17.02.2019 Views

TANZANI NA UCHUMI ENDELEVU

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

<strong>TANZANI</strong>A <strong>NA</strong> <strong>UCHUMI</strong> <strong>ENDELEVU</strong><br />

17/02/2019<br />

Tanzania ni moja ya mataifa yanayoendelea kimkakati na kimipango katika nyanja<br />

mbalimbali za kimaendeleo na utekelezaji ikiwa na azma ya kukuza uchumi na kupunguza<br />

umasikini kwa mwananchi mmoja mmoja na kwa jamii na taifa kiujumla. Kuanzia miaka ya<br />

mwanzoni mwa karne hii ya 21, jitihada za dhati zilipangwa na kuanza kufanyika kama vile<br />

kuimarisha ubora wa maisha na ustawi wa jamii kwa kuanzisha mpango wa maendeleo wa<br />

elimu ya sekondari (MMES), mpango wa maendeleo wa elimu ya msingi (MMEM),<br />

kuimarisha utawala bora na uwajibikaji hasa likihusika na mapambano dhidi ya rushwa.<br />

Katika harakati na jitihada hizo za kimaendeleo, yapo mabadiliko ya sera za kijumla na<br />

mipango ya kitaifa iliyojitokeza katika kipindi cha utekelezaji wa sera hizi. Kutokana na Dira<br />

ya Taifa ya Maendeleo 2025 na Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Muda mrefu 2011/12<br />

hadi 2024/25, Serikali ililenga kujenga jamii iliyoelimika na yenye kupenda kujielimisha.<br />

Pamoja na azma hiyo, Tanzania iliridhia Itifaki ya SADC (1997) kuhusu elimu na mafunzo<br />

iliyozitaka nchi wanachama kuwa na elimu msingi ya lazima kwa kipindi kisichopungua<br />

miaka tisa (9); Itifaki ya Dakar (2000) kuhusu Elimu kwa wote; Makubaliano ya Perth<br />

UNESCO (2007) kuhusu Elimu ya Sayansi na Teknolojia na mafunzo ya ufundi.<br />

Kwa mujibu wa itifaki ya makubaliano ya Dakar, mwaka 2000 (WEF 2000), yaliwekwa<br />

malengo kadhaa kwa wanachana wake na moja ya malengo hayo ni utoaji wa elimu bure na<br />

ya<br />

lazima kwa wote. Pia, kulingana na malengo ya millennia yaliyopangwa na nchi<br />

wanachama wa umoja wa mataifa mwaka 2000 kule Marekani; elimu ni moja ya vipaumbele<br />

vya malengo hayo. Na hapa ninaainisha malengo matatu tu likiwamo hili la elimu ambayo<br />

ndio msingi wa ujumbe wangu; kuondoa umaskini na njaa, kufikia Elimu ya msingi kwa<br />

1


wote, kuhakikisha mazingira endelevu kwa wananchi wake ili kuwajengea uwezo wa kufanya<br />

kazi za uzalishaji na kujiongezea kipato ili kukuza uchumi.<br />

Katika hili, nchi wanachama zilitakiwa kutoa taarifa kwa Umoja wa Mataifa, na Tanzania ni<br />

miongoni mwa nchi wanachama walioendelea kutoa taarifa na hiyo ilianza mwaka 2001 na<br />

kuendelea; taarifa ikieleza hatua zilizochukukuliwa au zinazochukuliwa kuhusiana na<br />

malengo husika na kiwango kilichofikiwa cha maendeleo kuhusiana na malengo hayo.<br />

Baada ya miaka 15, Taifa la Tanzania lilipitia nusu awamu na awamu moja ya utawala wa<br />

maraisi wawili na kufikia mafanikio makubwa kama vile kuimarika kwa mahusiano<br />

(kidiplomasia) na mataifa mengine hasa katika awamu ya nne. Hili lilienda sambamba na<br />

changamoto mbali mbali katika jitihada za kukuza na kuendelea kiuchumi kwa njia ya<br />

kumwezesha mwananchi kuinua kipato chake. Changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa<br />

nishati ya umeme ya uhakika hasa kwa maeneo ya vijijini na pia kuzidiwa nguvu katika<br />

mapambano dhidi ya ufisadi na usimamizi mbovu wa rasilimali za taifa.<br />

Wakati huo (2015) Tanzania iliingia katika mchakato wa uchaguzi mkuu wa Raisi, Wabunge<br />

na Madiwani uchaguzi ambao ulifuata baada ya chaguzi za serikali za mitaa na kufanikisha<br />

kuingia madarakani utawala mpya wa serikali ya awamu ya tano. Utawala ambao uliingia na<br />

kauli mbiu ya “Hapa kazi tu.” Hasa ikilenga kutekeleza ilani ya chama tawala huku Raisi,<br />

ndugu John Pombe Magufuli akiongoza jitihada za kutaka kurudisha heshima ya chama na<br />

kuweka sawa mwelekeo wa nchi katika kujijenga kiuchumi. Hiyo ilionekana kuzaa matunda<br />

mara baada ya muda mfupi kuonekana kuimarika nidhamu ya kazi kwa watumishi wa umma,<br />

kuimarika kwa utawala bora na uwajibikaji na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa katika<br />

mapambano dhidi ya rushwa na ufisaji.<br />

Mafanikio ya mapambano na kutokomeza rushwa katika taifa yamedhihirika na kushuhudiwa<br />

na mataifa makubwa baada ya ripoti iliyotolewa hivi karibuni katika kikao cha viongozi wa<br />

