MAKALA YA BIASHARA YA HEWA UKAA

Ndugu wananchi ni jukumu letu kuhifadhi Misitu kwa Maendeleo ya jamii zetu na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi - Tanzania. Ndugu wananchi ni jukumu letu kuhifadhi Misitu kwa Maendeleo ya jamii zetu na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi - Tanzania.

lungoabdallah
from lungoabdallah More from this publisher
13.04.2021 Views

14 MAKALAHABARILEO, IJUMAA JANUARI 15, 2021Na Budoya NillaHEWA ya ukaa ni biasharapoa na inalipa.Mtu akisikia sentensihiyo kwa mara ya kwanzaanaweza asielewe kitu lakiniukisoma makala haya hadimwisho, bila shaka utaelewa.Kazi kubwa unayotakiwakufanya ili uweze kufanya biasharahii ni kuhifadhi misitu ya asiliiliyo katika eneo lako na kutunzamazingira yako, basi. Misitu ya asiliina uwezo mkubwa wa kufyonzana kuhifadhi hewa ukaa na hewasumu.Ukiwa na misitu hii, ili ufanikishehilo lazima uzuie uharibifukwa maana ya kuhakikisha hakunaukataji miti hovyo, hakuna kufyekamiti, kuchoma misitu na kuzuiakufanya shughuli zingine hatarishikwa uhifadhi wa misitu ikiwemokufyeka misitu kwa ajili ya kufuguamashamba mapya au kuigeuzamalisho ya mifugo.Badala yake matumizi yamisitu yanatakiwa yawe endelevusambamba na kupanda miti mbalimbali katika maeneo yako. Ukiwezakufanya hayo utakuwa sasana uhakika wa kuvuna hewa ukaana kufanya biashara.Pengine unaweza kujiuliza, jebiashara hii ni kama biashara yamahindi au biashara nyingine?Kwamba mtu anaweza kupanda nakuvuna mahindi na kuuza sokoni?Hapana sivyo.Katika biashara hii, mhusikiaanachotakiwa kufanya ni kuhifadhimisitu ya asili iliyo katika eneolake, basi.Kwa hatua hiyo, taasisi ya CarbonTanzania watamtafutia watejaduniani wanaotoa ruzuku kwawanaofaya uhifadhi huo.Biashara hii imeingia katikaMkoa wa Katavi, hususani katikaHalmashauri ya Wilaya ya Tanganyikana tayari wananchi 21,000katika vijiji vinane walio katikahalmashauri hiyo wamenufaika namradi wa hewa ukaa.Hii ni baada ya kuivuna na kulipwakiasi cha shilingi milioni 380kupitia Carbon Tanzania chini yamradi uitwao Ntakata MountainsRedd Plus Project.Wananchi katika wilaya hiyowamezuia uharibifu wa misituwaliyoihifadhi ili iwasaide kutunzamazingira ikiwemo kufyonza hewaukaa na hewa sumu iliyo katikaanga la nchi yetu na nje ya nchi.Kutokana na uhifadhi huo, vijijihusika vimevuna jumla ya tani82,000 za hewa ukaa na kuiuza kwathamani ya shilingi 250,000,000.Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homera akishiriki upandaji mitikutunza mazingaira.Biashara ya hewa ukaainavyowanufaisha KataviMwakilishi wa Carbon Tanzania, Frank Kweka akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homerahundi yenye thamani ya Sh milioni 225 fedha inayotokana na mauzo ya hewa ya ukaa.Pamoja na uvunaji wa tani hizo,mauzo yake hayajafikia hata nusuya tani 270,000 ambazo bado hazijauzwa.Tarehe 2/5/2020 na 12/11/2020kiasi cha Sh milioni 130 zilitolewakama motisha na wadau mbalimbali wa uhifadhi kwa vijiji kablaya kupata wateja na vyeti vya uuzajiwa hewa ukaa na kugawanywakulingana na makubaliano yamradi.Makubaliano hayo yanabainishakuwa asilimia 10 ya fedha zinazopatikanazinaenda kwenye Halmashauriya Wilaya ya Tanganyikaili kugharimia shughuli za usimamizimazingira wakati asilimia 90zinagawiwa kwenye vijiji vilivyokatika mradi ambao unakadiriwakuwa na hekta 230 katika msitu waTongwe Magharibi.Fedha hizo zinatarajiwa kutimikakatika miradi ya maendelao yakijamii na kiuchumi kwa wananchikama vile ujenzi wa madarasa,utengenezaji wa madawati,kujenga vituo vya afya na miradiya kuwaletea wananchi nishati yaumeme.Inaelezewa kuwa ikiwa hewaya ukaa itauzwa kwa wingi na ukamilifuwake uliopo katika misituya vijiji hivyo, kuna uwezekano wavijiji hivyo kulipwa shiligi bilionisita na hivyo wananchi wanatakiwakuendelea kuhifadhi misitu nakutunza mazingira. Miti isikatweovyo wala kuchomwa, waepukekilimo