You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>TANZANI</strong>A <strong>NA</strong> <strong>UCHUMI</strong> <strong>ENDELEVU</strong><br />
17/02/2019<br />
Tanzania ni moja ya mataifa yanayoendelea kimkakati na kimipango katika nyanja<br />
mbalimbali za kimaendeleo na utekelezaji ikiwa na azma ya kukuza uchumi na kupunguza<br />
umasikini kwa mwananchi mmoja mmoja na kwa jamii na taifa kiujumla. Kuanzia miaka ya<br />
mwanzoni mwa karne hii ya 21, jitihada za dhati zilipangwa na kuanza kufanyika kama vile<br />
kuimarisha ubora wa maisha na ustawi wa jamii kwa kuanzisha mpango wa maendeleo wa<br />
elimu ya sekondari (MMES), mpango wa maendeleo wa elimu ya msingi (MMEM),<br />
kuimarisha utawala bora na uwajibikaji hasa likihusika na mapambano dhidi ya rushwa.<br />
Katika harakati na jitihada hizo za kimaendeleo, yapo mabadiliko ya sera za kijumla na<br />
mipango ya kitaifa iliyojitokeza katika kipindi cha utekelezaji wa sera hizi. Kutokana na Dira<br />
ya Taifa ya Maendeleo 2025 na Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Muda mrefu 2011/12<br />
hadi 2024/25, Serikali ililenga kujenga jamii iliyoelimika na yenye kupenda kujielimisha.<br />
Pamoja na azma hiyo, Tanzania iliridhia Itifaki ya SADC (1997) kuhusu elimu na mafunzo<br />
iliyozitaka nchi wanachama kuwa na elimu msingi ya lazima kwa kipindi kisichopungua<br />
miaka tisa (9); Itifaki ya Dakar (2000) kuhusu Elimu kwa wote; Makubaliano ya Perth<br />
UNESCO (2007) kuhusu Elimu ya Sayansi na Teknolojia na mafunzo ya ufundi.<br />
Kwa mujibu wa itifaki ya makubaliano ya Dakar, mwaka 2000 (WEF 2000), yaliwekwa<br />
malengo kadhaa kwa wanachana wake na moja ya malengo hayo ni utoaji wa elimu bure na<br />
ya<br />
lazima kwa wote. Pia, kulingana na malengo ya millennia yaliyopangwa na nchi<br />
wanachama wa umoja wa mataifa mwaka 2000 kule Marekani; elimu ni moja ya vipaumbele<br />
vya malengo hayo. Na hapa ninaainisha malengo matatu tu likiwamo hili la elimu ambayo<br />
ndio msingi wa ujumbe wangu; kuondoa umaskini na njaa, kufikia Elimu ya msingi kwa<br />
1
wote, kuhakikisha mazingira endelevu kwa wananchi wake ili kuwajengea uwezo wa kufanya<br />
kazi za uzalishaji na kujiongezea kipato ili kukuza uchumi.<br />
Katika hili, nchi wanachama zilitakiwa kutoa taarifa kwa Umoja wa Mataifa, na Tanzania ni<br />
miongoni mwa nchi wanachama walioendelea kutoa taarifa na hiyo ilianza mwaka 2001 na<br />
kuendelea; taarifa ikieleza hatua zilizochukukuliwa au zinazochukuliwa kuhusiana na<br />
malengo husika na kiwango kilichofikiwa cha maendeleo kuhusiana na malengo hayo.<br />
Baada ya miaka 15, Taifa la Tanzania lilipitia nusu awamu na awamu moja ya utawala wa<br />
maraisi wawili na kufikia mafanikio makubwa kama vile kuimarika kwa mahusiano<br />
(kidiplomasia) na mataifa mengine hasa katika awamu ya nne. Hili lilienda sambamba na<br />
changamoto mbali mbali katika jitihada za kukuza na kuendelea kiuchumi kwa njia ya<br />
kumwezesha mwananchi kuinua kipato chake. Changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa<br />
nishati ya umeme ya uhakika hasa kwa maeneo ya vijijini na pia kuzidiwa nguvu katika<br />
mapambano dhidi ya ufisadi na usimamizi mbovu wa rasilimali za taifa.<br />
Wakati huo (2015) Tanzania iliingia katika mchakato wa uchaguzi mkuu wa Raisi, Wabunge<br />
na Madiwani uchaguzi ambao ulifuata baada ya chaguzi za serikali za mitaa na kufanikisha<br />
kuingia madarakani utawala mpya wa serikali ya awamu ya tano. Utawala ambao uliingia na<br />
kauli mbiu ya “Hapa kazi tu.” Hasa ikilenga kutekeleza ilani ya chama tawala huku Raisi,<br />
ndugu John Pombe Magufuli akiongoza jitihada za kutaka kurudisha heshima ya chama na<br />