2


nchi wanachama wa mataifa ya Afrika kilichofanyika mwezi huu wa februari 2019 huko<br />

Addis Ababa, Ethiopia. huku Waziri mkuu, ndugu Kasim Majaliwa akimwakilisha Raisi.<br />

Katika taarifa hiyo, Tanzania ilitajwa kuwa miongoni mwa mataifa machache ambayo<br />

takwimu zinaonyesha kuwa imefanikiwa zaidi katika mapambano dhidi ya rushwa.<br />

Katika utekelezaji na uboreshaji wa huduma kwa wananchi, kulikuwa na moja ya ahadi ya<br />

chama (kulingana na ilani yake) kwa wananchi wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015<br />

ambayo ni kuleta elimu bila malipo ili huduma hii ya utoaji elimu iwafikie watanzania wote<br />

wa matabaka yote ya kiuchumi.<br />

Utekelezaji wa ilani ya chama mwaka 2015 kuhusu sera hii ya elimu bure ulianza mapema<br />

mwanzoni mwa mwaka 2016. Katika kufanikisha hilo, msisitizo na usimamizi makini<br />

ulionekana katika kuhakikisha watoto wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza<br />

wanaendelea na masomo hayo sambamba na uandikishaji wa watoto darasa la kwanza kwa<br />

wale waliokuwa wameshafikisha umri wa kuanza shule. Hatua hiyo iliyoambatana na uhaba<br />

wa vyumba vya madarasa na madawati ambao pia jitihada zimefanyika na zinaendelea ili<br />

kuhakikisha watoto wanahudhuria shule na kupata haki yao ya msingi ya elimu bila malipo.<br />

Kwa hatua hiyo, hapo kama taifa limefanikiwa kwa serikali kuonyesha jitihada hizo za<br />

utekelezaji wa ahadi hiyo na kumjali mwananchi hasa wa tabaka la chini ili kumjengea<br />

mazingira na vigezo vya kumtoa katika wimbi la ujinga na umasikini wa kipato na ikiwa na<br />

dhamiri njema ya kulitoa hapa taifa lilipo na kulipeleka katika uchumi wa kati na wa<br />

viwanda. Pia hii ni kwa mujibu wa makusudi ya serikali (dira ya taifa) ya kuleta mapinduzi<br />

ya kiuchumi ili kuibadili Tazania kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo 2025.<br />

Fursa ya elimu bila malipo (kwa usawa) imeendelea kutolewa kwa watoto wote kujiunga na<br />

shule na kupatiwa malezi kimwili, kiakili, kimaadili na kiroho kwa shule ya msingi na mpaka<br />

3


kidato cha nne tangu mwaka 2016 na sasa huu ni mwaka wa nne toka kuanza kutekelezwa<br />

kwa sera ya elimu bila malipo.<br />

Kwa upande mwingine, watahiniwa-watarajiwa hao walioanza kufaidi utekelezaji wa sera ya<br />

elimu bure sasa wameshafika kidato cha nne mwaka huu (2019). Mazinigira na takwimu<br />

(kwa baadhi ya maeneo) zinaonyesha kuwa kundi hili ni kubwa sana ikilinganishwa na miaka<br />

mingine iliyopita, huku ikionyesha idadi ndogo kabisa ya walioacha masomo (drop out)<br />

ambayo pia ni mafanikio katika kudhibiti watoto kukatisha masomo (katika awamu hii ya<br />

tano) kutokana na sababu mbali mbali kama vile mimba, ndoa, ajira za watoto n:k. Hivyo<br />

kuna uwezekano wa kuanza kuwa na ongezeko kubwa la ghafla la wahitimu wa kidato cha<br />

nne mwaka huu (2019) kuliko miaka iliyopita. Hayo pia ni mafanikio kwa sababu tumeanza<br />

kupatia ufumbuzi changamoto ya mfumo wa elimu na mafunzo ambao hapo nyuma ulikuwa<br />

ukitawaliwa na muundo wa kitaaluma wenye dhana ya kuchuja wahitimu na kupata<br />

wachache wenye uwezo mkubwa katika taaluma.<br />

Kwa mujibu wa matokeo ya mitihani mwaka 2017/2018 na 2018/2019 ni rahisi matokeo<br />

hayo kuakisi aina ya matokeo yajayo ya 2019/2020 na kutupa picha ya jinsi ambavyo<br />

tunapaswa kujiandaa kupokea idadi kubwa ya (wananchi watakaoingia mitaani) walioshinda<br />

