Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Kwa kujita<strong>ya</strong>risha kwa hukumu, watu wanapashwa kushika sheria <strong>ya</strong> Mungu, kipimo cha<br />
tabia katika hukumu. Paulo anasema: “Wote waliokosa wakiwa na sheria, watahukumiwa<br />
kwa sheria, ... katika siku ile Mungu atakapohukumu siri za watu ... kwa Yesu Kristo.” “Wale<br />
wanaotenda sheria watakaohesabiwa haki.” Imani ina maana sana ili kushika sheria <strong>ya</strong><br />
Mungu; kwani “pasipo imani haiwezekani kumupendeza.” “Kila tendo lisilotoka katika imani<br />
ni zambi.” Waroma 2:12-16; Waebrania 11:6; Waroma 14:23.<br />
Malaika wa kwanza aliita watu kwa “kuogopa Mungu, na kumutukuza” na kumwabudu<br />
yeye aliyefan<strong>ya</strong> mbingu na dunia. Kwa kufan<strong>ya</strong> hii, wanapaswa kutii sheria <strong>ya</strong>ke. Bila kutii<br />
hakuna ibada inayoweza kupendeza Mungu. “Kwa maana kupenda Mungu ni kushika amri<br />
zake.” 1 Yoane 5:3; Tazama Mezali 28:9.<br />
Mwito kwa Kuabudu Muumba<br />
Wajibu kwa kuabudu Mungu unaimarishwa juu <strong>ya</strong> kweli kwamba yeye ni Muumba.<br />
“Kujeni, tuabudu na kuinama; Tupige magoti mbele <strong>ya</strong> Bwana mwenye kutuumba.” Zaburi<br />
95:6; Tazama Zaburi 95:5; Zaburi 100:3; Isa<strong>ya</strong> 40:25,26; 45:18.<br />
Katika Ufunuo 14, watu wameitwa kuabudu Muumba na kushika amri za Mungu.<br />
Mojawapo <strong>ya</strong> amri hizi inaonyesha kwa Mungu kama Muumba: “Siku <strong>ya</strong> saba ni sabato kwa<br />
Bwana Mungu wako: ... Maana kwa siku sita Bwana akafan<strong>ya</strong> mbingu na inchi, bahari na<br />
vyote vilivyo ndani <strong>ya</strong>ke, akapumzika siku <strong>ya</strong> saba. Kwa hivi Bwana akabariki siku <strong>ya</strong> sabato<br />
na kuitakasa.” Kutoka 20:10,11. Sabato, Bwana anasema, ni “alama, ... mujue <strong>ya</strong> kuwa mimi<br />
ni Bwana Mungu wenu.” Ezekieli 20:20. Kama Sabato ingeshikwa kwa wote, mtu angeweza<br />
kuongozwa kwa Muumba kama jambo la kuabudu. Hapo hapangalikuwa kamwe mwabudu<br />
sanamu, asiyesadiki (Mungu), wala kafiri. Kushika Sabato ni alama <strong>ya</strong> uaminifu kwa “yeye<br />
aliyefan<strong>ya</strong> mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.” Ujumbe unaoagiza watu<br />
kuabudu Mungu na kushika amri zake utawaita kwa kipekee muwaite kushika amri <strong>ya</strong> ine.<br />
Katika tofauti kuwa wale wanaoshika amri za Mungu na imani <strong>ya</strong> Yesu, malaika wa tatu<br />
anaonyesha kwa kundi lingine: “Mtu akiabudu n<strong>ya</strong>ma na sanamu <strong>ya</strong>ke, na kupokea chapa<br />
katika kipaji cha uso wake, ao katika mkono wake, yeye atakunywa mvinyo <strong>ya</strong> gazabu <strong>ya</strong><br />
Mungu.” Ufunuo 14:9,10. Ni nini inayokuwa mfano wa n<strong>ya</strong>ma, sanamu, chapa?<br />
Unabii ambamo mifano hii inapatikana unaanza kwa Ufunuo 12. Joka yule aliyetafuta<br />
kuharibu Kristo kwa kuzaliwa kwake ilisemwa kuwa Shetani (Ufunuo 12:9); akavuta Herode<br />
kuua Mwokozi. Lakini mjumbe wa Shetani katika kufan<strong>ya</strong> vita juu <strong>ya</strong> Kristo na watu wake<br />
kwa karne za kwanza ilikuwa ufalme wa Roma, ambamo upagani ulikuwa ni dini iliyoshinda.<br />
Kwa hiyo joka ni, kwa namna <strong>ya</strong> pili, mfano wa Roma <strong>ya</strong> kipagani.<br />
Katika Ufunuo 13 ni n<strong>ya</strong>ma mwingine, “mfano wa chui,” ambaye joka akamupa “nguvu<br />
zake, na kiti chake cha ufalme na mamlaka nyingi.” Mfano huu, kama vile Waprostanti wengi<br />
walivyoamini, unakuwa mfano wa dini <strong>ya</strong> Papa, iliyofuata kwa nguvu (mamlaka) na kiti cha<br />
ufalme na mamlaka iliyoshikwa kuanza na ufalme wa Roma. Juu <strong>ya</strong> n<strong>ya</strong>ma aliyekuwa na<br />
179