You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
aliyebaki ndani <strong>ya</strong> Yerusalema, ataitwa mtakatifu, kila mmoja aliyeandikwa katika wale walio<br />
hai ndani <strong>ya</strong> Yerusalema.” Yeremia 31:34; 50:20; Isa<strong>ya</strong> 4:3.<br />
Kufutia Mbali kwa Zambi<br />
Kazi <strong>ya</strong> hukumu <strong>ya</strong> uchunguzi na kufutia mbali zambi inapashwa kutimizwa mbele <strong>ya</strong><br />
kuja kwa Bwana mara <strong>ya</strong> pili. Katika huduma <strong>ya</strong> mfano kuhani mkuu alitoka inje na kubariki<br />
makutano. Vivyo hivyo Kristo, kwa mwisho wa kazi <strong>ya</strong>ke kama mpatanishi, ataonekana” si<br />
tena kwa zambi, lakini kwa wokovu.” Waebrania 9:28.<br />
Kuhani, katika kuondoa zambi kutoka Pahali patakatifu, aliziungama juu <strong>ya</strong> kichwa mbuzi<br />
wa Azazeli. Kristo ataweka zambi hizi zote juu <strong>ya</strong> Shetani, mshawishi wa zambi. Mbuzi wa<br />
Azazeli akapelekwa mbali “katika inchi isiyo na watu.” Walawi 16:22. Shetani, katika<br />
kuchukua hatia za zambi alizolazimisha watu wa Mungu kuzifan<strong>ya</strong>, atafungwa miaka elfu<br />
katika inchi isiyokaliwa kama jangwa na mwishoni atateswa kwa azabu <strong>ya</strong> moto<br />
utakaoangamiza waovu. Kwa hivi mpango wa wokovu utafikia utimilifu wake katika kungoa<br />
kwa mwisho kwa zambi.<br />
Kwa Wakati Uliotajwa<br />
Kwa wakati uliotajwa--mwisho wa siku 2300 katika 1844--kazi <strong>ya</strong> uchunguzi ikaanza na<br />
kufutiwa mbali kwa zambi. Zambi zisizoungamwa na kuachwa hazitafutwa kutoka vitabu v<strong>ya</strong><br />
ukumbusho. Malaika wa Mungu wakashuhudia kila zambi na kuiandika. Zambi inaweza<br />
kukanwa, kufichwa kwa Baba, mama, bibi, watoto, na kwa rafiki; lakini inawekwa wazi<br />
mbele <strong>ya</strong> mbingu. Mungu hadanganywe kwa matendo <strong>ya</strong>nayoonekana. Hafanyi makosa.<br />
Watu wanaweza kudanganywa kwa wale wanaochafuka ndani <strong>ya</strong> moyo, lakini Mungu<br />
anasoma maisha <strong>ya</strong> ndani.<br />
Ni wazo la kutisha namna gani! Mshindi mkubwa kupita duniani hawezi kurudisha<br />
ukumbusho wa matendo <strong>ya</strong> siku hata moja. Matendo yetu, maneno yetu, hata makusudi yetu<br />
<strong>ya</strong> siri, ijapo tuki<strong>ya</strong>sahau, <strong>ya</strong>tatoa ushuhuda wake kwa kuhesabiwa haki wala kuhukumiwa.<br />
Katika hukumu matumizi <strong>ya</strong> kila kipaji <strong>ya</strong>tachunguzwa. Namna gani tumetumia wakati<br />
wetu, kalamu yetu <strong>ya</strong> wino, sauti yetu, mali yetu, mvuto wetu? Tumefan<strong>ya</strong> nini kwa Kristo<br />
katika nafsi <strong>ya</strong> maskini, wenye kuteswa, <strong>ya</strong>tima, ao mjane? Tumefan<strong>ya</strong> nini na nuru pia na<br />
kweli tuliyopewa? Ila tu upendo ulioonyeshwa kwa matendo unaohesabiwa kuwa wa kweli.<br />
Upendo peke <strong>ya</strong>ke mbele <strong>ya</strong> Mungu wa mbinguni haufanye tendo lo lote la damani.<br />
Choyo lliyofichwa Imefunuliwa<br />
Mambo yote <strong>ya</strong> ukaidi wa choyo iliyofichwa <strong>ya</strong>mefunuliwa katika vitabu v<strong>ya</strong> mbinguni.<br />
Mara ngapi wakati, mawazo, na nguvu zinazokuwa za Kristo zilitolewa kwa Shetani. Wafuasi<br />
wa Kristo wanashughulika katika upataji wa mali <strong>ya</strong> kidunia ao furaha <strong>ya</strong> anasa <strong>ya</strong><br />
ulimwengu. Mali, wakati, na nguvu zinatumiwa kwa maonyesho na anasa; n<strong>ya</strong>kati za bidii<br />
kwa kuomba ni chache, kwa kutafuta Maandiko, kuungama zambi.<br />
199