kuweka sawa mwelekeo wa nchi katika kujijenga kiuchumi. Hiyo ilionekana kuzaa matunda<br />
mara baada ya muda mfupi kuonekana kuimarika nidhamu ya kazi kwa watumishi wa umma,<br />
kuimarika kwa utawala bora na uwajibikaji na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa katika<br />
mapambano dhidi ya rushwa na ufisaji.<br />
Mafanikio ya mapambano na kutokomeza rushwa katika taifa yamedhihirika na kushuhudiwa<br />
na mataifa makubwa baada ya ripoti iliyotolewa hivi karibuni katika kikao cha viongozi wa<br />
2
nchi wanachama wa mataifa ya Afrika kilichofanyika mwezi huu wa februari 2019 huko<br />
Addis Ababa, Ethiopia. huku Waziri mkuu, ndugu Kasim Majaliwa akimwakilisha Raisi.<br />
Katika taarifa hiyo, Tanzania ilitajwa kuwa miongoni mwa mataifa machache ambayo<br />
takwimu zinaonyesha kuwa imefanikiwa zaidi katika mapambano dhidi ya rushwa.<br />
Katika utekelezaji na uboreshaji wa huduma kwa wananchi, kulikuwa na moja ya ahadi ya<br />
chama (kulingana na ilani yake) kwa wananchi wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015<br />
ambayo ni kuleta elimu bila malipo ili huduma hii ya utoaji elimu iwafikie watanzania wote<br />
wa matabaka yote ya kiuchumi.<br />
Utekelezaji wa ilani ya chama mwaka 2015 kuhusu sera hii ya elimu bure ulianza mapema<br />
mwanzoni mwa mwaka 2016. Katika kufanikisha hilo, msisitizo na usimamizi makini<br />
ulionekana katika kuhakikisha watoto wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza<br />
wanaendelea na masomo hayo sambamba na uandikishaji wa watoto darasa la kwanza kwa<br />
wale waliokuwa wameshafikisha umri wa kuanza shule. Hatua hiyo iliyoambatana na uhaba<br />
wa vyumba vya madarasa na madawati ambao pia jitihada zimefanyika na zinaendelea ili<br />
kuhakikisha watoto wanahudhuria shule na kupata haki yao ya msingi ya elimu bila malipo.<br />
Kwa hatua hiyo, hapo kama taifa limefanikiwa kwa serikali kuonyesha jitihada hizo za<br />
utekelezaji wa ahadi hiyo na kumjali mwananchi hasa wa tabaka la chini ili kumjengea<br />
mazingira na vigezo vya kumtoa katika wimbi la ujinga na umasikini wa kipato na ikiwa na<br />
dhamiri njema ya kulitoa hapa taifa lilipo na kulipeleka katika uchumi wa kati na wa<br />
viwanda. Pia hii ni kwa mujibu wa makusudi ya serikali (dira ya taifa) ya kuleta mapinduzi<br />
ya kiuchumi ili kuibadili Tazania kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo 2025.<br />
Fursa ya elimu bila malipo (kwa usawa) imeendelea kutolewa kwa watoto wote kujiunga na<br />
shule na kupatiwa malezi kimwili, kiakili, kimaadili na kiroho kwa shule ya msingi na mpaka<br />
3
kidato cha nne tangu mwaka 2016 na sasa huu ni mwaka wa nne toka kuanza kutekelezwa<br />
kwa sera ya elimu bila malipo.<br />
Kwa upande mwingine, watahiniwa-watarajiwa hao walioanza kufaidi utekelezaji wa sera ya<br />
elimu bure sasa wameshafika kidato cha nne mwaka huu (2019). Mazinigira na takwimu<br />
(kwa baadhi ya maeneo) zinaonyesha kuwa kundi hili ni kubwa sana ikilinganishwa na miaka<br />
mingine iliyopita, huku ikionyesha idadi ndogo kabisa ya walioacha masomo (drop out)<br />
ambayo pia ni mafanikio katika kudhibiti watoto kukatisha masomo (katika awamu hii ya<br />
tano) kutokana na sababu mbali mbali kama vile mimba, ndoa, ajira za watoto n:k. Hivyo<br />
kuna uwezekano wa kuanza kuwa na ongezeko kubwa la ghafla la wahitimu wa kidato cha<br />
nne mwaka huu (2019) kuliko miaka iliyopita. Hayo pia ni mafanikio kwa sababu tumeanza<br />
kupatia ufumbuzi changamoto ya mfumo wa elimu na mafunzo ambao hapo nyuma ulikuwa<br />
ukitawaliwa na muundo wa kitaaluma wenye dhana ya kuchuja wahitimu na kupata<br />
wachache wenye uwezo mkubwa katika taaluma.<br />
Kwa mujibu wa matokeo ya mitihani mwaka 2017/2018 na 2018/2019 ni rahisi matokeo<br />
