You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Sura 24. Kristo Anafan<strong>ya</strong> Kazi Gani Sasa?<br />
Fundisho la Pahali patakatifu likafungua siri <strong>ya</strong> uchungu. Likafungua kwa maoni kanuni<br />
kamili <strong>ya</strong> ukweli, yenye uhusiano na <strong>ya</strong> kulingana, kuonyesha mkono wa Mungu ulioongoza<br />
kazi kubwa juu <strong>ya</strong> kuja kwa Yesu. Wale waliotazamia kwa imani kuja kwake mara <strong>ya</strong> pili<br />
wakamtazamia kutokea katika utukufu, lakini kwa namna matumaini <strong>ya</strong>o ha<strong>ya</strong>kufanyikiwa,<br />
wakapoteza akili juu <strong>ya</strong> Yesu. Sasa ndani <strong>ya</strong> patakatifu pa patakatifu wakatazama tena Kuhani<br />
wao mkubwa, kutokea upesi kama mfalme na mkombozi. Nuru kutoka kwa Pahali patakatifu<br />
ikaangazia wakati uliopita, wakati wa sasa, na wakati ujao. Ingawa walishindwa kufahamu<br />
ujumbe waliopata, kwani ulikuwa wa kweli.<br />
Kosa halikuwa katika kutambua kwa n<strong>ya</strong>kati za unabii, lakini katika tukio kufanyika kwa<br />
mwisho wa siku 2300. Kwani yote <strong>ya</strong>liyotabiriwa na unabii <strong>ya</strong>litimilika. Kristo alikuja, si<br />
duniani, bali katika Pahali patakatifu pa patakatifu pa hekalu katika mbingu; “Nikaona katika<br />
maono <strong>ya</strong> usiku, na tazama, pamoja na mawingu <strong>ya</strong> mbingu alikuwa mmoja aliye mfano wa<br />
mwana wa watu, akakaribia huyu Mzee wa Siku, wakamuleta karibu naye.” Danieli 7:13.<br />
Kuja huku kulitabiriwa pia na Malaika: “Na Bwana munayemutafuta atakuja gafula<br />
hekaluni mwake; na mujumbe wa agano munayemupenda, tazameni, atakuja, Bwana wa<br />
majeshi anasema.” Malaki 3:1. Kuja kwa Bwana katika hekalu <strong>ya</strong>ke kulikuwa kwa gafula,<br />
hakukuzaniwa kwa watu wake. Hawakuwa wakimtazamia pale.<br />
Watu hawakuwa bado ta<strong>ya</strong>ri kukutana na Bwana wao. Pale kulikuwa kungali kazi <strong>ya</strong><br />
mata<strong>ya</strong>risho itimizwe kwa ajili <strong>ya</strong>o. Kwa namna walipashwa kufuata kwa imani Kuhani wao<br />
mkubwa katika huduma <strong>ya</strong>ke, kazi mp<strong>ya</strong> zingeweza kufunuliwa. Ujumbe mwengine<br />
ulipashwa kutolewa kwa kanisa.<br />
Nani Atakayesimama?<br />
Nabii akasema: “Nani atakayevumilia siku <strong>ya</strong> kuja kwake? na nani atakayesimama wakati<br />
atakapoonekana? ... Naye atakaa kama mwenye kusafisha na kutakasa feza, naye atatakasa<br />
wana wa Lawi, na atawasafisha kama zahabu na feza, nao watatoa kwa Bwana sadaka kwa<br />
haki.” Malaki 3:2,3. Wale wanaokaa duniani wakati teteo <strong>ya</strong> Kristo <strong>ya</strong>takapoisha wanapashwa<br />
kusimama mbele <strong>ya</strong> Mungu bila muombezi. Mavazi <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong>napashwa kuwa safi bila doa, tabia<br />
zao zenye kutakaswa kutoka zambini kwa damu <strong>ya</strong> manyunyu. Kwa njia <strong>ya</strong> neema <strong>ya</strong> Mungu<br />
na juhudi <strong>ya</strong>o wenyewe <strong>ya</strong> utendaji wanapashwa kuwa washindaji katika vita na yule muovu.<br />
Wakati hukumu <strong>ya</strong> ukaguzi inapoendelea mbele kule mbinguni, wakati zambi za waamini<br />
waliotubu zinapoondolewa kutoka kwa Pahali patakatifu, hapo panapashwa kuwa na kazi <strong>ya</strong><br />
kipekee <strong>ya</strong> kuacha zambi miongoni mwa watu wa Mungu duniani. Kazi hii inaonyeshwa<br />
katika ujumbe wa Ufunuo 14. Wakati kazi hii itakapotimizwa, wafuasi wa Kristo watakuwa<br />
ta<strong>ya</strong>ri kwa kutokea kwake. Ndipo kanisa ambalo Bwana wetu kwa kuja kwake analopashwa<br />
kupokea litakuwa “kanisa la utukufu, pasipo doa wala kikunjo wala kitu cho chote kama hivi.”<br />
Waefeso 5:27.<br />
174