12.04.2023 Views

Kupinga ya Kiprotestanti

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />

juu <strong>ya</strong> kichwa cha mbuzi wa Azazeli, yeye katika mufano akahamisha zambi hizi zote kutoka<br />

kwake mwenyewe hata kwa mbuzi. Ndipo mbuzi akazichukua mbali, na ziliangaliwa kwamba<br />

zilitengwa milele kutoka kwa watu.<br />

Uhakika wa Mbinguni<br />

Kitu kilichotendwa katika mufano wa huduma <strong>ya</strong> Pahali patakatifu pa kidunia, inatendwa<br />

katika ukweli katika Pahali patakatifu pa mbinguni. Baada <strong>ya</strong> kupanda kwake mbinguni<br />

Mwokozi wetu akaanza kazi <strong>ya</strong>ke kama kuhani mkuu wetu: ” Kwa sababu Kristo hakuingia<br />

katika Pahali patakatifu palipofanywa kwa mikono, ndio mufano wa kweli, lakini aliingia<br />

mbinguni zenyewe, aonekane sasa mbele <strong>ya</strong> Mungu kwa ajili yetu.” Waebrania 9:24.<br />

Utumishi wa kuhani katika chumba cha kwanza, “ndani <strong>ya</strong> pazia” inayotenga Pahali<br />

patakatifu pa patakatifu kwa behewa (uwanja) <strong>ya</strong> inje, ni mufano wa kazi ambayo Kristo<br />

alianza kisha wakati alipo panda mbinguni. Kuhani katika utumishi wa kila siku akaonyesha<br />

mbele <strong>ya</strong> Mungu damu <strong>ya</strong> sadaka <strong>ya</strong> zambi, vilevile uvumba ambao unapanda pamoja na<br />

maombi <strong>ya</strong> wa Israeli. Kwa hivyo Kristo anaombea damu <strong>ya</strong>ke mbele <strong>ya</strong> Baba kwa ajili <strong>ya</strong><br />

wenye zambi na anaonyesha mbele <strong>ya</strong>ke, pamoja na manukato <strong>ya</strong> haki <strong>ya</strong>ke mwenyewe,<br />

maombi <strong>ya</strong> waamini waliotubu. Hiyo ndiyo iliyokuwa huduma katika chumba cha kwanza<br />

cha Pahali patakatifu katika mbingu.<br />

Huko imani <strong>ya</strong> wanafunzi wa Kristo wakamfuata wakati alipokuwa akipanda. Hapa<br />

matumaini <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong>likuwa, “tumaini gani tuliyo nayo kama nanga <strong>ya</strong> roho, yote mbili kweli na<br />

kuwa imara, na inayoingia ndani <strong>ya</strong> pazia, pahali alipoingia Yesu kwa ajili yetu, mutangulizi<br />

wetu, amekuwa kuhani mkubwa kwa milele.” “Kwa damu <strong>ya</strong>ke mwenyewe aliingia mara<br />

moja tu katika Pahali patakatifu alikwisha kupata ukombozi wa milele kwa ajili yetu.”<br />

Waebrania 6:19,20; 9:12.<br />

Kwa mda wa karne <strong>ya</strong> kumi na mnane kazi hii ikaendelea katika chumba cha kwanza cha<br />

Pahali patakatifu. Damu <strong>ya</strong> Kristo ikahakikisha rehema na ukubali wa Baba kwa ajili <strong>ya</strong><br />

waamini waliotubu, lakini zambi zao zingali zikidumu kwa vitabu v<strong>ya</strong> ukumbusho. Kama<br />

katika huduma <strong>ya</strong> mfano huko kulikuwa na kazi <strong>ya</strong> upatanisho kwa mwisho wa mwaka, kwa<br />

hivyo kabla <strong>ya</strong> kazi <strong>ya</strong> Kristo kwa ajili <strong>ya</strong> watu kumalizika kunakuwa kazi <strong>ya</strong> upatanisho kwa<br />

ajili <strong>ya</strong> ondoleo la zambi kwa Pahali patakatifu. Kazi hii ilianza wakati siku 2300<br />

zilipokwisha. Kwa wakati ule Kuhani wetu Mkubwa akaingia Pahali patakatifu pa patakatifu<br />

kwa kusafisha Pahali patakatifu.<br />

Kazi <strong>ya</strong> Hukumu<br />

Katika agano jip<strong>ya</strong> zambi za mwenye kutubu zinawekwa kwa imani juu <strong>ya</strong> Kristo na<br />

kuhamishwa kweli kwa Pahali patakatifu pa mbinguni. Na kama kusafishwa kwa mfano kwa<br />

Pahali patakatifu pa kudunia kulifanywa na ondoleo la zambi ambazo zilipachafua, vivyo<br />

hivyo utakaso wa sasa wa mbinguni unatimizwa kwa ondoleo, ao kufutwa, kwa zambi<br />

zilizoandikwa pale. Lakini kabla <strong>ya</strong> jambo hili kuweza kufanyika uchunguzi unapashwa<br />

172

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!