hayo kuakisi aina ya matokeo yajayo ya 2019/2020 na kutupa picha ya jinsi ambavyo<br />
tunapaswa kujiandaa kupokea idadi kubwa ya (wananchi watakaoingia mitaani) walioshinda<br />
au kushindwa kabisa. Na hapo ndipo panahitaji uvumilivu, umakini na usikivu wa hali ya juu<br />
katika kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya kijamii na kitaifa katika sekta nyeti kama hii ya<br />
elimu. Kwa sababu swala hili halitakiwi kuwekwa katika mkondo wa kisiasa wala ushawishi<br />
wa amri inayoelekezwa kwa watendaji na watumishi wa chini ili wafanikishe kuboresha<br />
matokeo hayo yajayo. Bali ni swala linalogusa gharama kwa pande zote mbili; serikali na<br />
nguvu kazi iliyopo. Endapo jukumu litaachiwa upande mmoja tu litafutie ufumbuzi,<br />
hakutakuwa na matokeo chanya. Na itakuwa ni jambo la kushangaza hapo mwakani endapo<br />
tutaanza kuunda tume ili kuchunguza chanzo na sababu baada ya matokeo hayo yajayo ya<br />
kidato cha nne 2019/2020.<br />
4
Kwa upande mwingine, watanzania tuna utamaduni wa kusubiri tukio litokee ndio<br />
tunachukua hatua kulitatua, ingawa mazingira na hali ilianza kuonekana hapo kabla. Kwa<br />
mfano idadi ya madarasa kwa kidato cha tano na sita na madawati inaweza kutokidhi hitaji<br />
kwa sababu ya wingi wa wanafunzi watakaochaguliwa kujiunga kidato cha tano. Sasa upo<br />
uwezekano kwamba tukaanza kuamshana na kukimbizana ili kuwashughulikia watoto hao<br />
(wenye sifa) wasikose masomo ya kidato cha tano kuanzia mwezi wa saba, 2020. Lakini hilo<br />
ni angalizo tu kutokana na mtazamo wangu ambao pia unaweza kukosolewa.<br />
Sasa, ninarudi tena kwenye hoja yangu, kulingana na aina ya wanafunzi wanaopokelewa<br />
(miaka hii) wa kidato cha kwanza kwa shule nyingi za kawaida za sekondari serikalini<br />
unaotokana na mfumo (ule unaojulikana) wa kujibu maswali ya mitihani ya darasa la saba<br />
kutoka shule ya msingi; Ni matarajio kwamba idadi ya wasiojiweza na wasio na sifa mitaani<br />
itaongezeka ghafla kwa mwaka ujao 2019/2020, maana hao tunawajua na pia tunao huko<br />
madarasani na tunawafundisha. Lakini je, hii ndio idadi kubwa ya watanzania<br />
tunaowasafirisha katika chombo hiki cha elimu ili wafikie hatua ya kuwa nguvu kazi ya taifa<br />
lililoelimika ili lipate maendeleo? … (hiyo ni changamoto pia).<br />
Ijapokuwa haya (yawezekana) ni matokeo ya swala la vipaumbele. Kuamua kutilia mkazo wa<br />
kujenga upande Fulani na kuacha upande mwingine au kufumbia macho changamoto zilizopo<br />
eneo fulani au kuzitatua polepole pasipo kujali madhara na matokeo yake.<br />
Lakini, tatizo kama hilo si la mtu fulani pekee, wala kiongozi fulani pekee, wala taasisi fulani<br />
ya elimu pekee. Ni ugonjwa wa kitaifa unaomhusa kila mtanzania wa kiwango cha chini, kati<br />
na juu kiuchumi. Lakini kwa kuwa sio katika kila changamoto ya taifa itahitaji wananchi<br />
wote wahusike moja kwa moja katika kutatua changamoto hizo ila tunao wawakilishi (wenye<br />
sifa) pia wenye mamlaka ya maamuzi (pasipo siasa) na utekelezaji wa moja kwa moja<br />
unahitajika. Ikumbukwe kuwa “Elimu ni uwekezaji mkubwa, na ili kupunguza tatizo lijalo<br />
5
(kuepusha aibu) ni muhimu kukumbuka kuwa uwekezaji mkubwa zaidi kifedha na rasilimali<br />
watu (nguvu kazi hasa sayansi) unahitajika, hapo.“<br />
Ni kushughulika na maeneo yote<br />
yanayogusa kitu kinachoitwa ‘fedha.‘<br />
Ni ukweli usiopingika kwamba taifa lina mzigo mkubwa wa majukumu yanayohitaji fedha<br />
hasa katika kutekeleza miradi mbalimbali na mikubwa inayoendelea na ijayo - hapo tunaunga<br />
mkono. Lakini ni swala la kipaumbele pia. Eneo la elimu ya msingi na sekondari sio la<br />
