24.03.2017 Views

MWONGOZO WA UWEKEZAJI MKOANI SIMIYU

mwongozo-simiyu

mwongozo-simiyu

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

UTANGULIZI<br />

Karibu Mkoa wa Simiyu. Mwongozo wa Uwekezaji wa mkoa wa Simiyu<br />

umeandaliwa sambamba na sera ya uwekezaji ya Tanzania. Unaainisha<br />

fursa za uwekezaji zinazopatikana katika mkoa wa Simiyu. Vile vile<br />

unaendana na dira ya mkoa wa Simiyu kama ilivyoelezwa na Mheshimiwa<br />

Rais wa Jamhuri ya Muungano Dr. John Pombe Magufuli wa Tanzania<br />

mnamo tarehe 11, Januari 2017, na umeandaliwa kulingana na mifumo<br />

ya kimaendeleo ya kitaifa kama vile Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 na<br />

Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016-2021 (FYDP II).<br />

Mwongozo huu wa uwekezaji unatoa taarifa za uwekezaji kwa makampuni<br />

ya uwekezaji ya hapa nchini, ya nchi za nje na watu binafsi. Vile vile,<br />

Mwongozo unaainisha rasilimali na kubainisha fursa za uwekezaji zilizopo<br />

katika mkoa wa Simiyu ili kuchochea biashara, maendeleo na ukuaji wa<br />

uchumi. Pia Mwongozo unadhamiria kukuza uwezo wa ushindani wa<br />

Mkoa wa Simiyu katika maeneo ambayo Mkoa una fursa za kiuchumi.<br />

Madhumuni mengine ni kukuza uwezo wa uzalishaji katika sekta muhimu<br />

za msingi ili kuleta maendeleo endelevu yatakayochangia kukua kwa pato<br />

la jumla la Taifa na ustawi wa mkoa wa Simiyu.<br />

Kwa hiyo, mkoa wa Simiyu na wilaya zake na Serikali za Mitaa: Bariadi,<br />

Busega, Itilima, Maswa, na Meatu wamedhamiria kutoa kipaumbele katika<br />

uwekezaji na kutoa huduma stahiki na motisha za kuvutia kwa wawekezaji<br />

katika Mkoa. Zaidi ya hayo, Ofisi ya Mkoa wa Simiyu na mamlaka zake<br />

za Serikali za Mitaa wataandaa mipango mwafaka na mazingira bora ya<br />

uendeshaji na ya kibiashara na watakuwa wanapatikana wakati wote ili<br />

kutoa maelezo zaidi kuhusu fursa zilizopo kwa wawekezaji wenye nia ya<br />

kuwekeza.<br />

Napenda kulipongeza Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)<br />

kwa msaada wa kifedha na utaalamu, pia Taasisi ya Utafiti wa Kiuchumi na<br />

Kijamii (ESRF) kwa kuandaa Mwongozo huu. Napenda pia, kuwashukuru<br />

<strong>MWONGOZO</strong> <strong>WA</strong> <strong>UWEKEZAJI</strong> <strong>MKOANI</strong> <strong>SIMIYU</strong> | iii

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!