Kupinga ya Kiprotestanti

newcovenantpublicationsintl
from newcovenantpublicationsintl More from this publisher
12.04.2023 Views

Kupinga ya Kiprotestanti chache tu mbele ya kutimilika kwake akaandika: “Itamalizika kwa tarehe 11 ya Agosti, 1840, wakati mamlaka ya Ottoman katika Constantinople kuweza kutazamiwa kuvunjika.” Maonyo Yalitimilika Kwa wakati kabisa uliotajwa, Turkey ilikubali ulinzi wa mamlaka za mapatano ya Ulaya na kwa hivyo ikajitia yenyewe chini ya utawala wa mataifa ya Kikristo. Jambo kwa halisi kweli likatimiliza ukashiri. (Tazama Nyongezo.) Watu wengi walisadikishwa na kanuni za maelezo ya unabii yaliyokubaliwa na Miller na wafuasi wake. Watu wenye elimu na cheo wakajiunga pamoja na Miller katika kuhubiri na kutangaza maonyo yake. Tangu 1840 hata 1844 kazi ikaenea kwa upesi. William Miller alikuwa na akili za kichwa cha nguvu, na akaongeza kwa haya hekima ya mbinguni kwa kujiunga mwenyewe na Chemchemi ya hekima. Aliamuru heshima po pote, ukamilifu na tabia njema vilitumiwa. Kwa damani unyenyekevu wa Kikristo, alikuwa muangalifu na mpole kwa wote, tayari kusikiliza wengine na kupima mabishano yao. Alijaribu maelezo yote kwa Neno la Mungu, na mawazo yake halisi na maarifa ya Maandiko vikamwezesha kukanusha makosa. Lakini, kama pamoja na Watengenezaji wa kwanza, kweli alizoonyesha hazikukubaliwa na walimu wengi wa dini. Kwa hivyo hawa hawakuweza kudumisha hali yao kwa Maandiko, wakarejea kwa mafundisho ya watu, haya kiasili cha Wababa. Lakini Neno la Mungu lilikuwa ni ushuhuda pekee uliokubaliwa na wahubiri wa kweli wa kuja kwa Yesu. Cheko na zarau vilitumiwa kwa upande wa adui katika kusingizia wale waliotazamia kwa furaha juu ya kurudi kwa Bwana wao na walikuwa wakijitahidi kuishi maisha takatifu na kutayarisha wengine kwa kuonekana kwake. Ilifanyika kuonyesha zambi kwa kujifunza mambo ya unabii wa kuja kwa Kristo na mwisho wa dunia. Kwa hivyo kazi ya mapadri wa watu wengi ikapunguza imani katika Neno la Mungu. Mafundisho yao yakafanya watu kuwa watu kutokuwa Waaminifu, na wengi wakajiruhusu kwa kutembea kwa tamaa mbaya. Halafu watenda maovu wakayaweka yote juu ya Waadventisti. Ingawa Miller akavuta makundi ya wasikilizi wenye akili, jina lake lilitajwa kwa shida na magazeti ya dini isipokuwa tu kwa cheko ao mashitaki. Waovu, waliposukumwa na walimu wa dini, wakakimbilia kwa mabisho ya matukano juu yake na kazi yake. Mzee huyu mwenye imvi aliyeacha makao yake ya kupendeza kwa kusafiri kwa garama yake mwenyewe kuletea dunia onyo kubwa la hukumu inayokaribia akasitakiwa kama upumbavu. Usikivu na Kutokuamini Usikivu ukaendelea kuongezeka. Kutoka kwa makumi mawili na mamia, makutano yakaongezeka kwa maelfu mengi. Lakini baada ya wakati, upinzani ulionekana juu ya hawa waliogeuka, makanisa yakaanza kuchukua hatua za kutiisha kwa wale waliokubali maoni ya Miller. Jambo hili likaita jibu kwa kalamu yake: “Kama tunakuwa wakosefu ninawaomba mtuonyeshe kwa namna gani kosa letu linakuwa kutoka katika neno la Mungu; tulichekwa ya 136

