You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Kupinga</strong> <strong>ya</strong> <strong>Kiprotestanti</strong><br />
Sura 13. Katika Uholandi na Scandanavia<br />
Katika Uholandi ukali wa Papa ukaleta haraka upinzani. Miaka mia saba kabla <strong>ya</strong> Luther,<br />
askofu wa Roma kwa uhodari akashitakiwa na maaskofu wawili, waliotumwa kuwa mabalozi<br />
huko Roma, wakajifunza tabia <strong>ya</strong> kweli <strong>ya</strong> “jambo takatifu la askofu”; “Unakaa mwenyewe<br />
ndani <strong>ya</strong> hekalu la Mungu; baada <strong>ya</strong> mchungaji unakuwa mbwa mwitu kwa kondoo, ... lakini<br />
ulipashwa kuwa mtumishi wa watumishi, kama upendavyo kujiita mwenyewe, unatumaini<br />
kuwa bwana wa mabwana. ... Unaleta ha<strong>ya</strong> kwa amri za Mungu.”<br />
Wengine wakatokea katika karne zote kukariri kukataa huku. Biblia <strong>ya</strong> Wavaudois<br />
ilitafsiriwa katika lugha <strong>ya</strong> Kijeremani. Wakatangaza “kwamba hapo kulikuwa faida ndani<br />
<strong>ya</strong>ke; hakuna mizaha wala uongo, wala mambo <strong>ya</strong> michezo, wala udanganyifu, bali maneno<br />
<strong>ya</strong> kweli.” Ndivyo waliandika rafiki za imani <strong>ya</strong> zamani tangu karne <strong>ya</strong> kumi na mbili.<br />
Sasa wakati wa mateso <strong>ya</strong> kanisa la Roma ikaanza; lakini waaminifu wakaendelea<br />
kuongezeka, kutangaza kwamba Biblia ni mamlaka pekee <strong>ya</strong> haki katika dini na kwamba<br />
“hakuna mtu anayepashwa kushurutishwa kuamini, bali angepashwa kusadikishwa kwa njia<br />
<strong>ya</strong> mahubiri.”<br />
Mafundisho <strong>ya</strong> Luther <strong>ya</strong>kapata katika Uholandi watu wa juhudi na waaminifu kwa<br />
kuhubiri injili. Menno Simons, mtu wa elimu mkatoliki na aliyetakaswa kwa upadri, alikuwa<br />
mjinga kabisa wa Biblia na hakuisoma kwa ajili <strong>ya</strong> hofu <strong>ya</strong> upinzani wa ibada <strong>ya</strong> dini. Kwa<br />
ondoleo la zambi akajitahidi kun<strong>ya</strong>mazisha sauti <strong>ya</strong> zamiri, lakini bila manufaa. Baada <strong>ya</strong><br />
wakati akaongozwa kujifunza Agano Jip<strong>ya</strong>; hili pamoja na maandiko <strong>ya</strong> Luther ikamletea<br />
kukubali imani <strong>ya</strong> matengenezo. Kwa mda kitambo akashuhudia mtu aliyeuawa kwa sababu<br />
alibatizwa mara <strong>ya</strong> pili. Jambo hili likamwongoza kujifunza Biblia kwa ajili <strong>ya</strong> ubatizo wa<br />
watoto wadogo. Aliona kwamba toba na imani vinahitajiwa kuwa sababu <strong>ya</strong> ubatizo.<br />
Menno akatoka kwa kanisa la Roma na akajitoa wakfu kwa kufundisha maneno <strong>ya</strong> ukweli<br />
aliyokubali. Katika Ujeremani na Uholandi kundi la washupavu likatokea, kuharibu kanuni<br />
na adabu, na kuendelea kufan<strong>ya</strong> maasi. Menno kwa nguvu zake zote akapinga mafundisho <strong>ya</strong><br />
uongo na mashauri <strong>ya</strong> ushenzi <strong>ya</strong> washupavu. Kwa miaka makumi mbili na tano akapitia<br />
Uhollande na upande wa kaskazini <strong>ya</strong> Ujeremani, kutumia mvuto mkubwa sana, kufananisha<br />
katika maisha <strong>ya</strong>ke mwenyewe mafundisho aliyofundisha. Alikuwa mtu wa haki, mpole na<br />
mtulivu, mwaminifu na mwenye bidii. Hesabu kubwa <strong>ya</strong> watu wakageuka sababu <strong>ya</strong> kazi<br />
zake.<br />
Katika Ujeremani Charles V alikomesha Matengenezo, lakini watawala wakasimama<br />
kama boma juu <strong>ya</strong> utawala wa ukaidi wake. Katika Uhollande mamlaka <strong>ya</strong>ke ilikuwa kubwa<br />
sana. Amri za mateso zikafuatana kwa upesi. Kwa kusoma Biblia, kuisikia ao kuihubiri,<br />
kumwomba Mungu kwa siri, kukataa kusujudu mbele <strong>ya</strong> sanamu ao kuimba Zaburi ilikuwa<br />
azabu <strong>ya</strong> kifo. Maelfu waliangamia chini <strong>ya</strong> Charles na Philip II.<br />
93