au kushindwa kabisa. Na hapo ndipo panahitaji uvumilivu, umakini na usikivu wa hali ya juu<br />

katika kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya kijamii na kitaifa katika sekta nyeti kama hii ya<br />

elimu. Kwa sababu swala hili halitakiwi kuwekwa katika mkondo wa kisiasa wala ushawishi<br />

wa amri inayoelekezwa kwa watendaji na watumishi wa chini ili wafanikishe kuboresha<br />

matokeo hayo yajayo. Bali ni swala linalogusa gharama kwa pande zote mbili; serikali na<br />

nguvu kazi iliyopo. Endapo jukumu litaachiwa upande mmoja tu litafutie ufumbuzi,<br />

hakutakuwa na matokeo chanya. Na itakuwa ni jambo la kushangaza hapo mwakani endapo<br />

tutaanza kuunda tume ili kuchunguza chanzo na sababu baada ya matokeo hayo yajayo ya<br />

kidato cha nne 2019/2020.<br />

4


Kwa upande mwingine, watanzania tuna utamaduni wa kusubiri tukio litokee ndio<br />

tunachukua hatua kulitatua, ingawa mazingira na hali ilianza kuonekana hapo kabla. Kwa<br />

mfano idadi ya madarasa kwa kidato cha tano na sita na madawati inaweza kutokidhi hitaji<br />

kwa sababu ya wingi wa wanafunzi watakaochaguliwa kujiunga kidato cha tano. Sasa upo<br />

uwezekano kwamba tukaanza kuamshana na kukimbizana ili kuwashughulikia watoto hao<br />

(wenye sifa) wasikose masomo ya kidato cha tano kuanzia mwezi wa saba, 2020. Lakini hilo<br />

ni angalizo tu kutokana na mtazamo wangu ambao pia unaweza kukosolewa.<br />

Sasa, ninarudi tena kwenye hoja yangu, kulingana na aina ya wanafunzi wanaopokelewa<br />

(miaka hii) wa kidato cha kwanza kwa shule nyingi za kawaida za sekondari serikalini<br />

unaotokana na mfumo (ule unaojulikana) wa kujibu maswali ya mitihani ya darasa la saba<br />

kutoka shule ya msingi; Ni matarajio kwamba idadi ya wasiojiweza na wasio na sifa mitaani<br />

itaongezeka ghafla kwa mwaka ujao 2019/2020, maana hao tunawajua na pia tunao huko<br />

madarasani na tunawafundisha. Lakini je, hii ndio idadi kubwa ya watanzania<br />

tunaowasafirisha katika chombo hiki cha elimu ili wafikie hatua ya kuwa nguvu kazi ya taifa<br />

lililoelimika ili lipate maendeleo? … (hiyo ni changamoto pia).<br />

Ijapokuwa haya (yawezekana) ni matokeo ya swala la vipaumbele. Kuamua kutilia mkazo wa<br />

kujenga upande Fulani na kuacha upande mwingine au kufumbia macho changamoto zilizopo<br />

eneo fulani au kuzitatua polepole pasipo kujali madhara na matokeo yake.<br />

Lakini, tatizo kama hilo si la mtu fulani pekee, wala kiongozi fulani pekee, wala taasisi fulani<br />

ya elimu pekee. Ni ugonjwa wa kitaifa unaomhusa kila mtanzania wa kiwango cha chini, kati<br />

na juu kiuchumi. Lakini kwa kuwa sio katika kila changamoto ya taifa itahitaji wananchi<br />

wote wahusike moja kwa moja katika kutatua changamoto hizo ila tunao wawakilishi (wenye<br />

sifa) pia wenye mamlaka ya maamuzi (pasipo siasa) na utekelezaji wa moja kwa moja<br />

unahitajika. Ikumbukwe kuwa “Elimu ni uwekezaji mkubwa, na ili kupunguza tatizo lijalo<br />

5


(kuepusha aibu) ni muhimu kukumbuka kuwa uwekezaji mkubwa zaidi kifedha na rasilimali<br />

watu (nguvu kazi hasa sayansi) unahitajika, hapo.“<br />

Ni kushughulika na maeneo yote<br />

yanayogusa kitu kinachoitwa ‘fedha.‘<br />

Ni ukweli usiopingika kwamba taifa lina mzigo mkubwa wa majukumu yanayohitaji fedha<br />

hasa katika kutekeleza miradi mbalimbali na mikubwa inayoendelea na ijayo - hapo tunaunga<br />

mkono. Lakini ni swala la kipaumbele pia. Eneo la elimu ya msingi na sekondari sio la<br />

kugusa juu juu. Siku zote, misingi ikiharibika, tujue kwamba huko juu na huko mbeleni<br />

tunaenda kuvuna uharibifu. Uwezekano ni mkubwa wa kuwamwaga mitaani hao wahitimu<br />

wote (walioshindwa) na wakakosa mwelekeo kwa sababu hatujaandaa mazingira (kama taifa<br />

na sio wazazi na walezi pekee) ya kuwafanya wawe na faida kwa jamii, ni sawa na kuzalisha<br />

kwa makusudi kitu au kifaa hatari usichokijua na kukiacha au kukitupa na baadae bila kujua<br />

kinakuja kukudhuru mwenyewe.<br />

Endapo kutakuwa na ongezeko kubwa la walioshidwa kidato cha nne, pasipo kuwepo<br />

mikakati mahususi ya jinsi ya kuwaboresha katika ujuzi na maarifa yanayoendana na uhitaji<br />

wa kiuchumi wa dunia ya sasa, hapo tunaandaa taifa lenye watu wasiozalisha na waharibifu<br />