cha kuhamahama na ufugajiusiozingatia tija.Vijiji vilivyonufaika na mauzoya hewa ukaa ni Lugonesi, Mwese,Lwega na Bujombe. Vijiji vinginevilivyo katika mradi wa mauzo yahewa ukaa ni Kapanga, Mpembe,Kagunga na Katuma. Baadhi yavijiji hivyo viko katika Kata yaMwese, Tarafa ya Mwese na vijijivingine viko Kata ya Kasekese.Carbon Tanzania ndio taasisiinayowezesha vijiji hivyo kupatamasoko ya hewa ukaa ipatikanayokatika misitu ya hifadhi za vijiji namaeneo ya malisho.Je, biashara hii ilianzaje? Ilianzabaada ya vijiji vinane kuwekwakwenye mpango wa matumizi boraya ardhi kwa maana ya kupimwamaeneo yao na kuyatenga kamavile eneo la hifadhi ya misitu, eneola kilimo, eneo la makazi, mifugo,huduma za jamii na kadhalika.Yaani wananchi kupitia mkutanowao wa kujiji wanajipangianamna ya kutumia ardhi yaoiliyopimwa kwa faida yao.Matumizi bora ya ardhi ndiochanzo cha mradi wa hewa ya ukaakwa maana ya kutenga maeneo yahifadhi ya misitu na kuilida sawia.Mradi wa Ntakata MountainsRedd Plus Project unalenga kuhifadhimisitu ya asili na kulindabayoanuai zote muhimu hasa zilizohatarini kutoweka ikiwemo sokwe.Mradi pia umejikita katikakukabiliana na mabadiliko yatabianchi, kutunza vyanzo vyamaji, kutunza wanyamapori na kuwawezeshawananchi walio katikavijiji venye uhifadhi wa misitu asilikunufaika na mauzo ya hewa ukaa.Mashuleni wanafuzi hufundishwakwamba sisi binadamuhupumua hewa ya ukaa na baadayehewa hiyo hufyonzwa na mitina kuhifadhiwa kwenye miti naardhini lakini sisi binadamu huvutahewa ya oksijeni inayotolewa namimea.Mbali na hewa tunayopumua,anga letu limejaa hewa ukaa zinazozalishwana shughuli mbalimbaliza mwanadamu hususani viwanda.Uchomaji wa mimea pia husababishahewa ukaa kwenda angani kwanjia ya moshi.Uzalishaji mkubwa wa hewaukaa (kaboni) angani huchocheaathari ya jotogesi na kusababishamabadiliko ya tabianchi.Ongezeko la viwango vya hewaya ukaa na gesi nyingine anganizinazotokana na shughuli za binadamuhusababisha pia kiwango chajoto duniani kuongezeka.Mabadiliko haya yana maanagani? Mabadiliko haya yana maanaya kuongezeka kwa joto duniani,kuwa na misimu ya mvua isiyoaminika,kupata mvua chache aunyingi zinazosababisha mafuriko,utabiri wa majira kuwa mgumuna mvua kunyesha nje ya misimuiliyozoeleka.Hali hii huleta athari katikakilimo, uzalishaji wa chakulakupungua kwa sababu ya uhabawa mvua au mafuriko yanayozoamazao na ongezeko kubwa la joto,milipuko ya magonjwa ya mimeana wadudu waharibifu wa mazaowanaweza kusambaa hata maeneoambayo awali hawakuwepo.Ongezeko la joto duniani limesababishakuyeyuka kwa theluji katikancha za dunia na kusababishaongezeko la kima cha maji baharini.Kimsingi, kasi ya mwanadamukuongeza hewa ukaa angani nikubwa kuliko uwezo wa duniakufyonza gesi hiyo.Ukataji wa misitu kwa sababumbalimbali hupunguza uwezo waardhi kuhifadhi hewa ya ukaa, tunapochomamafuta kwa kuendeshamagari yetu na wakati mwingie kuzalishaumeme kwa njia ya mafutapia tunaongeza hewa ukaa angani.Kwa kuwa kasi ya ongezeko lahewa ukaa angani ni kubwa, kituambacho ni hatari kwa maisha yamwanadamu mintarafu suala lamabadiliko ya tabianchi, wataalamuwamefanya tafiti na kubainikuwa njia moja wapo katika kukabilianana mabadiliko ya tabianchini uhifadhi wa misitu ya asili.Misitu ya asili ina uwezomkubwa wa kutumia hewa ya ukaana hewa sumu kama chakula chake.Misitu ya asili iliyopo katikaHalmashauri ya Tanganyika nimiongoni mwa misiti iliyo nauwezo wa kuchangia katika sualala kabiliana na mabadiliko ya tabianchi.Wananchi mkoani Katavi,watanzania na Waafrika kwa ujumlahatuna budi kuhifadhi misituna kutunza mazingira yetu kwamanufaa yetu na vizazi vilivyo.Tuendelee kutunza mazingira yetukwa kupanda miti mbali ikiwemoya matunda kwa ajili matumizimbambali sambamba na kufyonzahewa ukaa kwa manufaa yetu.Mwandishi wa makala haya niOfisa Habari Mkuu, Ofisi ya Mkuuwa Mkoa wa Katavi.

