Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Sura 14. Ukweli Unaendelea Katika Uingereza<br />
Wakati Luther alipokuwa akifungua Biblia iliyofungwa kwa watu wa Ujeremamy,<br />
Tyndale akasukumwa na Roho wa Mungu kufan<strong>ya</strong> tendo lilelile katika Uingereza. Biblia <strong>ya</strong><br />
Wycliffe ilitafsiriwa kutoka kwa Kilatini, ambamo mulikuwa makosa mengi. Bei <strong>ya</strong> kurasa<br />
zilizoandikwa ilikuwa juu sana na kwa hiyo mtawanyiko wake ulikuwa wa shida.<br />
Kwa mwaka 1516, kwa mara <strong>ya</strong> kwanza Agano Jip<strong>ya</strong> likachapwa katika lugha <strong>ya</strong> asili <strong>ya</strong><br />
Kigiriki. Makosa mengi <strong>ya</strong> tafsiri <strong>ya</strong> kwanza <strong>ya</strong>kasahihishwa, na maana <strong>ya</strong>karudishwa vizuri<br />
zaidi. Nakala zile zikaletea watu waliojifunza ufahamu bora kwa kweli na zikatoa mwendo<br />
mp<strong>ya</strong> kwa kazi <strong>ya</strong> matengenezo. Lakini sehemu kubwa <strong>ya</strong> watu walikosa Neno la Mungu.<br />
Tyndale alipaswa kutimiza kazi <strong>ya</strong> Wycliffe katika kutoa Biblia kwa watu wa inchi <strong>ya</strong>ke.<br />
Akahubiri bila woga mambo <strong>ya</strong> hakika <strong>ya</strong>ke. Kwa tangazo la Papa kwamba ni kanisa<br />
lililotoa Biblia, na ni kanisa pekee linaloweza kuieleza, Tyndale akajibu: “Kamwe<br />
haukutupatia Maandiko, ni wewe uliye<strong>ya</strong>ficha kwetu; ni wewe uliyewachoma wale<br />
walio<strong>ya</strong>fundisha, na kama ungaliweza, ungalichoma Maandiko yenyewe.”<br />
Mahubiri <strong>ya</strong> Tyndale <strong>ya</strong>kaamsha usikizi kubwa. Lakini mapadri wakajitahidi kuharibu<br />
kazi <strong>ya</strong>ke. “Ni kitu gani kinapaswa kufanywa?” akapaza sauti. “Siwezi kuwa po pote. Ee!<br />
kama Wakristo wangalikuwa na Maandiko matakatifu katika lugha <strong>ya</strong>o wenyewe,<br />
wangaliweza wao wenyewe kushindana na wenye kutumia maneno madanganyifu hawa. Bila<br />
Biblia haiwezekani kuimarisha watu katika kweli.”<br />
Nia mp<strong>ya</strong> ikaja katika mawazo <strong>ya</strong>ke. “Injili haitasema lugha <strong>ya</strong> Ungereza miongoni<br />
mwetu? ... Kanisa linapaswa kuwa na nuru ndogo kwa wakati wa azuhuri kuliko wakati wa<br />
mapambazuko <strong>ya</strong>ke? ... Wakristo wanapashwa kusoma Agano Jip<strong>ya</strong> katika lugha <strong>ya</strong>o <strong>ya</strong><br />
kuzaliwa.” Ila tu kwa njia <strong>ya</strong> Biblia watu waliweza kufikia ukweli.<br />
Mtaalamu mmoja wa Katoliki katika mabishano pamoja naye akapaza sauti <strong>ya</strong> mshangao,<br />
“Ingekuwa vema kutokuwa na sheria za Mungu kuliko kukosa zile za Papa.” Tyndale akajibu,<br />
“Ninazarau Papa na sheria zake zote; na kama Mungu angenipatia maisha, kabla <strong>ya</strong> miaka<br />
mingi nitawezesha kijana anayeongoza jembe la kukokotwa na ngombe kufahamu Maandiko<br />
zaidi kuliko ninyi.”<br />
Tyndale Anatafsiri Agano Jip<strong>ya</strong> kwa Kiingereza<br />
Alipofukuzwa nyumbani kwa ajili <strong>ya</strong> mateso, akaenda Londoni na huko kwa mda<br />
akatumika bila kizuizi. Lakini tena Wakatoliki wakamlazimisha kukimbia. Uingereza wote<br />
ukaonekana wenye kufungwa kwake. Katika Ujeremani akaanza uchapaji wa Agano Jip<strong>ya</strong><br />
kwa lugha <strong>ya</strong> kingereza. Alipokatazwa kuchapa katika mji moja, akaenda kwa mji mwengine.<br />
Mwishowe akasafiri kwenda Worms, ambako, miaka michache mbele, Luther alipotetea injili<br />
mbele <strong>ya</strong> baraza. Katika mji ule kulikuwa rafiki wengi wa Matengenezo. Vitabu elfu tatu v<strong>ya</strong><br />
Agano Jip<strong>ya</strong> vikachapwa, na mchapo mwengine ukafuata.<br />
97