(vibaka, madawa ya kulevya, wezi, waporaji na majangiri). Taifa lenye watu wengi<br />

waliosoma na wenye ujuzi katika maeneo tofauti tofauti litaendelea haraka kuliko kuwa na<br />

wazurulaji wengi, ambao ni ‘wacheza pooltable asubuhi, walewa viroba siku nzima, wapiga<br />

debe wasio rasmi katika vituo vya mabasi masaa 24.’<br />

Kama mtanzania-mzalendo, ninadiriki kuandika hivi kwa sababu mimi sio mwanasiasa, niko<br />

upande wa utendaji zaidi na hapo haihitaji siasa endapo tunataka kuliweka taifa liendelee<br />

kuwa salama. Ni hatari sana endapo taifa halitachukua hatua zenye tija katika kuzuia<br />

ongezeko la watu wasiozalisha kitu katika jamii. Kwa sababu mtoto anatakiwa angalau kwa<br />

jitihada zote zilizowekwa (kwa miaka minne shuleni) basi apate alama ambazo itakuwa rahisi<br />

6


kumuwezesha aidha kuendelea na masomo, kuendelea na masomo ya ufundi stadi au kujenga<br />

mazingira ya mtoto huyo aondoke shulani akiwa na ujuzi katika eneo fulani ili akienda<br />

mitaani basi ikawe rahisi kuwezeshwa. Na hilo ndilo eneo lililo nje ya mkondo wa taaluma<br />

hasa kwa kuzingatia vipawa na karama walizonazo wanafunzi mashuleni. Ikumbukwe kuwa<br />

moja ya mahitaji ya taifa ili liendelee linahitaji kuwa na rasilimali watu (nguvu kazi<br />

iliyoelimika na yenye ujuzi wa kutosha).<br />

Na hapa ndipo tunaelewa msisitizo wa kufanya kazi unaotolewa mara kadhaa na Raisi, ndugu<br />

John pombe magufuli akisema “mimi nataka watu wafanye kazi.” Ikimaanisha kwamba<br />

tukifanya kazi kwa bidii, hatutasubiri wakati wote misaada toka nje ili tufanye au tupate<br />

maendeleo, hatutaomba chakula cha msaada toka nje, kama ni chakula basi tutazalisha kwa<br />

wingi na kubakiwa na ziada (excess) ambacho kitatoka nje (kwa utaratibu sahihi) ili tupate<br />

fedha za kigeni. Kwa mantiki hiyo, inatukumbusha kuwa rasilimali watu nyingine<br />

inaandaliwa shuleni. Shuleni ndio mazingira yanayotakiwa kupika, kupakuwa na<br />

kuwamwaga hao wataalamu katika maeneo husika. Lakini kama hawakuiva, basi wanatupwa<br />

jalalani (mitaani), nao wanaanza kutafuta mazingira ya kula bila kufanya kazi. Tayari huo ni<br />

mzigo tuliozalisha wenyewe.<br />

Kwa mujibu wa sera ya Elimu na mafunzo (2014) inabaini jitihada na malengo ya sekta ya<br />

elimu (ambayo mimi ninaita “JIKONI” kwa sababu ndio sekta mama katika kuzalisha, kulea<br />

na kukuza rasilimali watu na kada zote zinatoka hapo). Hivyo sekta ya elimu na mafunzo,<br />

kwa mujibu wa dira ya maendeleo ya taifa 2011/2012 hadi 2024/25, ilitarajiwa na inaendelea<br />

kutarajiwa kuleta maendeleo ya haraka ya rasilimali watu kwa kutayarisha idadi ya kutosha<br />

ya watanzania walioelimika na kupenda kujielimisha zaidi ili kulifanya taifa lipate maendeleo<br />

na kuwa lenye uchumi wa kati na baadae iwezekane kuwa na uchumi wa juu.<br />

7


Ninanukuu maelezo ya sera ya elimu, yanasema; ‘kumekuwa na changamoto katika kuinua<br />

ubora wa elimu na mafunzo kutokana na mitaala katika ngazi mbalimbali za elimu na<br />

mafunzo kutokidhi mahitaji ya mabadiliko ya kiuchumi, kijamii, kisayansi na teknolojia na<br />

hivyo kutoa wahitimu ambao hawana umahiri wa kutosha kuhimili ushindani katika<br />

ulimwengu wa kazi.’<br />

Moja ya mabadiliko katika upepo wa kimaendeleo katika jamii ni msisitizo katika sera ya<br />

viwanda, ambao umetoa fursa kwa wananchi na wawekezaji (ndani na nje) kupatiwa maeneo<br />