14 MAKALA

HABARILEO, IJUMAA JANUARI 15, 2021

Na Budoya Nilla

HEWA ya ukaa ni biashara

poa na inalipa.

Mtu akisikia sentensi

hiyo kwa mara ya kwanza

anaweza asielewe kitu lakini

ukisoma makala haya hadi

mwisho, bila shaka utaelewa.

Kazi kubwa unayotakiwa

kufanya ili uweze kufanya biashara

hii ni kuhifadhi misitu ya asili

iliyo katika eneo lako na kutunza

mazingira yako, basi. Misitu ya asili

ina uwezo mkubwa wa kufyonza

na kuhifadhi hewa ukaa na hewa

sumu.

Ukiwa na misitu hii, ili ufanikishe

hilo lazima uzuie uharibifu

kwa maana ya kuhakikisha hakuna

ukataji miti hovyo, hakuna kufyeka

miti, kuchoma misitu na kuzuia

kufanya shughuli zingine hatarishi

kwa uhifadhi wa misitu ikiwemo

kufyeka misitu kwa ajili ya kufugua

mashamba mapya au kuigeuza

malisho ya mifugo.

Badala yake matumizi ya

misitu yanatakiwa yawe endelevu

sambamba na kupanda miti mbali

mbali katika maeneo yako. Ukiweza

kufanya hayo utakuwa sasa

na uhakika wa kuvuna hewa ukaa

na kufanya biashara.

Pengine unaweza kujiuliza, je

biashara hii ni kama biashara ya

mahindi au biashara nyingine?

Kwamba mtu anaweza kupanda na

kuvuna mahindi na kuuza sokoni?

