You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
UTANGULIZI<br />
Karibu Mkoa wa Simiyu. Mwongozo wa Uwekezaji wa mkoa wa Simiyu<br />
umeandaliwa sambamba na sera ya uwekezaji ya Tanzania. Unaainisha<br />
fursa za uwekezaji zinazopatikana katika mkoa wa Simiyu. Vile vile<br />
unaendana na dira ya mkoa wa Simiyu kama ilivyoelezwa na Mheshimiwa<br />
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dr. John Pombe Magufuli wa Tanzania<br />
mnamo tarehe 11, Januari 2017, na umeandaliwa kulingana na mifumo<br />
ya kimaendeleo ya kitaifa kama vile Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na<br />
Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016-2021 (FYDP II).<br />
Mwongozo huu wa uwekezaji unatoa taarifa za uwekezaji kwa makampuni<br />
ya uwekezaji ya hapa nchini, ya nchi za nje na watu binafsi. Vile vile,<br />
Mwongozo unaainisha rasilimali na kubainisha fursa za uwekezaji zilizopo<br />
katika mkoa wa Simiyu ili kuchochea biashara, maendeleo na ukuaji wa<br />
uchumi. Pia Mwongozo unadhamiria kukuza uwezo wa ushindani wa<br />
Mkoa wa Simiyu katika maeneo ambayo Mkoa una fursa za kiuchumi.<br />
Madhumuni mengine ni kukuza uwezo wa uzalishaji katika sekta muhimu<br />
za msingi ili kuleta maendeleo endelevu yatakayochangia kukua kwa pato<br />
la jumla la Taifa na ustawi wa mkoa wa Simiyu.<br />
Kwa hiyo, mkoa wa Simiyu na wilaya zake na Serikali za Mitaa: Bariadi,<br />
Busega, Itilima, Maswa, na Meatu wamedhamiria kutoa kipaumbele katika<br />
uwekezaji na kutoa huduma stahiki na motisha za kuvutia kwa wawekezaji<br />
katika Mkoa. Zaidi ya hayo, Ofisi ya Mkoa wa Simiyu na mamlaka zake<br />
za Serikali za Mitaa wataandaa mipango mwafaka na mazingira bora ya<br />
uendeshaji na ya kibiashara na watakuwa wanapatikana wakati wote ili<br />
kutoa maelezo zaidi kuhusu fursa zilizopo kwa wawekezaji wenye nia ya<br />
kuwekeza.<br />
Napenda kulipongeza Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)<br />
kwa msaada wa kifedha na utaalamu, pia Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na<br />
Kijamii (ESRF) kwa kuandaa Mwongozo huu. Napenda pia, kuwashukuru<br />
<strong>MWONGOZO</strong> <strong>WA</strong> <strong>UWEKEZAJI</strong> <strong>MKOANI</strong> <strong>SIMIYU</strong> | iii