Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Katika matengenezo adui zake wakashitakiwa maovu <strong>ya</strong> ushupavu juu <strong>ya</strong> wale waliokuwa<br />
wakiomba sana kukataa ushupavu. Mwendo wa namna ileile ulikuwa ukifuatwa na wapinzani<br />
wa kazi <strong>ya</strong> kiadventiste. Hawakutoshelewa na kuzidisha makosa <strong>ya</strong> ushupavu, wakaeneza<br />
taarifa ambazo hazikuwa hata na uhusiano kidogo wa kweli. Amani <strong>ya</strong>o ilikuwa ikisumbuliwa<br />
na kutangazwa kwa Kristo kuwa mlangoni. Waliogopa ingeweza kuwa kweli, huku<br />
wakatumaini kwamba haikuwako. Hii ilikuwa siri <strong>ya</strong> vita <strong>ya</strong>o kwa kupinga Waadventiste.<br />
Mahubiri <strong>ya</strong> ujumbe wa malaika wa kwanza <strong>ya</strong>lielekea mara kukomesha ushupavu. Wale<br />
walioshirikiana kwa kazi hizi kubwa walikuwa katika umoja; mioyo <strong>ya</strong>o ilijazwa na upendo<br />
wa mtu kwa mwenzake na kwa ajili <strong>ya</strong> Yesu, ambaye walimtazamia kumwona upesi. Imani<br />
moja, tumaini la baraka moja, wakahakikisha ngabo juu <strong>ya</strong> mashambulio <strong>ya</strong> Shetani.<br />
Kosa Linasahihishwa<br />
“Basi wakati bwana arusi alipokawia, wao wote wakasinzia na kulala usingizi. Lakini saa<br />
sita <strong>ya</strong> usiku kulikuwa kelele: Tazama bwana arusi anakuja! tokeni kukutana naye.” Katika<br />
wakati wa jua kali wa mwaka 1844 ujumbe ukatangazwa katika maneno <strong>ya</strong> Maandiko kabisa.<br />
Kile kilichoongoza kwa maendeleo ha<strong>ya</strong> kilikuwa ni uvumbuzi kwamba amri <strong>ya</strong> Artasasta<br />
kwa ajili <strong>ya</strong> kurudishwa kwa Yerusalema, ambayo ilisaidia kujua mwanzo wa hesabu <strong>ya</strong> siku<br />
2300, ikafanyika katika masika <strong>ya</strong> mwaka wa 457 B.C., na si kwa mwanzo wa mwaka, kama<br />
ilivyoaminiwa. Hesabu kutoka masika <strong>ya</strong> mwaka 457, miaka 2300 ikamalizika wakati wa<br />
masika <strong>ya</strong> mwaka 1844. Mifano <strong>ya</strong> Agano la Kale pia ilielekeza kwa wakati wa masika kama<br />
wakati ambao “kutakaswa kwa mahali patakatifu” kulipaswa kufanyika.<br />
Kuchinjwa kwa Kondoo wa Pasaka kulikuwa ni kivuli cha mauti <strong>ya</strong> Kristo, mfano<br />
ulitimilika, si kwa tukio tu, bali na kwa wakati. Kwa siku <strong>ya</strong> kumi na ine <strong>ya</strong> mwezi wa kwanza<br />
wa Wayuda, siku ile kabisa na mwezi ambapo kwa karne nyingi kondoo wa Pasaka alikuwa<br />
akichinjwa, Kristo akaanzisha karamu hiyo ambayo ilikuwa kwa kukumbuka mauti <strong>ya</strong>ke<br />
mwenyewe “Mwana-kondoo wa Mungu.” Kwa usiku uleule akakamatwa kwa kusulibiwa na<br />
kuuawa.<br />
UNABII WA 2300 SIKU / MIAKA<br />
161