Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
angeweza kuamuru shauri fulani ao imani leo na ingine kesho; kama ilivyokuwa ikifanyika<br />
katika Uingereza na wafalme wa kuachana na wamalkia, na mapapa wa kuachana na<br />
mabaraza katika Kanisa la Roma.”<br />
Kuhuzuria katika kanisa lililosimamishwa ililazimishwa chini <strong>ya</strong> malipo ao kifungo.<br />
“Kushurutisha watu kuungana pamoja na wale wa imani <strong>ya</strong> kuachana, yeye (Williams)<br />
aliangalia jambo hilo kama kutendea zambi kwa wazi kwa haki zao halisi, kukokota watu<br />
wasio kuwa wa dini kwa ibada na wasiopenda, ilikuwa ni kukuza unafiki... Hakuna mutu<br />
alipashwa kulazimishwa kuabudu Mungu, ao, akaongeza, kushikilia ibada, kinyume cha<br />
ukubali wake mwenyewe!”<br />
Roger Williams aliheshimiwa, lakini haja <strong>ya</strong>ke kwa ajili <strong>ya</strong> uhuru wa dini haukuweza<br />
kuvumiliwa. Kwa kuepuka kufungwa akalazimishwa kukimbilia kati kati <strong>ya</strong> baridi ng zoruba<br />
<strong>ya</strong> majira <strong>ya</strong> baridi katika poli usiokatwa bado.<br />
“Kwa muda wa majuma kumi na inne,” akasema, “Nikarushwa sana katika majira <strong>ya</strong><br />
uchungu, bila kuwa na mkate ao kitanda.” Lakini “Kunguru wakanilisha jangwani,” shimo<br />
ndani <strong>ya</strong> mti nikaitumia mara kwa mara kuwa ficho.” Akaendelea na ukimbizi wake wa<br />
uchungu katika theluji na mwitu usio na njia hata akapata kimbilio pamoja na kabila la<br />
Wahindi ambao aliopata matumaini na upendo wao.<br />
Akaweka msingi wa jimbo la kwanza la n<strong>ya</strong>kati za kisasa lile lililo tambua haki “kwamba<br />
kila mutu alipashwa kuwa na uhuru kwa kuabudu Mungu kufuatana na nuru <strong>ya</strong> zamiri <strong>ya</strong>ke<br />
mwenyewe.” Jimbo lake ndogo, Kisiwa cha Rhode, likaongezeka na kusitawi hata kwa kanuni<br />
zake za msingi--uhuru wa serekali na wa dini--vikawa mawe <strong>ya</strong> pembeni <strong>ya</strong> Jamuhuri <strong>ya</strong><br />
Amerika.<br />
Barua <strong>ya</strong> maagano wa Uhuru<br />
Tangazo la Amerika la Uhuru likatangazwa: “Tunashika kweli hizi kuwa zamiri binafsi,<br />
kwamba watu wote waliumbwa kuwa sawasawa; na kwamba Muumba aliwapa haki fulani<br />
zisizoondolewa; ambazo katika hizo kuna uzima, uhuru, na kutafuta furaha.” Serkali (<strong>ya</strong><br />
Amerika) iliahidi heshima <strong>ya</strong> zamiri: “Baraza kuu halitaweza kufan<strong>ya</strong> sheria hata moja<br />
inayosimamia kwa dini, ao inayokataza uhuru wa dini.”<br />
“Watengenezaji wa Serkali wakatambua kanuni <strong>ya</strong> milele kwamba uhusiano wa mtu na<br />
Mungu wake unakuwa juu <strong>ya</strong> sheria <strong>ya</strong> binadamu, na haki zake za zamiri <strong>ya</strong> daima... Ni<br />
kanuni <strong>ya</strong>kuliwa ambayo hakuna kitu kitakacho weza kuiondoa.”<br />
Habari ikaenezwa katika Ula<strong>ya</strong> kwamba kuna inchi ambapo kila mtu anaweza kufurahiwa<br />
matunda <strong>ya</strong> kazi <strong>ya</strong>ke na kutii zamiri <strong>ya</strong>ke. Maelfu wakasongana kwa pande za pwani za<br />
Dunia Mp<strong>ya</strong>. Katika miaka makumi mbili kutoka siku <strong>ya</strong> kufika mara <strong>ya</strong> kwanza huko<br />
Plymouth (1620), jinsi maelfu mengi <strong>ya</strong> Wasafiri walikaa katika Uingereza Mp<strong>ya</strong>.<br />
117