Hapana sivyo.

Katika biashara hii, mhusikia

anachotakiwa kufanya ni kuhifadhi

misitu ya asili iliyo katika eneo

lake, basi.

Kwa hatua hiyo, taasisi ya Carbon

Tanzania watamtafutia wateja

duniani wanaotoa ruzuku kwa

wanaofaya uhifadhi huo.

Biashara hii imeingia katika

Mkoa wa Katavi, hususani katika

Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika

na tayari wananchi 21,000

katika vijiji vinane walio katika

halmashauri hiyo wamenufaika na

mradi wa hewa ukaa.

Hii ni baada ya kuivuna na kulipwa

kiasi cha shilingi milioni 380

kupitia Carbon Tanzania chini ya

mradi uitwao Ntakata Mountains

Redd Plus Project.

Wananchi katika wilaya hiyo

wamezuia uharibifu wa misitu

waliyoihifadhi ili iwasaide kutunza

mazingira ikiwemo kufyonza hewa

ukaa na hewa sumu iliyo katika

anga la nchi yetu na nje ya nchi.

Kutokana na uhifadhi huo, vijiji

husika vimevuna jumla ya tani

82,000 za hewa ukaa na kuiuza kwa

thamani ya shilingi 250,000,000.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homera akishiriki upandaji miti

kutunza mazingaira.

Biashara ya hewa ukaa

inavyowanufaisha Katavi

Mwakilishi wa Carbon Tanzania, Frank Kweka akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Juma Homera

hundi yenye thamani ya Sh milioni 225 fedha inayotokana na mauzo ya hewa ya ukaa.

Pamoja na uvunaji wa tani hizo,

mauzo yake hayajafikia hata nusu

ya tani 270,000 ambazo bado hazijauzwa.

Tarehe 2/5/2020 na 12/11/2020

kiasi cha Sh milioni 130 zilitolewa

kama motisha na wadau mbali

mbali wa uhifadhi kwa vijiji kabla

ya kupata wateja na vyeti vya uuzaji

wa hewa ukaa na kugawanywa

kulingana na makubaliano ya

mradi.

Makubaliano hayo yanabainisha

kuwa asilimia 10 ya fedha zinazopatikana

zinaenda kwenye Halmashauri

ya Wilaya ya Tanganyika

ili kugharimia shughuli za usimamizi

mazingira wakati asilimia 90

zinagawiwa kwenye vijiji vilivyo

katika mradi ambao unakadiriwa

kuwa na hekta 230 katika msitu wa

Tongwe Magharibi.

Fedha hizo zinatarajiwa kutimika

katika miradi ya maendelao ya

kijamii na kiuchumi kwa wananchi

kama vile ujenzi wa madarasa,

utengenezaji wa madawati,

kujenga vituo vya afya na miradi

ya kuwaletea wananchi nishati ya

umeme.

Inaelezewa kuwa ikiwa hewa

ya ukaa itauzwa kwa wingi na ukamilifu

wake uliopo katika misitu

ya vijiji hivyo, kuna uwezekano wa

vijiji hivyo kulipwa shiligi bilioni

sita na hivyo wananchi wanatakiwa

kuendelea kuhifadhi misitu na

kutunza mazingira. Miti isikatwe

ovyo wala kuchomwa, waepuke

kilimo cha kuhamahama na ufugaji

usiozingatia tija.

Vijiji vilivyonufaika na mauzo

ya hewa ukaa ni Lugonesi, Mwese,

Lwega na Bujombe. Vijiji vingine

vilivyo katika mradi wa mauzo ya

hewa ukaa ni Kapanga, Mpembe,

Kagunga na Katuma. Baadhi ya

vijiji hivyo viko katika Kata ya

Mwese, Tarafa ya Mwese na vijiji

vingine viko Kata ya Kasekese.

Carbon Tanzania ndio taasisi

inayowezesha vijiji hivyo kupata

masoko ya hewa ukaa ipatikanayo

katika misitu ya hifadhi za vijiji na

maeneo ya malisho.