kugusa juu juu. Siku zote, misingi ikiharibika, tujue kwamba huko juu na huko mbeleni<br />
tunaenda kuvuna uharibifu. Uwezekano ni mkubwa wa kuwamwaga mitaani hao wahitimu<br />
wote (walioshindwa) na wakakosa mwelekeo kwa sababu hatujaandaa mazingira (kama taifa<br />
na sio wazazi na walezi pekee) ya kuwafanya wawe na faida kwa jamii, ni sawa na kuzalisha<br />
kwa makusudi kitu au kifaa hatari usichokijua na kukiacha au kukitupa na baadae bila kujua<br />
kinakuja kukudhuru mwenyewe.<br />
Endapo kutakuwa na ongezeko kubwa la walioshidwa kidato cha nne, pasipo kuwepo<br />
mikakati mahususi ya jinsi ya kuwaboresha katika ujuzi na maarifa yanayoendana na uhitaji<br />
wa kiuchumi wa dunia ya sasa, hapo tunaandaa taifa lenye watu wasiozalisha na waharibifu<br />
(vibaka, madawa ya kulevya, wezi, waporaji na majangiri). Taifa lenye watu wengi<br />
waliosoma na wenye ujuzi katika maeneo tofauti tofauti litaendelea haraka kuliko kuwa na<br />
wazurulaji wengi, ambao ni ‘wacheza pooltable asubuhi, walewa viroba siku nzima, wapiga<br />
debe wasio rasmi katika vituo vya mabasi masaa 24.’<br />
Kama mtanzania-mzalendo, ninadiriki kuandika hivi kwa sababu mimi sio mwanasiasa, niko<br />
upande wa utendaji zaidi na hapo haihitaji siasa endapo tunataka kuliweka taifa liendelee<br />
kuwa salama. Ni hatari sana endapo taifa halitachukua hatua zenye tija katika kuzuia<br />
ongezeko la watu wasiozalisha kitu katika jamii. Kwa sababu mtoto anatakiwa angalau kwa<br />
jitihada zote zilizowekwa (kwa miaka minne shuleni) basi apate alama ambazo itakuwa rahisi<br />
6
kumuwezesha aidha kuendelea na masomo, kuendelea na masomo ya ufundi stadi au kujenga<br />
mazingira ya mtoto huyo aondoke shulani akiwa na ujuzi katika eneo fulani ili akienda<br />
mitaani basi ikawe rahisi kuwezeshwa. Na hilo ndilo eneo lililo nje ya mkondo wa taaluma<br />
hasa kwa kuzingatia vipawa na karama walizonazo wanafunzi mashuleni. Ikumbukwe kuwa<br />
moja ya mahitaji ya taifa ili liendelee linahitaji kuwa na rasilimali watu (nguvu kazi<br />
iliyoelimika na yenye ujuzi wa kutosha).<br />
Na hapa ndipo tunaelewa msisitizo wa kufanya kazi unaotolewa mara kadhaa na Raisi, ndugu<br />
John pombe magufuli akisema “mimi nataka watu wafanye kazi.” Ikimaanisha kwamba<br />
tukifanya kazi kwa bidii, hatutasubiri wakati wote misaada toka nje ili tufanye au tupate<br />
maendeleo, hatutaomba chakula cha msaada toka nje, kama ni chakula basi tutazalisha kwa<br />
wingi na kubakiwa na ziada (excess) ambacho kitatoka nje (kwa utaratibu sahihi) ili tupate<br />
fedha za kigeni. Kwa mantiki hiyo, inatukumbusha kuwa rasilimali watu nyingine<br />
inaandaliwa shuleni. Shuleni ndio mazingira yanayotakiwa kupika, kupakuwa na<br />
kuwamwaga hao wataalamu katika maeneo husika. Lakini kama hawakuiva, basi wanatupwa<br />
jalalani (mitaani), nao wanaanza kutafuta mazingira ya kula bila kufanya kazi. Tayari huo ni<br />
mzigo tuliozalisha wenyewe.<br />
Kwa mujibu wa sera ya Elimu na mafunzo (2014) inabaini jitihada na malengo ya sekta ya<br />
elimu (ambayo mimi ninaita “JIKONI” kwa sababu ndio sekta mama katika kuzalisha, kulea<br />
na kukuza rasilimali watu na kada zote zinatoka hapo). Hivyo sekta ya elimu na mafunzo,<br />
kwa mujibu wa dira ya maendeleo ya taifa 2011/2012 hadi 2024/25, ilitarajiwa na inaendelea<br />
kutarajiwa kuleta maendeleo ya haraka ya rasilimali watu kwa kutayarisha idadi ya kutosha<br />
ya watanzania walioelimika na kupenda kujielimisha zaidi ili kulifanya taifa lipate maendeleo<br />
na kuwa lenye uchumi wa kati na baadae iwezekane kuwa na uchumi wa juu.<br />
7
Ninanukuu maelezo ya sera ya elimu, yanasema; ‘kumekuwa na changamoto katika kuinua<br />
ubora wa elimu na mafunzo kutokana na mitaala katika ngazi mbalimbali za elimu na<br />