Kupinga ya Kiprotestanti kutosha; na ile haiwezi kutusadikisha kwamba tunakuwa katika kosa; Neno la Mungu pekee linaweza kugeuza maoni yetu. Hukumu yetu ilifanyika kwa kusudi pamoja na maombi, kama tulivyoona ushuhuda katika Maandiko.” Wakati uovu wambele ya garika ulipomsukuma Mungu kuleta garika duniani, kwanza akawajulisha kusudi lake. Kwa miaka 120 likasikiwa onyo kwa kutubu. Lakini hawakuliamini. Wakazarau mjumbe wa Mungu. Kama ujumbe wa Noa ulikuwa wa kweli, sababu gani watu wote wa dunia hawakuuona na kuuamini? Tendo la kudai haki la mtu mmoja kupinga hekima ya maelfu! Hawakuweza kuamini onyo wala kutafuta kimbilio ndani ya safina. Watu wa zarau wakaonyesha kwa mwandamano usiobadilika wa majira, mbingu za rangi ya samawi zisizonyesha mvua kamwe. Katika zarau wakatangaza mhubiri wa haki kama mwenye juhudi ya kishenzi. Wakaenda zao, kujikaza zaidi kwa njia zao mbovu kuliko mbele. Lakini kwa wakati uliotajwa Hukumu za Mungu zikaanguka juu ya waliokataa huruma yake. Wenye Mashaka na Wasioamini Kristo alisema kwamba kama vile watu wa siku za Noa “hawakujua hata garika ilipokuja na kuwaondosha wote; ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa Mwana wa watu.” Matayo 24:39. Wakati watu wanaojidai kuwa watu wa Mungu wanapojiunga pamoja na dunia, wakati anasa ya dunia inakuwa anasa ya kanisa, wakati wote wanapotazamia miaka nyingi ya mafanikio ya kidunia--ndipo, kwa gafula kama nuru ya umeme, utakuja mwisho wa matumaini yao ya uongo. Kama vile Mungu alivyotuma mtumishi wake kwa kuonya dunia juu ya kuja kwa Garika, ndivyo alivyotuma wajumbe waliochaguliwa kujulisha ukaribu wa hukumu ya mwisho. Na kama watu wa wakati wa Noa walichekelea kwa kuzarau ubashiri wa muhubiri wa haki, ndivyo hivyo katika siku za Miller wengi kati ya wale wanaojidai kuwa watu wa Mungu wakachekelea maneno ya maonyo. Hapo hapakuwa tena na ushahidi wa mwisho wakuonyesha kwamba makanisa yalitoka kwa Mungu kuliko machukio yaliyoamshwa na ujumbe huu uliotumwa na Mungu. Wale waliokubali mafundisho ya kuja waliona kwamba ilikuwa wakati wa kukamata msimamo. “Mambo ya umilele yakawa kwao kitu cha kweli. Mbingu ililetwa karibu, na walijiona wao wenyewe kuwa na kosa mbele za Mungu.” Wakristo walifanywa kuona kwamba wakati ulikuwa karibu, mambo walipashwa kutendea wenzao yalipaswa kufanywa kwa upesi. Umilele ulionekana kufunguliwa mbele yao. Roho wa Mungu alitoa uwezo kwa miito yao kujitayarisha kwa ajili ya siku ya Mungu. Maisha yao ya siku kwa siku ilikuwa mi laumu kwa washiriki wa kanisa wasiotakaswa. Hawa hawakutaka kusumbuliwa katika furaha yao, kutafuta feza, na tamaa ya nguvu kwa ajili ya heshima ya kidunia. Ndipo wakapinga imani ya kiadventisti. Wapinzani wakajitahidi kupinga uchunguzi kwa kufundisha kwamba mambo ya unabii yalitiwa muhuri. Kwa hiyo Waprotestanti wakafuata nyayo za washiriki wa kanisa la Roma. 137

<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />

kutosha; na ile haiwezi kutusadikisha kwamba tunakuwa katika kosa; Neno la Mungu pekee<br />

linaweza kugeuza maoni yetu. Hukumu yetu ilifanyika kwa kusudi pamoja na maombi, kama<br />

tulivyoona ushuhuda katika Maandiko.”<br />

Wakati uovu wambele <strong>ya</strong> garika ulipomsukuma Mungu kuleta garika duniani, kwanza<br />

akawajulisha kusudi lake. Kwa miaka 120 likasikiwa onyo kwa kutubu. Lakini<br />

hawakuliamini. Wakazarau mjumbe wa Mungu. Kama ujumbe wa Noa ulikuwa wa kweli,<br />

sababu gani watu wote wa dunia hawakuuona na kuuamini? Tendo la kudai haki la mtu mmoja<br />

kupinga hekima <strong>ya</strong> maelfu! Hawakuweza kuamini onyo wala kutafuta kimbilio ndani <strong>ya</strong><br />

safina.<br />

Watu wa zarau wakaonyesha kwa mwandamano usiobadilika wa majira, mbingu za rangi<br />

