wote wa Mungu walipiga kelele<br />
kwa furaha.” Yobu 38:7. Nyuma <strong>ya</strong> kuanguka kwa mtu, malaika walitumwa kulinda mti wa<br />
uzima mbele <strong>ya</strong> mwanadamu kufa. Malaika wanakuwa wakubwa kwa cheo kuliko watu, kwa<br />
kuwa mtu aliumba “chini kidogo kupita malaika “. Zaburi 8:5.<br />
Nabii anasema, “Nikasikia sauti <strong>ya</strong> malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi.” Mbele<br />
<strong>ya</strong> Mufalme wa wafalme wanangojea-“ninyi watumishi wake, munaofan<strong>ya</strong> mapenzi <strong>ya</strong>ke,”<br />
“mukisikiliza sauti <strong>ya</strong> neno lake,” “majeshi <strong>ya</strong> malaika elfu nyingi.” Ufunuo 5:11; Zaburi<br />
103:20,21; Waebrania 12:22. Kama wajumbe wa Mungu wanatoka, kama “kuonekana, kwa<br />
kumulika kwa umeme,” mruko wao mwepesi sana. Malaika aliyetokea kwa kaburi la<br />
Mwokozi, sura <strong>ya</strong>ke “kama umeme,” ikawaletea walinzi kwa ajili <strong>ya</strong> hofu kutetemeka, na<br />
“wakawa kama wafu.” Wakati Saniaribu alipomtukana Mungu na kuogopesha Waisraeli,<br />
“malaika wa Bwana alitoka, akapiga katika kambi <strong>ya</strong> Waasuria watu elfu mia moja makumi<br />
mnane na tano.” Ezekieli 1:14; Matayo 28:3,4; 2 Wafalme 19:35.<br />
Malaika wanatumwa kwa kazi <strong>ya</strong> rehema kwa wana wa Mungu. Kwa Abrahamu, kwa<br />
ahadi za baraka; kwa Sodomo, kuokoa Loti kwa maangamizo; kwa Elia, karibu kuangamizwa<br />
katika jangwa; kwa Elisa, kwa magari <strong>ya</strong> farasi <strong>ya</strong> moto alipofungiwa ndani na adui zake;<br />
kwa Danieli, wakati alipoachwa kuwa mawindo <strong>ya</strong> simba; kwa Petro, alipohukumiwa kifo<br />
katika gereza <strong>ya</strong> Herode; kwa wafungwa kule Filipi; kwa Paulo katika usiku wa zoruba juu<br />
<strong>ya</strong> bahari; kwa kufungua akili <strong>ya</strong> Kornelio kwa kukubali habari njema; kwa kutuma Petro<br />
pamoja na habari njema <strong>ya</strong> wokovu kwa mgeni wa Kimataifa--kwa hivi malaika watakatifu<br />
walitumikia watu wa Mungu.<br />
Malaika Walinzi<br />
Malaika mlinzi amewekwa kwa kila mfuasi wa Kristo. “Malaika <strong>ya</strong> Bwana anapiga kambi<br />
kuzunguka wale wanaomwogopa, na anawaokoa.” Akasema Mwokozi, juu <strong>ya</strong> wale<br />
wanaomwamini: “Mbinguni malaika zao wanatazama siku zote uso wa Baba <strong>ya</strong>ngu.” Zaburi<br />
34:7; Matayo 18:10. Watu wa Mungu, walihatarishwa kwa uovu usiolala wa mfalme wa giza,<br />
wanaahidiwa na ulinzi usiokoma wa malaika. Matumaini <strong>ya</strong> namna hiyo <strong>ya</strong>natolewa kwa<br />
sababu kunakuwa na nguvu kubwa za uovu za kukutana nazo--nguvu zisizohesabika, imara<br />
na zisizochoka.<br />
209