mafunzo kutokidhi mahitaji ya mabadiliko ya kiuchumi, kijamii, kisayansi na teknolojia na<br />
hivyo kutoa wahitimu ambao hawana umahiri wa kutosha kuhimili ushindani katika<br />
ulimwengu wa kazi.’<br />
Moja ya mabadiliko katika upepo wa kimaendeleo katika jamii ni msisitizo katika sera ya<br />
viwanda, ambao umetoa fursa kwa wananchi na wawekezaji (ndani na nje) kupatiwa maeneo<br />
(ardhi) kwa masharti nafuu ili kuanzisha na kuendeleza viwanda. Sasa hali hii inaonyesha<br />
umuhimu wa kuweka mabadiliko na mkazo (mitaala) katika utoaji wa elimu inayokidhi<br />
mahitaji hayo ya sasa ili kuandaa taifa lenye mtazamo wa kiviwanda toka wakiwa shule ya<br />
msingi na sekondari.<br />
Na badiliko lingine katika jamii ni ongezeko kubwa la watu na uhaba wa ajira (ajira rasmi).<br />
Kwa mfano walimu wa masomo ya sanaa mpaka sasa hawajaingia katika ajira ya serikali<br />
toka mwaka 2015. Lakini vyuo vinaendelea kuzalisha idadi kubwa ya walimu hao wa sanaa<br />
ambao wanaendelea kuingia mitaani na vyeti na taaluma zao wakitegemea ajira mpya<br />
serikalini na sekta binafsi. Na wakati ajira hiyo imesimama, bado kumekuwa na ongezeko la<br />
idadi ya wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza na pia shule ya msingi.<br />
Hapo pia naweka angalizo. Uandaliwe mfumo wa kuwafanyia usahili walimu wanaohitaji<br />
kuingia ajira ya serikali. Kwa sababu haiwezekani na haiingii akilini kuwa tuna idadi kubwa<br />
sana ya walimu wahitimu wa vyuo vikuu na diploma mitaani lakini bado hakuna utaratibu<br />
wenye manufaa wa kuwachuja ili kuwapata walimu bora na kuwapa ajira. Unajua, hatuhitaji<br />
kuwa na bora walimu, ila walimu bora. Sasa hivi vyuo ni vingi na wengine wameenda<br />
kusomea ualimu na kuingizwa kwenye ajira ya ualimu ili kutafuta riziki tu (watu wa<br />
mshahara) lakini mwito na uwezo wa kumsaidia mtoto hasa kitaaluma hana.<br />
8
Ushauri wangu kwa Serikali ni kuwa kila halmashauri iwe na kitengo hicho (ikiwezekana<br />
watu wa HR na TSC); usahili ufanyike angalau mara mbili kwa mwaka kwa kila<br />
halmashauri) na kuandaliwa database ya walimu wenye sifa (wanaohitaji ajira) baada ya<br />
kufanyiwa usahili na kupeleka majina na taarifa zao TAMISEMI (hiyo inawezekana kama<br />
kweli tunataka kuingia gharama ambayo inamanufaa kwa hatima njema ya elimu yetu. Hili<br />
pia ni katika kuandaa mazingira yenye tija katika kuandaa taifa lijalo la uchumi wa viwanda.<br />
Maana msingi mkuu ni kuimarisha utoaji wa elimu bora.<br />
Na kama utatumia kigezo cha GPA tu ili kubaini mwalimu bora basi hapo ndio utapotea<br />
kabisa. Ualimu sio GPA peke yake. Humu mitaani kuna waalimu ni darasa la saba wa<br />
zamani, lakini wanauwezo wa kumsaidia mtoto wa darasa la kwanza kwa usahihi kuliko huyu<br />
mwalimu mwenye degree ya kwanza ya ualimu (ijapokuwa tunawatambua hao wa mitaani<br />
kuwa wanawaharibia msingi watoto kwa mfano kwenye kanuni kama za kufundisha<br />
kingereza na hesabu). Lakini ni bora kumchukua huyu wa mitaani na kumpeleka chuo ili<br />
akajue kanuni za ufundishaji na kumjengea uwezo na kumfanya awe mwalimu rasmi. (huo ni<br />
mfano tu).<br />
Kwa swala la kuwafanyia walimu usahili, changamoto inakuja katika kudhibiti rushwa na<br />
undugu. Hapo pia inatakiwa kuwekwa mazingira magumu ya kuchukuana kindugu au kwa<br />
rushwa. Lakini kama zitawekwa sheria kali, inawezekana kulitekeleza hilo (na kupunguza<br />
sana kubebana katika ajira) kwa sababu hitaji letu ni kuona kuwa ualimu sio ‘dampo’ la<br />
kupokea kila mtu aliyekosa kwa kwenda. Ualimu ni taaluma na lazima iheshimiwe, na<br />
serikali iwe na uhakika kuwa imeajiri nguvu kazi yenye kutaka kuleta mabadiliko. Hata<br />
