Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Wahuduma, ambao kama walinzi walipashwa kuwa wa kwanza kutambua dalili za kuja<br />
kwa Yesu, walishindwa kujifunza ukweli kutoka kwa manabii ao kwa ishara za wakati.<br />
Upendo kwa Mungu na imani katika Neno lake vikapunguka, na mafundisho juu <strong>ya</strong> kurudi<br />
kwa kristo ikaamsha tu kutokuamini kwao. Kama kwa zamani ushuhuda wa Neno la Mungu<br />
ukakutana na swali: “Nani katika wakubwa ao Wafarisayo aliyemwamini?” Yoane 7:48.<br />
Wengi walipinga majifunzo <strong>ya</strong> unabii, kufundisha kwamba vitabu v<strong>ya</strong> unabii vilitiwa muhuri<br />
na havikuwa v<strong>ya</strong> kufahamika. Makundi, kwa kutumainia wachungaji wao, wakakataa<br />
kusikiliza; na wengine, ingawa walisadikishwa na ukweli, hawakusubutu kukiri ili wasipate<br />
“kutoshzwa katika sunagogi.” Yoane 9:22. Ujumbe Mungu alioutuma kwa kujaribu kanisa<br />
ulionyesha namna gani watu walikuwa wengi waliotia mapendo <strong>ya</strong>o kwa dunia hii kuliko kwa<br />
Kristo.<br />
Kukataa maonyo <strong>ya</strong> malaika wa kwanza kulisababisha na hali <strong>ya</strong> kutisha <strong>ya</strong> tabia <strong>ya</strong><br />
kupenda anasa <strong>ya</strong> kidunia, kuacha dini, na mauti <strong>ya</strong> kiroho ambayo <strong>ya</strong>likuwa katika makanisa<br />
katika mwaka 1844.<br />
Ujumbe wa Malaika wa Pili<br />
Katika Ufunuo 14 malaika wa kwanza amefuatwa na wa pili, kutangaza, “Umeanguka,<br />
umeanguka, Babeli mji ule mkubwa, kwani umefan<strong>ya</strong> mataifa yote kunywa mvinyo <strong>ya</strong> gazabu<br />
<strong>ya</strong> uasherati wake.” Ufunuo 14:8. Neno “Babeli” lilitoka kwa “Babel,” na maana <strong>ya</strong>ke ni<br />
machafuko. Katika Maandiko inaonyesha namna mbalimbali <strong>ya</strong> dini <strong>ya</strong> uongo ao ukufuru wa<br />
dini. Katika Ufunuo 17 Babeli inafananishwa kama mwanamke--mfano uliotumiwa katika<br />
Biblia kama mfano wa kanisa, mwanamke mwema hufananishwa na kanisa safi; mwanamke<br />
mwovu ni kama kanisa lililokufuru.<br />
Katika Biblia ushirika kati <strong>ya</strong> Kristo na kanisa lake unafananishwa na ndoa. Bwana<br />
anasema: “Na nitakuoa kuwa wangu kwa milele, ndiyo, nitakuoa kwa haki.” “Mimi ni mme<br />
wenu.” Na Paulo anasema: “Niliwapatanisha ninyi kwa mme mmoja, ili niletee Kristo bikira<br />
safi.” Hosea 2:19; Yeremia 3:14; 2 Wakorinto 11:2.<br />
Uzinzi wa Kiroho<br />
Kanisa, Kutokuwa na uaminifu kwa Kristo katika kuruhusu mambo <strong>ya</strong> kidunia kutawala<br />
moyo ni kama kuvunja kwa kiapo <strong>ya</strong> ndoa. Zambi <strong>ya</strong> Israeli katika kumwacha Bwana<br />
inaonyeshwa chini <strong>ya</strong> mfano huu. “Kama vile mke anavyoacha mme wake kwa udanganyifu,<br />
ndivyo mulivyonitendea mimi kwa udanganyifu, Ee nyumba <strong>ya</strong> Israeli, anasema Bwana.”<br />
“Mke wa kufan<strong>ya</strong> uasherati! anayekaribisha wageni pahali pa mme wake!” Yeremia 3:20;<br />
Ezekieli 16:32.<br />
Asema mtume Yakobo: “Ninyi wazini, hamujui <strong>ya</strong> kwamba kuwa rafiki <strong>ya</strong> dunia ni kuwa<br />
adui <strong>ya</strong> Mungu? Basi kila mtu anayetaka kuwa rafiki <strong>ya</strong> dunia anageuka kuwa adui <strong>ya</strong><br />
Mungu.” Yakobo 4:4.<br />
154