You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Kristo” lilikuwa “tumaini la baraka.” Tito 2:13. Paulo alionyesha kwamba ufufuo utafika<br />
wakati wa kurudi kwa Mwokozi, wakati waliokufa katika Kristo * watakapofufuka, na<br />
pamoja na wahai kuchukuliwa juu kukutana na Bwana katika mawingu. “Na hivi” akasema,<br />
“tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi mufarijiane kwa maneno ha<strong>ya</strong>.” 1 Watesalonika<br />
4:17.<br />
Kule Patemo mwanafunzi mpendwa akasikia ahadi, “Ndiyo: ninakuja upesi.” Na jibu lake<br />
linasimamia ombi la kanisa. “Amina, kuja Bwana Yesu.” Ufunuo 22:20. Kati <strong>ya</strong> gereza,<br />
kigingi, mahali wanaponyongwa kwa sheria, pahali watakatifu na wafia dini waliposhuhudia<br />
kwa ajili <strong>ya</strong> kweli, kutoka kwa karne nyingi za usemi wa imani <strong>ya</strong>o na tumaini.”<br />
Walipohakikishwa na ufufuo wa Yesu mwenyewe, na baadaye ufufuo wao wenyewe wakati<br />
wa kuja kwake, kwa sababu hii, “akasema mmojawapo wa Wakristo hawa,” walizarau mauti,<br />
na wakapatikana kuwa juu <strong>ya</strong>ke, wa Waldenses walitunzaimani ile ile, Wyccliffe, Luther,<br />
Calvin, Knox, Ridley, na Baxter walitazamia kwa imani kurudi kwa Bwana. Ndiyo iliyokuwa<br />
tumaini la kanisa la mitume, la “kanisa katika jangwa,” na la Watengenezaji.<br />
Unabii hautabiri tu namna na kusudi la kuja kwa Kristo mara <strong>ya</strong> pili, bali huonyesha ishara<br />
ambazo watu wanapashwa kujua wakati siku ile inapokaribia. “Na kutakuwa na ishara katika<br />
jua na mwezi na nyota.” Luka 21:25. “...jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa nuru <strong>ya</strong>ke, na<br />
nyota za mbingu zitaanguka, na nguvu zilizo mbinguni zitatikisika. Na wakati ule wataona<br />
Mwana wa watu akikuja katika mawingu pamoja na uwezo kubwa na utukufu.” Marko 13:24-<br />
26.<br />
Muonyeshaji (nabii) basi anaonyesha mojawapo wa ishara zitakazo tangulia kuja kwa<br />
mara <strong>ya</strong> pili: “... tazama, palikuwa na tetemeko kubwa la inchi, jua likakuwa jeusi kama gunia<br />
la manyo<strong>ya</strong>, na mwezi wote ukakuwa kama damu.” Ufunuo 6:12.<br />
Tetemeko la inchi lililotikisa Ulimwengu<br />
Kwa kutimilika kwa unabii huu kulitokea katika mwaka 1755 tetemeko la inchi lililokuwa<br />
la kutisha zaidi lililoandikwa. Lilijulikana kama tetemeko la inchi la Lisbon, likaenea Ula<strong>ya</strong>,<br />
Afrika, na Amerika. Likasikiwa Groenland, Upande wa Magharibi <strong>ya</strong> Uhindi, katika Antilles,<br />
Norvege na Swede, Uingereza na Irland, kwa eneo si chini kuliko kilometres milioni ine kwa<br />
mraba. Katika Afrika mshindo ulikuwa karibu sana wa nguvu kama katika Ula<strong>ya</strong>. Sehemu<br />
Kubwa <strong>ya</strong> Algiers (Mji mkuu wa Algeria) ikaharibiwa. Wimbi kubwa la kutisha likazamisha<br />
pwani <strong>ya</strong> Espagne na <strong>ya</strong> Afrika na kudidimiisha miji.<br />
Milima, “ingine katika milima inayo kuwa kubwa sana katika Portugal, ikatikiswa kwa<br />
nguvu sana, tangu kwa misingi <strong>ya</strong>o; na ingine kati <strong>ya</strong>o ikafunguka kwa vilele v<strong>ya</strong>o, ambayo<br />
ilipasuka na kutengana kwa namna <strong>ya</strong> ajabu, mafungu makubwa <strong>ya</strong>o kutupwa katika mabonde<br />
<strong>ya</strong> karibu. Ndimi za moto imehadiziwa kutoka kwa milima hizo.”<br />
Huko Lisbon “Sauti <strong>ya</strong> ngurumo ilisikiwa chini <strong>ya</strong> udongo, na bila kukawia baadae<br />
kishindo kikali kikaangusha sehemu kubwa <strong>ya</strong> mji ule. Katika mwendo wa dakika karibu sita<br />
120