ikiwapa motisha, iwe na uhakika kuwa hiyo motisha imeelekezwa katika mkondo wa watu<br />
sahihi wanaostahili.<br />
9
Zipo sababu nyingi za shule binafsi kufanya vizuri kuliko za serikali kwa sasa, lakini sababu<br />
moja wapo ni kuwafanyia walimu usahili ili kubaini uwezo wao kabla ya kuwapa mkataba au<br />
ajira. Kuna usahili wa kuhojiwa kwa mdomo, wa kuandika na pia usahili wa kuingia<br />
darasani. Yote hayo yafanyike. Hujui kwamba kwa sasa unaweza kuajiri walimu ambao<br />
hawajui kuandika barua ya kuomba kazi. (lakini ile aliyopeleka kuomba kazi aliandikiwa na<br />
mtu mwingine).<br />
Ikumbukwe kuwa elimu ndio nyenzo pekee ya kubadili mawazo, fikra na mitazamo ya watu<br />
ili kuzalisha na kuharakisha matokeo chanya katika jamii na mazingira yanayomzunguka<br />
mwanamchi huyu. Na njia pekee ni kupatiwa elimu kwa njia rasmi na isiyo rasmi<br />
ili<br />
kupata/kupanua maarifa na ufahamu kutoka kwa wataalamu na wanataaluma<br />
Sera yetu ya elimu inayotekelezwa sasa inabaini pia kuwa kuna idadi kubwa ya wataalamu<br />
walioelimika kwa kiwango cha juu wanaohitajika ili Tanzania kufikia kiwango cha nchi<br />
yenye uchumi wa kati huku taarifa zinaonyesha kwamba rasilimali watu ya Tanzania, kwa<br />
kiasi kikubwa ni wafanyakazi wenye ujuzi wa chini ambao ni asilimia 84, wakifuatiwa na<br />
wenye ujuzi wa kati asilimia 13 na wenye ujuzi wa juu asilimia 3. Hata hivyo, kwa nchi za<br />
kipato cha kati ngazi ya chini, ulinganifu unaonyesha kuwa nchi hizo zina wastani wa<br />
asilimia 55 ya wafanyakazi wenye ujuzi wa chini, asilimia 33 ujuzi wa kati na asilimia 12<br />
ujuzi wa juu. Hivyo, Tanzania ina changamoto ya kuinua mchanganyiko wa wafanyakazi<br />
wenye ujuzi katika fani mbalimbali ili kufikia mahitaji ya rasilimaliwatu kwa nchi ya kipato<br />
cha kati kufikia mwaka 2025.<br />
Sasa, ili kuweza kuyafikia malengo haya pasipo shida, ni muhimu kushughulika hasa kwa<br />
kuanzia elimu ya msingi na sekondari (hapo ni swala la mitaala). Ijapokuwa watoto wa shule<br />
ya msingi na sekondari, hawapatiwi (kulingana na mitaala) elimu ya kujitegemea inayoweza<br />
kuwaandaa kwa ajili ya kuyakabili mazingira ya kazi yajayo hasa ikizingatiwa kuwa umri<br />
10
wao pia ni mdogo lakini bado tunajukumu kubwa lisilokwepeka la kuanzia msingi na<br />
sekondari kutoa elimu inayoweza kubadili mtazamo na fikra kuwa maisha ya shule<br />
yanatuandaa kwa ajili ya kufanya kazi za uzalishaji mali kwa njia ya kujitegemea (ajira<br />
binafsi). Mwanafunzi ajue kuwa anasoma hata kufikia (kidato cha nne au sita) ili aje<br />
kufanikiwa kuwa fundi cherehani (kushona nguo) na kuwa na kiwanda kidogo cha kuajiri<br />
wengine.<br />
Kazi hata ya kushona viatu na ndala na kubrashi maeneo ya mjini/mitaani inafanywa na idadi<br />
kubwa ya watu ambao hawakupata fursa ya kwenda shule au waliishia darasa la saba la<br />
zamani kidogo. Inaonekana si kazi yenye kufaa kwa wasomi kwa sababu ni matokeo ya<br />
elimu ya nadharia toka shuleni msingi.<br />
Kama ilivyokuwa hapo nyuma, swala la kilimo (mkulima-kushinda kwenye matope),<br />
haikuwa rahisi kufanywa na msomi wa chuo kikuu. Bali na wale waliokosa fursa ya elimu.<br />
Na hata yule mtaalamu wa kilimo (wengine maafisa kilimo) wakijifungia ofisini ili kusubiri<br />
wateja wawafuate, na kusubiri vikao ofisini na si kwenda kushida kwenye mapori, nyasi na<br />
matope ili wakatoa elimu kwa wakulima namna ya kufanya kilimo chenye tija. Hiyo yote ni<br />
mitazamo na fikra ambazo mtanzania ametoka nazo shule ya msingi.<br />
Lakini ukweli ni kwamba kazi ndogo ndogo kama hiyo ikifanywa na msomi inaweza<br />
kufanywa kwa umaridadi wa kiwango cha juu na kuleta mapinduzi katika sekta ndogo ndogo.<br />
Ni kama vile kumchukua profea wa chuo kikuu aende kufundisha shule ya msingi kwa<br />
