Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
<strong>ya</strong> mbinguni na ukombozi wa mwanadamu <strong>ya</strong>lifundishwa na Pahali patakatifu pa kidunia na<br />
huduma zake.<br />
Vyumba Viwili<br />
Nafasi takatifu za mahali patakatifu mbinguni zinafananishwa na vyumba viwili katika<br />
Pahali patakatifu duniani. Yohana alijaliwa na maono <strong>ya</strong> hekalu <strong>ya</strong> Mungu mbinguni.<br />
Alitazama kule “taa saba za moto ziliwaka mbele <strong>ya</strong> kiti cha enzi.” Aliona malaika “mwenye<br />
chungu cha zahabu <strong>ya</strong> uvumba; akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi <strong>ya</strong><br />
watakatifu wote juu <strong>ya</strong> mazabahu <strong>ya</strong> zahabu iliyo mbele <strong>ya</strong> kiti cha enzi.” Ufunuo 4:5; 8:3.<br />
Hapa nabii akaona chumba cha kwanza cha Pahali patakatifu pa mbinguni; na aliona “taa saba<br />
za moto” na “mazabahu <strong>ya</strong> zahabu”, iliyofananishwa kwa kinara cha zahabu na mazabahu <strong>ya</strong><br />
uvumba katika Pahali patakatifu pa dunia.<br />
Tena ‘’hekalu la Mungu likafunguliwa”, na akatazama ndani <strong>ya</strong> pazia juu <strong>ya</strong> patakatifu pa<br />
patakatifu. Na akaona “sanduku <strong>ya</strong> agano lake” la kufananishwa na sanduku lililojengwa na<br />
Musa kwa kuweka ndani amri <strong>ya</strong> Mungu. Ufunuo 11:19.<br />
Hivyo, wale wanaojifunza fundisho hili wakaone bila shaka kwamba hakika mbinguni<br />
kunakuwa hema. Musa alijenga hema <strong>ya</strong> kidunia akifuata mfano alioonyeshwa. Paulo<br />
anafundisha kuwa mfano ule ulikuwa hema <strong>ya</strong> kweli ambao unakuwa mbinguni. Na Yoane<br />
anashuhudia kwamba aliiona mbinguni.<br />
Ndani <strong>ya</strong> hekalu mbinguni, Pahali patakatifu pa patakatifu kunakuwa amri <strong>ya</strong> Mungu.<br />
Sanduku inayowekwa amri inafunikwa na kiti cha rehema, ambapo mbele <strong>ya</strong>ke Yesu anatetea<br />
mwenye zambi kwa ajili <strong>ya</strong> damu <strong>ya</strong>ke. Hapa ndipo kunafananishwa muungano wa haki na<br />
rehema katika mpango wa wokovu, muungano ambao unashangaza mbingu yote mzima. Hii<br />
ndiyo siri rehema ambamo malaika wanatamani kutazama vile Mungu anaweza kuwa<br />
mwenye haki wakati anahesabia haki mwenye zambi anayetubu.<br />
Kazi <strong>ya</strong> Kristo kama mutetezi wa binadamu, inafananishwa katika Zakaria: “Atajenga<br />
hekalu la Bwana; na atachukua utukufu, na atakaa na kutawala juu <strong>ya</strong> kiti chake cha enzi;<br />
naye atakuwa kuhani kwa enzi <strong>ya</strong>ke, na mshauri wa amani atakuwa katikati <strong>ya</strong>o wawili”.<br />
Zacharia 6:12,13.<br />
“Atajenga hekalu la Bwana”. Kwa zabihu <strong>ya</strong>ke na upatanisho, kristo ni msingi na mjengaji<br />
wa kanisa la Mungu, “jiwe kubwa la pembeni. Katika yeye jengo lote linaunganishwa vema<br />
na kukaa hata liwe hekalu takatifu katika Bwana”. Waefeso 2:20,21. “Atachukua utukufu”.<br />
Wimbo wa wale watakaonunuliwa utakuwa: “kwake yeye aliyetupenda na kutuosha zambi<br />
zetu kwa damu <strong>ya</strong>ke,...kwa yeye utukufu na uwezo hata milele na milele”. Ufunuo 1:5,6.<br />
Atakaa na kutawala juu <strong>ya</strong> kiti chake cha enzi; naye atakuwa kuhani juu <strong>ya</strong> kiti chake cha<br />
ufalme”. Ufalme wa utukufu haujaingiliwa bado. Mpaka kazi <strong>ya</strong>ke kama mpatanishi<br />
imalizike, ndipo Mungu atamtolea ufalme ambao “hautakuwa na mwisho” Luka 1:33. Kama<br />
169