Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
kungali Wa<strong>ya</strong>hudi, wajinga ambao hawakujua tabia na kazi <strong>ya</strong> Kristo. Na watoto<br />
hawakufurahia nuru ambayo wazazi wao waliikataa kwa zarau katika mahubiri <strong>ya</strong> mitume,<br />
Mungu aliwezesha nuru kuangaza juu <strong>ya</strong>o. Waliona namna gani unabii ulitimia, si katika<br />
kuzaliwa tu na maisha <strong>ya</strong> Kristo, bali katika kifo chake na ufufuo. Watoto hawakuhukumiwa<br />
kwa ajili <strong>ya</strong> zambi za wazazi; lakini wakati walipokataa nuru ingine waliopewa, wakawa<br />
washiriki wa zambi za wazazi na wakajaza kipimo cha uovu wao.<br />
Wa<strong>ya</strong>hudi katika ugumu wa mioyo <strong>ya</strong>o wakakataa shauri la mwisho la rehema. Ndipo<br />
Mungu akaondoa ulinzi wake kwao. Taifa likaachwa kwa utawala wa mwongozi lililo<br />
mchagua. Shetani akaamsha tamaa kali sana na mba<strong>ya</strong> kuliko za roho. Watu wakakosa akili<br />
wakatawaliwa na nguvu na hasira <strong>ya</strong> upofu, <strong>ya</strong> shetani katika ukaidi wao. Marafiki na ndugu<br />
wakasalitiana wao kwa wao. Wazazi wakaua watoto wao, na watoto wazazi wao. Watawala<br />
hawakuwa na uwezo wa kujitawala wao wenyewe. Tamaa ikawafan<strong>ya</strong> kuwa wajeuri.<br />
Wa<strong>ya</strong>hudi wakakubali ushuhuda wa uwongo kwa kuhukumu Mwana wa Mungu asiye na<br />
kosa. Sasa mashitaki <strong>ya</strong> uwongo <strong>ya</strong>kafan<strong>ya</strong> maisha <strong>ya</strong>o kuwa si <strong>ya</strong> haki. Kuogopa Mungu<br />
hakukuwashitusha tena. Shetani alikuwa akiongoza taifa.<br />
Waongozi wa makundi <strong>ya</strong> upinzani wakaanguka mmoja juu za mwingine na kuwa bila<br />
huruma. Hata utakatifu wa hekalu haukuweza kuzuia ukali wao wa kutisha. Mahali patakatifu<br />
pakanajisiwa na miili <strong>ya</strong> waliouawa. Lakini washawishi wa kazi hii <strong>ya</strong> kishetani walitangaza<br />
kwamba hawakuwa na hofu yo yote kwamba Yerusalema ingeharibiwa! Ulikuwa mji wa<br />
Mungu. Hata wakati majeshi <strong>ya</strong> Waroma walipozunguka hekalu, makundi <strong>ya</strong>lisimama imara<br />
kwa wazo kwamba Aliye juu angejitia kati kwa kushinda kwa maadui wao. Lakini Israeli<br />
alitupia mbali ulinzi wa Mungu, na sasa hakuwa na ulinzi.<br />
Alama za Musiba<br />
Unabii uliyotolewa na Kristo kwa ajili <strong>ya</strong> uharibifu wa Yerusalema <strong>ya</strong>litimia wazi wazi.<br />
Dalili na maajabu <strong>ya</strong>litokea. Kwa muda wa miaka saba mtu aliendelea kupanda na kutelemuka<br />
katika njia za Yerusalema, kutangaza misiba itakayokuja. Kiumbe hiki cha ajabu kilifungwa<br />
gerezani na kuazibiwa, lakini kwa matusi maba<strong>ya</strong> hayo akajibu tu, “Ole, ole kwa<br />
Yerusalema”! Aliuawa katika mitego <strong>ya</strong> maadui aliyotabiri.<br />
“Hakuna Mkristo hata mmoja aliyeangamia katika uharibifu wa Yerusalema. Baada <strong>ya</strong><br />
Waroma chini <strong>ya</strong> uongozi wa Cestius walipozunguka mji, kwa gafula wakaacha mazingiwa<br />
wakati kila kitu kilionekana kuwa cha kufaa kwa shambulio. Mkuu wa Roma akaondoa<br />
majeshi <strong>ya</strong>ke bila sababu ndogo wazi. Alama iliyoahidiwa ilitolewa kwa Wakristo waliokuwa<br />
wakingojea. Luka 21:20,21.<br />
Mambo <strong>ya</strong>kafanyika kwa namna ambayo hata Wa<strong>ya</strong>hudi ama Waroma hawakupinga<br />
kukimbia kwa Wakristo. Katika kushindwa kwa Cestius, Wa<strong>ya</strong>hudi wakafuata, na wakati<br />
majeshi hayo mawili <strong>ya</strong>lipokutana, Wakristo popote katika inchi waliweza kufan<strong>ya</strong> kimbilio<br />
lao bila kusumbuliwa mahali pa salama, kwa mji wa Pella.<br />
8