<strong>ya</strong> samawi zisizonyesha mvua kamwe. Katika zarau wakatangaza mhubiri wa haki kama<br />

mwenye juhudi <strong>ya</strong> kishenzi. Wakaenda zao, kujikaza zaidi kwa njia zao mbovu kuliko mbele.<br />

Lakini kwa wakati uliotajwa Hukumu za Mungu zikaanguka juu <strong>ya</strong> waliokataa huruma <strong>ya</strong>ke.<br />

Wenye Mashaka na Wasioamini<br />

Kristo alisema kwamba kama vile watu wa siku za Noa “hawakujua hata garika ilipokuja<br />

na kuwaondosha wote; ndivyo kutakavyokuwa kuja kwa Mwana wa watu.” Matayo 24:39.<br />

Wakati watu wanaojidai kuwa watu wa Mungu wanapojiunga pamoja na dunia, wakati anasa<br />

<strong>ya</strong> dunia inakuwa anasa <strong>ya</strong> kanisa, wakati wote wanapotazamia miaka nyingi <strong>ya</strong> mafanikio<br />

<strong>ya</strong> kidunia--ndipo, kwa gafula kama nuru <strong>ya</strong> umeme, utakuja mwisho wa matumaini <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong><br />

uongo. Kama vile Mungu alivyotuma mtumishi wake kwa kuon<strong>ya</strong> dunia juu <strong>ya</strong> kuja kwa<br />

Garika, ndivyo alivyotuma wajumbe waliochaguliwa kujulisha ukaribu wa hukumu <strong>ya</strong><br />

mwisho. Na kama watu wa wakati wa Noa walichekelea kwa kuzarau ubashiri wa muhubiri<br />

wa haki, ndivyo hivyo katika siku za Miller wengi kati <strong>ya</strong> wale wanaojidai kuwa watu wa<br />

Mungu wakachekelea maneno <strong>ya</strong> maonyo.<br />

Hapo hapakuwa tena na ushahidi wa mwisho wakuonyesha kwamba makanisa <strong>ya</strong>litoka<br />

kwa Mungu kuliko machukio <strong>ya</strong>liyoamshwa na ujumbe huu uliotumwa na Mungu. Wale<br />

waliokubali mafundisho <strong>ya</strong> kuja waliona kwamba ilikuwa wakati wa kukamata msimamo.<br />

“Mambo <strong>ya</strong> umilele <strong>ya</strong>kawa kwao kitu cha kweli. Mbingu ililetwa karibu, na walijiona wao<br />

wenyewe kuwa na kosa mbele za Mungu.”<br />

Wakristo walifanywa kuona kwamba wakati ulikuwa karibu, mambo walipashwa<br />

kutendea wenzao <strong>ya</strong>lipaswa kufanywa kwa upesi. Umilele ulionekana kufunguliwa mbele<br />

<strong>ya</strong>o. Roho wa Mungu alitoa uwezo kwa miito <strong>ya</strong>o kujita<strong>ya</strong>risha kwa ajili <strong>ya</strong> siku <strong>ya</strong> Mungu.<br />

Maisha <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong> siku kwa siku ilikuwa mi laumu kwa washiriki wa kanisa wasiotakaswa. Hawa<br />

hawakutaka kusumbuliwa katika furaha <strong>ya</strong>o, kutafuta feza, na tamaa <strong>ya</strong> nguvu kwa ajili <strong>ya</strong><br />

heshima <strong>ya</strong> kidunia. Ndipo wakapinga imani <strong>ya</strong> kiadventisti.<br />

Wapinzani wakajitahidi kupinga uchunguzi kwa kufundisha kwamba mambo <strong>ya</strong> unabii<br />

<strong>ya</strong>litiwa muhuri. Kwa hiyo Waprotestanti wakafuata n<strong>ya</strong>yo za washiriki wa kanisa la Roma.<br />

137

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!