(ardhi) kwa masharti nafuu ili kuanzisha na kuendeleza viwanda. Sasa hali hii inaonyesha<br />

umuhimu wa kuweka mabadiliko na mkazo (mitaala) katika utoaji wa elimu inayokidhi<br />

mahitaji hayo ya sasa ili kuandaa taifa lenye mtazamo wa kiviwanda toka wakiwa shule ya<br />

msingi na sekondari.<br />

Na badiliko lingine katika jamii ni ongezeko kubwa la watu na uhaba wa ajira (ajira rasmi).<br />

Kwa mfano walimu wa masomo ya sanaa mpaka sasa hawajaingia katika ajira ya serikali<br />

toka mwaka 2015. Lakini vyuo vinaendelea kuzalisha idadi kubwa ya walimu hao wa sanaa<br />

ambao wanaendelea kuingia mitaani na vyeti na taaluma zao wakitegemea ajira mpya<br />

serikalini na sekta binafsi. Na wakati ajira hiyo imesimama, bado kumekuwa na ongezeko la<br />

idadi ya wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza na pia shule ya msingi.<br />

Hapo pia naweka angalizo. Uandaliwe mfumo wa kuwafanyia usahili walimu wanaohitaji<br />

kuingia ajira ya serikali. Kwa sababu haiwezekani na haiingii akilini kuwa tuna idadi kubwa<br />

sana ya walimu wahitimu wa vyuo vikuu na diploma mitaani lakini bado hakuna utaratibu<br />

wenye manufaa wa kuwachuja ili kuwapata walimu bora na kuwapa ajira. Unajua, hatuhitaji<br />

kuwa na bora walimu, ila walimu bora. Sasa hivi vyuo ni vingi na wengine wameenda<br />

kusomea ualimu na kuingizwa kwenye ajira ya ualimu ili kutafuta riziki tu (watu wa<br />

mshahara) lakini mwito na uwezo wa kumsaidia mtoto hasa kitaaluma hana.<br />

8


Ushauri wangu kwa Serikali ni kuwa kila halmashauri iwe na kitengo hicho (ikiwezekana<br />

watu wa HR na TSC); usahili ufanyike angalau mara mbili kwa mwaka kwa kila<br />

halmashauri) na kuandaliwa database ya walimu wenye sifa (wanaohitaji ajira) baada ya<br />

kufanyiwa usahili na kupeleka majina na taarifa zao TAMISEMI (hiyo inawezekana kama<br />

kweli tunataka kuingia gharama ambayo inamanufaa kwa hatima njema ya elimu yetu. Hili<br />

pia ni katika kuandaa mazingira yenye tija katika kuandaa taifa lijalo la uchumi wa viwanda.<br />

Maana msingi mkuu ni kuimarisha utoaji wa elimu bora.<br />

Na kama utatumia kigezo cha GPA tu ili kubaini mwalimu bora basi hapo ndio utapotea<br />

kabisa. Ualimu sio GPA peke yake. Humu mitaani kuna waalimu ni darasa la saba wa<br />

zamani, lakini wanauwezo wa kumsaidia mtoto wa darasa la kwanza kwa usahihi kuliko huyu<br />

mwalimu mwenye degree ya kwanza ya ualimu (ijapokuwa tunawatambua hao wa mitaani<br />

kuwa wanawaharibia msingi watoto kwa mfano kwenye kanuni kama za kufundisha<br />

kingereza na hesabu). Lakini ni bora kumchukua huyu wa mitaani na kumpeleka chuo ili<br />

akajue kanuni za ufundishaji na kumjengea uwezo na kumfanya awe mwalimu rasmi. (huo ni<br />

mfano tu).<br />

Kwa swala la kuwafanyia walimu usahili, changamoto inakuja katika kudhibiti rushwa na<br />

undugu. Hapo pia inatakiwa kuwekwa mazingira magumu ya kuchukuana kindugu au kwa<br />

rushwa. Lakini kama zitawekwa sheria kali, inawezekana kulitekeleza hilo (na kupunguza<br />

sana kubebana katika ajira) kwa sababu hitaji letu ni kuona kuwa ualimu sio ‘dampo’ la<br />

kupokea kila mtu aliyekosa kwa kwenda. Ualimu ni taaluma na lazima iheshimiwe, na<br />

serikali iwe na uhakika kuwa imeajiri nguvu kazi yenye kutaka kuleta mabadiliko. Hata<br />

ikiwapa motisha, iwe na uhakika kuwa hiyo motisha imeelekezwa katika mkondo wa watu<br />

sahihi wanaostahili.<br />

9


Zipo sababu nyingi za shule binafsi kufanya vizuri kuliko za serikali kwa sasa, lakini sababu<br />

moja wapo ni kuwafanyia walimu usahili ili kubaini uwezo wao kabla ya kuwapa mkataba au<br />