watoto wanaotoa kamasi. Inakuwa ngumu kidogo (hata kama ataboreshewa mazingira ya<br />
kazi) na kupatiwa mshahara na marupurupu yale yale anayoyapata kule chuoni. Inatakiwa<br />
awe mzalendo. Ingawa tutasema kuwa kutokana na uhaba wa maprofesa chuo kikuu basi<br />
11
awaachie hao walimu wa cheti, diploma na degree wafanye kazi ya kufundisha shule ya<br />
msigni ambayo ni ya kwango chao. Kwa sababu itakuwa ni matumizi yasiyo sahihi ya<br />
rasilimali watu.<br />
Lakini pia mhandisi, akipewa ekari tano (kwa mfano) ili aziendeleze katika kuzalisha zao<br />
fulani, uwezekano wa kumudu hiyo kazi na kuleta matokeo chanya ni mkubwa kwa sababu<br />
tunategemea kuwa ana uwezo mkubwa wa kuelewa na kufuata maelekezo ya wataalamu wa<br />
kilimo. Zaidi ya hayo anafursa ya kujisomea na kujua kanuni nyingi zaidi za kilimo na<br />
kubadilika kulingana na mazingira na mahitaji katika kazi yake ya ukulima. Akienda kwenye<br />
duka la pembejeo kunakuwa na uwezekano mdogo wa kuzulumiwa au kuuziwa viwatilifu<br />
vilivyokwisha muda kwa sababu anauwezo wa kisomi (wa kubaini mambo) na kufanya tafiti<br />
kwa wahusika kama TFDA na kujua ukweli wa bidhaa. Msomi ana ujasiri wa kufuatilia na<br />
kuhoji ili kujua ukweli.<br />
Sasa, elimu ya uchumi wa viwanda inatakiwa kuingizwa katika mfumo rasmi mashuleni ili<br />
tufanikiwe katika harakati hizo na kubadili mtazamo na fikra kuanzia shule ya msingi na<br />
sekondari-hapo siongelei elimu ya nadharia bali kujitegema. Uhamasishaji usiishie mitaani na<br />
kwenye vyombo vya habari tu … hivyo kwa wakati huu, wengi wasiosoma ndio wanaelimu<br />
ya kutosha na kwa kuwa walikuwa na msingi ambao haukuwezeshwa na sera ya taifa ya<br />
viwanda hapo nyuma. Hii inamaanisha kuwa wakati ujao huyo mwenye vyerehani vitano vya<br />
kushonea nguo ndio atakuja kuajiri hao waliokwenda shule na kuhitimu lakini wakakosa sifa,<br />
kwa sababu hao walioshuleni sasa wanafikra kuwa watasoma ili waje kuajiriwa.<br />
Wazo langu pia ni kufikiri namna ambavyo tunaweza kuunganisha elimu ya sekondari na<br />
vyuo kama VETA au vyuo vilivyosajiliwa na VETA. Mazingira hayo yatumike kama sehemu<br />
12
ya kufanya mazoezi kwa kazi ndogo za ujuzi hasa kwa watoto wa sekondari (natambua ni<br />
gumu kutekelezeka.) lakini itambulike kuwa watoto wanauwezo mkubwa wa kushughulika na<br />
vitendo kuliko nadharia endapo tu wataandaliwa mazingira na kujengewa uwezo. Hata kama<br />
mtoto anashida kidogo ya akili lakini ukimpeleka kwenye maeneo ya kushika SPANNER,<br />
uzoefu unaonyesha kuwa anaweza kuendana na mazingira hayo ya ufundi na polepole kupata<br />
ujuzi na baadae kuimudu hiyo na kuifurahia kuliko kushinda kumlazimisha aelewe (kukariri)<br />
sheria za Newton wakati ubonngo wake umegoma.<br />
Hilo nina uhakika nalo (endapo utekelezaji wake ungekuwa rahisi). Hebu jaribu kumchukua<br />
dereva aliyelewa (mlevi) mpaka kufikia kiwango cha kushikwa mikono kwa sababu hawezi<br />
kutembea mwenyewe. Sasa mchukue (kumbeba) na kumuweka kwenye kiti cha gari yake ili<br />
awashe injini na kuendesha. Atafanikiwa kufuata kanuni zote mpaka kuanza kuendesha gari<br />
ingawa usalama utakuwa mdogo akiishaingia barabarani.<br />
Lakini huyo huyo dereva jaribu kumpa maswali yanayohusu taaluma yake ya udereva na<br />
ayajibu kwa kuandika, uhakika ni kuwa atashindwa kuyajibu. Kwa sababu hapo ameingia<br />
kwenye nadharia na sio vitendo.<br />
Hivyo katika kuandaa wanafunzi katika mabadiliko ya kiuchumi na kijamii, kuna jukumu la<br />
kuendelea kupeleka na kufikisha elimu ya kutosha kwa (jamii) wazazi. Mzazi/mlezi<br />
anapaswa kuandaa mazingira ya kujua mtoto wake anapendelea kufanya nini (kazi gani)<br />
