Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
inajumuisha Wilaya za Bariadi, Busega na Itilima, zenye topografia ya kupanda<br />
na kushuka zenye udongo mfinyanzi na udongo wa juu mweupe. Kiasi cha<br />
mvua ni baina ya mm 700 - 900. Shughuli kuu ya kiuchumi katika kanda<br />
hii ni pamoja na kilimo cha mazao hasa mahindi, mtama, pamba, muhogo<br />
na ufugaji. Kanda ya pili inajumuisha Wilaya ya Meatu yenye topografia ya<br />
kupanda na kushuka na kupindapinda upande wa Mashariki wenye udongo<br />
mfinyanzi wenye rutuba. Kanda hii ina mmomonyoko mbaya wa udongo<br />
unaopunguza kilimo cha mazao. Kiasi cha mvua kwa kawaida ni chini ya mm<br />
700 chenye tabia isiyotabirika. Kilimo cha mazao na ufugaji ndiyo shughuli<br />
kuu za kiuchumi katika eneo hili. Mazao makuu yanayolimwa katika eneo hili<br />
ni pamoja na mtama, pamba na mahindi. Kanda ya tatu inajumuisha Wilaya<br />
ya Maswa yenye topografia ya kupanda na kushuka na ya kupindapinda.<br />
Ardhi yake ni ya udongo wa Usukumani maarufru kwa jina la mbuga, udongo<br />
mfinyanzi mweusi wa tifutifu ambao ni mzuri kwa kilimo cha mpunga. Mazao<br />
mengine yanayolimwa katika eneo hili ni pamoja na mahindi, mtama na<br />
pamba. Kanda hii ina kiasi cha mvua kisichoaminika kati mm 700 hadi mm<br />
800 kwa mwaka. Eneo hili ni maarufu pia kwa shughuli za ufugaji.<br />
Kielelezo 1.1: Ramani ya Mkoa wa Simiyu<br />
6 | <strong>MWONGOZO</strong> <strong>WA</strong> <strong>UWEKEZAJI</strong> <strong>MKOANI</strong> <strong>SIMIYU</strong>