ajira. Kuna usahili wa kuhojiwa kwa mdomo, wa kuandika na pia usahili wa kuingia<br />

darasani. Yote hayo yafanyike. Hujui kwamba kwa sasa unaweza kuajiri walimu ambao<br />

hawajui kuandika barua ya kuomba kazi. (lakini ile aliyopeleka kuomba kazi aliandikiwa na<br />

mtu mwingine).<br />

Ikumbukwe kuwa elimu ndio nyenzo pekee ya kubadili mawazo, fikra na mitazamo ya watu<br />

ili kuzalisha na kuharakisha matokeo chanya katika jamii na mazingira yanayomzunguka<br />

mwanamchi huyu. Na njia pekee ni kupatiwa elimu kwa njia rasmi na isiyo rasmi<br />

ili<br />

kupata/kupanua maarifa na ufahamu kutoka kwa wataalamu na wanataaluma<br />

Sera yetu ya elimu inayotekelezwa sasa inabaini pia kuwa kuna idadi kubwa ya wataalamu<br />

walioelimika kwa kiwango cha juu wanaohitajika ili Tanzania kufikia kiwango cha nchi<br />

yenye uchumi wa kati huku taarifa zinaonyesha kwamba rasilimali watu ya Tanzania, kwa<br />

kiasi kikubwa ni wafanyakazi wenye ujuzi wa chini ambao ni asilimia 84, wakifuatiwa na<br />

wenye ujuzi wa kati asilimia 13 na wenye ujuzi wa juu asilimia 3. Hata hivyo, kwa nchi za<br />

kipato cha kati ngazi ya chini, ulinganifu unaonyesha kuwa nchi hizo zina wastani wa<br />

asilimia 55 ya wafanyakazi wenye ujuzi wa chini, asilimia 33 ujuzi wa kati na asilimia 12<br />

ujuzi wa juu. Hivyo, Tanzania ina changamoto ya kuinua mchanganyiko wa wafanyakazi<br />

wenye ujuzi katika fani mbalimbali ili kufikia mahitaji ya rasilimaliwatu kwa nchi ya kipato<br />

cha kati kufikia mwaka 2025.<br />

Sasa, ili kuweza kuyafikia malengo haya pasipo shida, ni muhimu kushughulika hasa kwa<br />

kuanzia elimu ya msingi na sekondari (hapo ni swala la mitaala). Ijapokuwa watoto wa shule<br />

ya msingi na sekondari, hawapatiwi (kulingana na mitaala) elimu ya kujitegemea inayoweza<br />

kuwaandaa kwa ajili ya kuyakabili mazingira ya kazi yajayo hasa ikizingatiwa kuwa umri<br />

10


wao pia ni mdogo lakini bado tunajukumu kubwa lisilokwepeka la kuanzia msingi na<br />

sekondari kutoa elimu inayoweza kubadili mtazamo na fikra kuwa maisha ya shule<br />

yanatuandaa kwa ajili ya kufanya kazi za uzalishaji mali kwa njia ya kujitegemea (ajira<br />

binafsi). Mwanafunzi ajue kuwa anasoma hata kufikia (kidato cha nne au sita) ili aje<br />

kufanikiwa kuwa fundi cherehani (kushona nguo) na kuwa na kiwanda kidogo cha kuajiri<br />

wengine.<br />

Kazi hata ya kushona viatu na ndala na kubrashi maeneo ya mjini/mitaani inafanywa na idadi<br />

kubwa ya watu ambao hawakupata fursa ya kwenda shule au waliishia darasa la saba la<br />

zamani kidogo. Inaonekana si kazi yenye kufaa kwa wasomi kwa sababu ni matokeo ya<br />

elimu ya nadharia toka shuleni msingi.<br />

Kama ilivyokuwa hapo nyuma, swala la kilimo (mkulima-kushinda kwenye matope),<br />

haikuwa rahisi kufanywa na msomi wa chuo kikuu. Bali na wale waliokosa fursa ya elimu.<br />

Na hata yule mtaalamu wa kilimo (wengine maafisa kilimo) wakijifungia ofisini ili kusubiri<br />

wateja wawafuate, na kusubiri vikao ofisini na si kwenda kushida kwenye mapori, nyasi na<br />

matope ili wakatoa elimu kwa wakulima namna ya kufanya kilimo chenye tija. Hiyo yote ni<br />

mitazamo na fikra ambazo mtanzania ametoka nazo shule ya msingi.<br />

Lakini ukweli ni kwamba kazi ndogo ndogo kama hiyo ikifanywa na msomi inaweza<br />

kufanywa kwa umaridadi wa kiwango cha juu na kuleta mapinduzi katika sekta ndogo ndogo.<br />

Ni kama vile kumchukua profea wa chuo kikuu aende kufundisha shule ya msingi kwa<br />

watoto wanaotoa kamasi. Inakuwa ngumu kidogo (hata kama ataboreshewa mazingira ya<br />

kazi) na kupatiwa mshahara na marupurupu yale yale anayoyapata kule chuoni. Inatakiwa<br />

awe mzalendo. Ingawa tutasema kuwa kutokana na uhaba wa maprofesa chuo kikuu basi<br />

