TPCC Annual Report 2008.indd - HeidelbergCement
TPCC Annual Report 2008.indd - HeidelbergCement
TPCC Annual Report 2008.indd - HeidelbergCement
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Tanzania Portland Cement Company Ltd, <strong>Annual</strong> <strong>Report</strong> 2008<br />
Taarifa ya Wakurugenzi kwa Mwaka ulioishia<br />
31 Desemba 2008<br />
Wakurugenzi wanayo furaha kuwasilisha taarifa yao pamoja na hesabu zilizokaguliwa kwa mwaka ulioishia 31 Desemba<br />
2008.<br />
Shughuli kuu<br />
Shughuli kuu ya Kampuni ni uzalishaji, usambazaji na uuzaji wa saruji.<br />
Wajibu wa Wakurugenzi<br />
Kwa mujibu wa Sheria ya Makampuni Na.12 ya mwaka 2002, ni wajibu wa wakurugenzi kuandaa hesabu za Kampuni<br />
kila mwaka zenye kutoa hali halisi ya Kampuni kifedha mwishoni mwa kila kipindi.<br />
Wakurugenzi wanathibitisha kwamba katika kutayarisha hesabu ambazo zinaonyesha hali halisi ya Kampuni kila wakati,<br />
wametumia sera na kanuni za kiuhasibu zinazohakikisha kuwa hesabu zinakidhi matakwa ya viwango vya kimataifa vya<br />
utayarishaji hesabu na taarifa za fedha. Hesabu zimeandaliwa kwa kuzingatia kuwa Kampuni itaendelea kufanya shughuli<br />
zake kwa muda mrefu ujao.<br />
Wakurugenzi wanawajibika kutunza vitabu na nyaraka za kiuhasibu zenye kuonyesha hali halisi na sahihi ya Kampuni<br />
na kuhakikisha kuwa hesabu zinazotayarishwa zinaendana na matakwa ya Sheria ya Makampuni Na.12 ya mwaka 2002.<br />
Wanawajibika pia kuhakikisha kwamba mali zote za Kampuni ziko katika hali ya usalama na kuweka mifumo ya udhibiti<br />
wa shughuli za Kampuni inayofanya kazi ya kuzuia au kugundua wizi, ufujaji au makosa kuwa rahisi.<br />
Wakurugenzi<br />
Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wakati huu ambao wamekuwa wajumbe katika kipindi chote cha mwaka 2008 ni<br />
hawa:<br />
Bw. Jean-Marc Junon Mfaransa Mwenyekiti<br />
Bw. Klaus Hvassing Mnorwei Mjumbe<br />
Bw. William Mlaki Mtanzania Mjumbe<br />
Bw. George Fumbuka Mtanzania Mjumbe<br />
Bw. Daniel Gauthier Mbeljiji Mjumbe<br />
Bw. Arne J. Selen Mnorwei Mjumbe mbadala wa Daniel Gauthier<br />
Bw. Ola Schippert Mswedi Mjumbe<br />
Wajumbe wote wa Bodi siyo watendaji katika Kampuni, isipokuwa Bw. Klaus Hvassing ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji.<br />
Wakurugenzi Wanahisa<br />
Bw. William Mlaki ana hisa 49,927 katika Kampuni<br />
22