12.04.2023 Views

Kupinga ya Kiprotestanti

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />

Sura 20. Upendo kwa Ajili <strong>ya</strong> Kuja kwa Kristo<br />

6 Uamsho mkubwa wa dini umetabiriwa katika ujumbe wa malaika wa kwanza wa Ufunuo<br />

14. Malaika moja ameonekana akiruka “katikati <strong>ya</strong> mbingu, mwenye Habari Njema <strong>ya</strong> milele,<br />

ahubiri kwao wanaokaa juu <strong>ya</strong> dunia, na kila taifa na kabila na lugha na jamaa.” “Kwa sauti<br />

kubwa” akatangaza: “Ogopeni Mungu, na kumutukuza kwa maana saa <strong>ya</strong> hukumu <strong>ya</strong>ke<br />

imekuja. Mukamwabudu yeye aliyefan<strong>ya</strong> mbingu na dunia na bahari na chemchemi za maji.”<br />

Ufunuo 14:6,7.<br />

Malaika ni mfano wa tabia bora <strong>ya</strong> kazi inayopaswa kutimizwa kwa ujumbe na uwezo na<br />

utukufu, ambavyo vinapaswa kuishugulikia. Kuruka kwa malaika “katikati <strong>ya</strong> Mbingu,”<br />

“sauti kubwa,” na matangazo <strong>ya</strong>ke “kwa kila taifa na kabila na lugha na jamaa” inatoa<br />

ushuhuda wa kuenea kwa upesi, katika dunia nzima kwa tendo. Kwa habari <strong>ya</strong> wakati ambao<br />

inapaswa kufanyika, inatangaza kufunguliwa kwa hukumu.<br />

Ujumbe huu ni sehemu <strong>ya</strong> habari njema (injili) ambayo ingeweza kutangazwa tu katika<br />

siku za mwisho, ambapo tu ndipo inaweza kuwa hatika kwamba saa <strong>ya</strong> hukumu <strong>ya</strong>ke imekuja.<br />

Sehemu ile <strong>ya</strong> unabii wake ambao inaelekea kwa siku za mwisho, Danieli aliagizwa kufunga<br />

na kutia muhuri “hata wakati wa mwisho.” Danieli 12:4. Mpaka wakati huu ndipo ujumbe juu<br />

<strong>ya</strong> hukumu utangazwe, wenye msingi na kutimilika kwa unabii.<br />

Paulo alion<strong>ya</strong> kanisa lisitazamie kuja kwa Kristo katika siku zake. Mpaka baada <strong>ya</strong> uasi<br />

mkubwa na utawala mrefu wa “mtu wa zambi” tunaweza kutazamia kuja kwa Bwana wetu.<br />

Tazama 2 Watesalonika 2:3. “Mtu wa zambi” vilevile “siri <strong>ya</strong> uasi,” “mwana wa uharibifu,”<br />

na “yule mwenye uovu,” ni mfano wa cheo cha Papa, ambacho kilikuwa kwa kushikilia<br />

mamlaka <strong>ya</strong>ke kwa miaka 1260. Mda huu ulimalizika kwa mwaka 1798. Kuja kwa Kristo<br />

hakungefanyika mbele <strong>ya</strong> wakati ule. Paulo anaeneza onyo lake kwa ile inayohusu Wakristo<br />

wote hata kwa mwaka 1798. Kwa upande huu wa wakati ule, ujumbe wa Kuja kwa Kristo<br />

mara <strong>ya</strong> pili ukatangazwa. Sivyo ujumbe wa namna ile haujatolewa kamwe kwa vizazi<br />

vilivyopita. Paulo, kama tulivyoona, hakuuhubiri; aliuweka mbali kwa wakati ujao ujumbe<br />

wa kuja kwa Bwana. Watengenezaji hawakuutangaza. Martin Luther aliweka siku <strong>ya</strong> hukumu<br />

karibu <strong>ya</strong> miaka 300 zijazo kutoka kwa siku zake. Lakini tangu 1798 kitabu cha Danieli<br />

kilifunuliwa, na wengi wakatangaza ujumbe wa hukumu kuwa karibu.<br />

Katika Inchi Mbalimbali kwa Wakati Moja<br />

Kama Matengenezo <strong>ya</strong> karne <strong>ya</strong> kumi na sita, Mwendo (kazi), la Kuja kwa Yesu<br />

likaonekana katika inchi mbalimbali kwa wakati moja. Watu wa imani wakaongozwa<br />

kujifunza mambo <strong>ya</strong> unabii na wakaona ushuhuda wa kusadikisha kwamba mwisho ulikuwa<br />

karibu. Makundi mbali mbali <strong>ya</strong> Wakristo, kwa kujifunza Maandiko tu, wakafikia kwa<br />

kuamini kwamba kuja kwa Mwokozi kulikuwa karibu.<br />

144

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!