11


awaachie hao walimu wa cheti, diploma na degree wafanye kazi ya kufundisha shule ya<br />

msigni ambayo ni ya kwango chao. Kwa sababu itakuwa ni matumizi yasiyo sahihi ya<br />

rasilimali watu.<br />

Lakini pia mhandisi, akipewa ekari tano (kwa mfano) ili aziendeleze katika kuzalisha zao<br />

fulani, uwezekano wa kumudu hiyo kazi na kuleta matokeo chanya ni mkubwa kwa sababu<br />

tunategemea kuwa ana uwezo mkubwa wa kuelewa na kufuata maelekezo ya wataalamu wa<br />

kilimo. Zaidi ya hayo anafursa ya kujisomea na kujua kanuni nyingi zaidi za kilimo na<br />

kubadilika kulingana na mazingira na mahitaji katika kazi yake ya ukulima. Akienda kwenye<br />

duka la pembejeo kunakuwa na uwezekano mdogo wa kuzulumiwa au kuuziwa viwatilifu<br />

vilivyokwisha muda kwa sababu anauwezo wa kisomi (wa kubaini mambo) na kufanya tafiti<br />

kwa wahusika kama TFDA na kujua ukweli wa bidhaa. Msomi ana ujasiri wa kufuatilia na<br />

kuhoji ili kujua ukweli.<br />

Sasa, elimu ya uchumi wa viwanda inatakiwa kuingizwa katika mfumo rasmi mashuleni ili<br />

tufanikiwe katika harakati hizo na kubadili mtazamo na fikra kuanzia shule ya msingi na<br />

sekondari-hapo siongelei elimu ya nadharia bali kujitegema. Uhamasishaji usiishie mitaani na<br />

kwenye vyombo vya habari tu … hivyo kwa wakati huu, wengi wasiosoma ndio wanaelimu<br />

ya kutosha na kwa kuwa walikuwa na msingi ambao haukuwezeshwa na sera ya taifa ya<br />

viwanda hapo nyuma. Hii inamaanisha kuwa wakati ujao huyo mwenye vyerehani vitano vya<br />

kushonea nguo ndio atakuja kuajiri hao waliokwenda shule na kuhitimu lakini wakakosa sifa,<br />

kwa sababu hao walioshuleni sasa wanafikra kuwa watasoma ili waje kuajiriwa.<br />

Wazo langu pia ni kufikiri namna ambavyo tunaweza kuunganisha elimu ya sekondari na<br />

vyuo kama VETA au vyuo vilivyosajiliwa na VETA. Mazingira hayo yatumike kama sehemu<br />

12


ya kufanya mazoezi kwa kazi ndogo za ujuzi hasa kwa watoto wa sekondari (natambua ni<br />

gumu kutekelezeka.) lakini itambulike kuwa watoto wanauwezo mkubwa wa kushughulika na<br />

vitendo kuliko nadharia endapo tu wataandaliwa mazingira na kujengewa uwezo. Hata kama<br />

mtoto anashida kidogo ya akili lakini ukimpeleka kwenye maeneo ya kushika SPANNER,<br />

uzoefu unaonyesha kuwa anaweza kuendana na mazingira hayo ya ufundi na polepole kupata<br />

ujuzi na baadae kuimudu hiyo na kuifurahia kuliko kushinda kumlazimisha aelewe (kukariri)<br />

sheria za Newton wakati ubonngo wake umegoma.<br />

Hilo nina uhakika nalo (endapo utekelezaji wake ungekuwa rahisi). Hebu jaribu kumchukua<br />

dereva aliyelewa (mlevi) mpaka kufikia kiwango cha kushikwa mikono kwa sababu hawezi<br />

kutembea mwenyewe. Sasa mchukue (kumbeba) na kumuweka kwenye kiti cha gari yake ili<br />

awashe injini na kuendesha. Atafanikiwa kufuata kanuni zote mpaka kuanza kuendesha gari<br />

ingawa usalama utakuwa mdogo akiishaingia barabarani.<br />

Lakini huyo huyo dereva jaribu kumpa maswali yanayohusu taaluma yake ya udereva na<br />

ayajibu kwa kuandika, uhakika ni kuwa atashindwa kuyajibu. Kwa sababu hapo ameingia<br />

kwenye nadharia na sio vitendo.<br />

Hivyo katika kuandaa wanafunzi katika mabadiliko ya kiuchumi na kijamii, kuna jukumu la<br />

kuendelea kupeleka na kufikisha elimu ya kutosha kwa (jamii) wazazi. Mzazi/mlezi<br />

anapaswa kuandaa mazingira ya kujua mtoto wake anapendelea kufanya nini (kazi gani)<br />

katika maisha. Kwa sababu maono ya maisha yajayo pia hayaanzii ukubwani tu, pia utotoni<br />

