You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Sura 28. Hukumu Nzito<br />
“Nikaangalia hata viti v<strong>ya</strong> enzi vilipowekwa, na mmoja aliye mzee wa siku akaketi:<br />
mavazi <strong>ya</strong>ke <strong>ya</strong>likuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi, kiti<br />
chake cha enzi kilikuwa ndimi za moto, na magurudumu <strong>ya</strong>ke moto unaowaka. Na mto wa<br />
moto ukatoka, ukapita mbele <strong>ya</strong>ke, elfu <strong>ya</strong> maelfu wakamutumikia, na elfu kumi mara elfu<br />
kumi walisimama mbele <strong>ya</strong>ke: hukumu ikawekwa, vitabu vikafunguliwa.” Danieli 7:9,10.<br />
R.V.<br />
Ndivyo ilivyoonyeshwa kwa njozi <strong>ya</strong> Danieli siku kubwa wakati maisha <strong>ya</strong> watu inapopita<br />
katika mkaguo mbele <strong>ya</strong> Mwamzi wa dunia yote. Mzee wa Siku ni Mungu Baba. Yeye,<br />
chemchemi <strong>ya</strong> viumbe vyote,kisima cha sheria yote, anapaswa kuongoza katika hukumu. Na<br />
malaika watakatifu kama wahuduma na washuhuda, wanahuzuria.<br />
“Na tazama, pamoja na mawingu <strong>ya</strong> mbingu alikuja mmoja aliye mfano wa mwana wa<br />
watu, akakaribia huyu Mzee wa Siku, wakamuleta karibu mbele <strong>ya</strong>ke. Akapewa mamlaka, na<br />
utukufu, na ufalme, ili watu wote, mataifa yote, na lugha zote wamutumikie; mamlaka <strong>ya</strong>ke<br />
ni mamlaka <strong>ya</strong> milele, isiyopita kamwe, na ufalme wake ufalme usioweza kuangamizwa.”<br />
Danieli 7:13,14.<br />
Kuja kwa Kristo kunakoelezwa hapa si kuja kwake kwa mara <strong>ya</strong> pili duniani. Anakuja<br />
kwa Mzee wa Siku katika mbingu kupokea ufalme ambao utatolewa kwake wakati wa<br />
mwisho wa kazi <strong>ya</strong>ke kama mpatanishi. Ni kuja huko, na si kuja kwake kwa mara <strong>ya</strong> pili<br />
dunianini, ile iliyopashwa kufanyika kwa mwisho wa siku 2300 katika mwaka 1844. Kuhani<br />
wetu Mkuu anaingia Pahali patakatifu pa patakatifu kushughulika katika kazi <strong>ya</strong>ke <strong>ya</strong> mwisho<br />
kwa ajili <strong>ya</strong> mtu.<br />
Katika huduma <strong>ya</strong> mfano ila wale ambao zambi zao zilihamishwa kwa Pahali patakatifu<br />
walikuwa na sehemu katika Siku <strong>ya</strong> Upatanisho. Vivyo hivyo katika upatanisho kubwa wa<br />
mwisho na hukumu <strong>ya</strong> uchunguzi kesi zilizoangaliwa ni zile za watu wa Mungu<br />
wanaojulikana. Hukumu <strong>ya</strong> waovu ni kazi iliyotengwa na itafanywa baadaye. “Hukumu<br />
inapashwa kuanza katika nyumba <strong>ya</strong> Mungu.” 1 Petro 4:17.<br />
Vitabu v<strong>ya</strong> ukumbusho katika mbingu vianapaswa kuamua matokeo <strong>ya</strong> hukumu. Kitabu<br />
cha uzima kinakuwa na majina <strong>ya</strong> wote walioingia daima kwa kazi <strong>ya</strong> Mungu. Yesu aliambia<br />
wanafunzi wake: “Lakini furahini kwa sababu majina yenu <strong>ya</strong>meandikwa katika mbingu.”<br />
Paulo anasema juu <strong>ya</strong> watumishi wenzake, “Walio na majina <strong>ya</strong>o katika kitabu cha uzima.”<br />
Danieli anatangaza kwamba watu wa Mungu watakombolewa, “kila mtu atakayeonekana<br />
ameandikwa katika kitabu.” Na mfumbuaji anasema kwamba wale tu watakaoingia Mji wa<br />
Mungu ambao majina <strong>ya</strong>o “walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.”<br />
Luka 10:20; Wafilipi 4:3; Danieli 12:1; Ufunuo 21:27.<br />
196