katika maisha. Kwa sababu maono ya maisha yajayo pia hayaanzii ukubwani tu, pia utotoni<br />
(kulingana na mazingira) Na hiyo itasaidia kubaini mwelekeo wa mtoto na pia kuanza<br />
kutengeneza mazingira ya kumwendeleza huyo mtoto. Ijapokuwa sio watoto wote watakuwa<br />
na wazo hilo lakini ni sehemu ya jukumu la wazazi, walezi na jamii kwa ujumla kuanza<br />
13
mapema kutengeneza au kuandaa kipawa kwa mtoto wake. Na shuleni ndio mahali pa<br />
kuviendeleza (mfumo rasmi) pia endapo mazingira yataruhusu (kimtaala na uwekezaji).<br />
Mataifa yaliyoendelea yametushinda hapo, kumuandaa mtoto akiwa bado mdogo katika<br />
kumtengenezea njia aje kuwa mtaalamu au fundi mwenye ujuzi utokanao na kipawa katika<br />
eneo Fulani. Na hii ndio siri kubwa ya mafanikio yao katika sekta ya michezo. Kwa mfano<br />
kumtengenezea bwawa la kuogelea na kumfundisha mtoto wa umri wa miaka 4 ili ajue<br />
kuogelea. Au kumuandaa mtoto huyo awe mchezaji mpira wa miguu. Mtoto huyo akitimiza<br />
umri wa miaka kumi (10) atakuwa tayari ni mchezaji mwenye kipaji ambacho kilianzia<br />
utotoni pale nyumbani kwa wazazi au walezi. Wakati huku kwetu (mataifa mengi ya afrika),<br />
mtoto wa miaka kumi ndio anaanza kuonekana kwa mbali akiwa shuleni kuwa anawezo wa<br />
kuja kuwa mchezaji mpira mzuri. Na hapo wazazi hawajui na hawana taarifa yoyote juu ya<br />
kipaji cha mtoto wao.<br />
Sasa hapo ndio tunategemea kwamba taifa kama letu Tanzania tunaweza kushindana na timu<br />
ya taifa ya wakubwa ya brazil au ujerumani. Wachezaji wetu hawa walioanza kutambulika<br />
kuwa na kipaji cha kucheza mpira walipoanza kusoma shule, tena sekondari. Inakuwa ngumu<br />
kidogo.<br />
Ikumbukwe kwamba mzazi au mlezi anaouwezo wa kuamua kumuandalia mtoto wake awe<br />
mwana sheria, mkandarasi, dereva, mcheza mpira, mwanariadha akiwa bado shule ya msingi.<br />
Na hapo ndio chimbuko la kupata taifa lisilo teteleka katika nguvu kazi kwenye maeneo ya<br />
uzalishaji. Hii ndio maana kama mzazi ni mwana siasa basi asilimia kubwa atakuwepo motto<br />
wake mwanasiasa. Kama mzazi ni mjasiriamali basi atakuwepo mtoto wa kufuata nyayo hizo<br />
14
za ujasiriamali. Kama mzazi ni mkulima basi hivyo hivyo atakuwepo mtoto mkulima katika<br />
wale.<br />
Changamoto kwa watanzanai na waafrika kiujumla ni kuwa hatuna utamaduni huo wa<br />
kumuandaa mtoto katika mazingira ya kutambua (kuibua) vipawa alivyonavyo akiwa angali<br />
katika umri mdogo. Pia hatuna utamaduni wa kujisomea mambo ya msingi (vitabu/hadithi ili<br />
kupanua mawazo), ufukara wa kijamii, kukosa elimu na pia mazingira duni ambayo hayafai<br />
kuandaa watoto wakiwa bado na umri mdogo pale nyumabni (katika jamii). Hayo yote ni<br />
changamoto katika safari ya kuandaa taifa la uchumi wa kati.<br />
Kwa mpango wa miaka mingi ijayo kwa mfano (kuanzia muongo mmoja hivi), mafanikio<br />
katika kumuandalia mwanafunzi mazingira rafiki pale nyumbani (jamii) na shuleni (mitaala)<br />
yatasaidia kuibua vipawa na kuviendeleza na hilo litarahisisha kupunguza idadi ya watoto<br />
wanaokuja kuhitimu kidato cha nne wakiwa hawana mwelekeo wa kufanya kitu (kuzalisha<br />
mali) hasa baada ya eneo la taaluma kushindikana.<br />
Hapo sijagusia swala la kipingamizi cha sheria ya ajira kwa watoto chini ya umri wa miaka<br />
kumi na nne (14), na wale wenye umri kati ya kumi na nne mpaka kumi na saba (14-17),<br />
ambapo kundi hili (14-17), ndilo linabeba wahitimu wengi wa kidacho cha nne kwa sasa.<br />
Ingawa (kwa mtazamo wangu) sheria ya kumbada mtoto wa umri huo (14-17), kufanya kazi<br />
nyepesi unatoa fursa moja kwa moja kuingia katika ulimwengu wa kazi endapo ana ujuzi.<br />
MUNGU LIBARIKI TAIFA LETU LA <strong>TANZANI</strong>A<br />
0719194900 ////// 0738753217<br />
15