(kulingana na mazingira) Na hiyo itasaidia kubaini mwelekeo wa mtoto na pia kuanza<br />

kutengeneza mazingira ya kumwendeleza huyo mtoto. Ijapokuwa sio watoto wote watakuwa<br />

na wazo hilo lakini ni sehemu ya jukumu la wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kuanza<br />

13


mapema kutengeneza au kuandaa kipawa kwa mtoto wake. Na shuleni ndio mahali pa<br />

kuviendeleza (mfumo rasmi) pia endapo mazingira yataruhusu (kimtaala na uwekezaji).<br />

Mataifa yaliyoendelea yametushinda hapo, kumuandaa mtoto akiwa bado mdogo katika<br />

kumtengenezea njia aje kuwa mtaalamu au fundi mwenye ujuzi utokanao na kipawa katika<br />

eneo Fulani. Na hii ndio siri kubwa ya mafanikio yao katika sekta ya michezo. Kwa mfano<br />

kumtengenezea bwawa la kuogelea na kumfundisha mtoto wa umri wa miaka 4 ili ajue<br />

kuogelea. Au kumuandaa mtoto huyo awe mchezaji mpira wa miguu. Mtoto huyo akitimiza<br />

umri wa miaka kumi (10) atakuwa tayari ni mchezaji mwenye kipaji ambacho kilianzia<br />

utotoni pale nyumbani kwa wazazi au walezi. Wakati huku kwetu (mataifa mengi ya afrika),<br />

mtoto wa miaka kumi ndio anaanza kuonekana kwa mbali akiwa shuleni kuwa anawezo wa<br />

kuja kuwa mchezaji mpira mzuri. Na hapo wazazi hawajui na hawana taarifa yoyote juu ya<br />

kipaji cha mtoto wao.<br />

Sasa hapo ndio tunategemea kwamba taifa kama letu Tanzania tunaweza kushindana na timu<br />

ya taifa ya wakubwa ya brazil au ujerumani. Wachezaji wetu hawa walioanza kutambulika<br />

kuwa na kipaji cha kucheza mpira walipoanza kusoma shule, tena sekondari. Inakuwa ngumu<br />

kidogo.<br />

Ikumbukwe kwamba mzazi au mlezi anaouwezo wa kuamua kumuandalia mtoto wake awe<br />

mwana sheria, mkandarasi, dereva, mcheza mpira, mwanariadha akiwa bado shule ya msingi.<br />

Na hapo ndio chimbuko la kupata taifa lisilo teteleka katika nguvu kazi kwenye maeneo ya<br />

uzalishaji. Hii ndio maana kama mzazi ni mwana siasa basi asilimia kubwa atakuwepo motto<br />

wake mwanasiasa. Kama mzazi ni mjasiriamali basi atakuwepo mtoto wa kufuata nyayo hizo<br />

14


za ujasiriamali. Kama mzazi ni mkulima basi hivyo hivyo atakuwepo mtoto mkulima katika<br />

wale.<br />

Changamoto kwa watanzanai na waafrika kiujumla ni kuwa hatuna utamaduni huo wa<br />

kumuandaa mtoto katika mazingira ya kutambua (kuibua) vipawa alivyonavyo akiwa angali<br />

katika umri mdogo. Pia hatuna utamaduni wa kujisomea mambo ya msingi (vitabu/hadithi ili<br />

kupanua mawazo), ufukara wa kijamii, kukosa elimu na pia mazingira duni ambayo hayafai<br />

kuandaa watoto wakiwa bado na umri mdogo pale nyumabni (katika jamii). Hayo yote ni<br />

changamoto katika safari ya kuandaa taifa la uchumi wa kati.<br />

Kwa mpango wa miaka mingi ijayo kwa mfano (kuanzia muongo mmoja hivi), mafanikio<br />

katika kumuandalia mwanafunzi mazingira rafiki pale nyumbani (jamii) na shuleni (mitaala)<br />

yatasaidia kuibua vipawa na kuviendeleza na hilo litarahisisha kupunguza idadi ya watoto<br />

wanaokuja kuhitimu kidato cha nne wakiwa hawana mwelekeo wa kufanya kitu (kuzalisha<br />

mali) hasa baada ya eneo la taaluma kushindikana.<br />

Hapo sijagusia swala la kipingamizi cha sheria ya ajira kwa watoto chini ya umri wa miaka<br />

kumi na nne (14), na wale wenye umri kati ya kumi na nne mpaka kumi na saba (14-17),<br />

ambapo kundi hili (14-17), ndilo linabeba wahitimu wengi wa kidacho cha nne kwa sasa.<br />

Ingawa (kwa mtazamo wangu) sheria ya kumbada mtoto wa umri huo (14-17), kufanya kazi<br />

nyepesi unatoa fursa moja kwa moja kuingia katika ulimwengu wa kazi endapo ana ujuzi.<br />

MUNGU LIBARIKI TAIFA LETU LA <strong>TANZANI</strong>A<br />

0719194900 ////// 0738753217<br />

15

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!