Je, biashara hii ilianzaje? Ilianza

baada ya vijiji vinane kuwekwa

kwenye mpango wa matumizi bora

ya ardhi kwa maana ya kupimwa

maeneo yao na kuyatenga kama

vile eneo la hifadhi ya misitu, eneo

la kilimo, eneo la makazi, mifugo,

huduma za jamii na kadhalika.

Yaani wananchi kupitia mkutano

wao wa kujiji wanajipangia

namna ya kutumia ardhi yao

iliyopimwa kwa faida yao.

Matumizi bora ya ardhi ndio

chanzo cha mradi wa hewa ya ukaa

kwa maana ya kutenga maeneo ya

hifadhi ya misitu na kuilida sawia.

Mradi wa Ntakata Mountains

Redd Plus Project unalenga kuhifadhi

misitu ya asili na kulinda

bayoanuai zote muhimu hasa zilizo

hatarini kutoweka ikiwemo sokwe.

Mradi pia umejikita katika

kukabiliana na mabadiliko ya

tabianchi, kutunza vyanzo vya

maji, kutunza wanyamapori na kuwawezesha

wananchi walio katika

vijiji venye uhifadhi wa misitu asili

kunufaika na mauzo ya hewa ukaa.

Mashuleni wanafuzi hufundishwa

kwamba sisi binadamu

hupumua hewa ya ukaa na baadaye

hewa hiyo hufyonzwa na miti

na kuhifadhiwa kwenye miti na

ardhini lakini sisi binadamu huvuta

hewa ya oksijeni inayotolewa na

mimea.

Mbali na hewa tunayopumua,

anga letu limejaa hewa ukaa zinazozalishwa

na shughuli mbalimbali

za mwanadamu hususani viwanda.

Uchomaji wa mimea pia husababisha

hewa ukaa kwenda angani kwa

njia ya moshi.

Uzalishaji mkubwa wa hewa

ukaa (kaboni) angani huchochea

athari ya jotogesi na kusababisha

mabadiliko ya tabianchi.

Ongezeko la viwango vya hewa

ya ukaa na gesi nyingine angani

zinazotokana na shughuli za binadamu

husababisha pia kiwango cha

joto duniani kuongezeka.

Mabadiliko haya yana maana

gani? Mabadiliko haya yana maana

ya kuongezeka kwa joto duniani,

kuwa na misimu ya mvua isiyoaminika,

kupata mvua chache au

nyingi zinazosababisha mafuriko,

utabiri wa majira kuwa mgumu

na mvua kunyesha nje ya misimu

iliyozoeleka.

Hali hii huleta athari katika

kilimo, uzalishaji wa chakula

kupungua kwa sababu ya uhaba

wa mvua au mafuriko yanayozoa

mazao na ongezeko kubwa la joto,

milipuko ya magonjwa ya mimea

na wadudu waharibifu wa mazao

wanaweza kusambaa hata maeneo

ambayo awali hawakuwepo.

Ongezeko la joto duniani limesababisha

kuyeyuka kwa theluji katika

ncha za dunia na kusababisha

ongezeko la kima cha maji baharini.

Kimsingi, kasi ya mwanadamu

kuongeza hewa ukaa angani ni

kubwa kuliko uwezo wa dunia

kufyonza gesi hiyo.

Ukataji wa misitu kwa sababu

mbalimbali hupunguza uwezo wa

ardhi kuhifadhi hewa ya ukaa, tunapochoma

mafuta kwa kuendesha

magari yetu na wakati mwingie kuzalisha

umeme kwa njia ya mafuta

pia tunaongeza hewa ukaa angani.

Kwa kuwa kasi ya ongezeko la

hewa ukaa angani ni kubwa, kitu

ambacho ni hatari kwa maisha ya

mwanadamu mintarafu suala la

mabadiliko ya tabianchi, wataalamu

wamefanya tafiti na kubaini

kuwa njia moja wapo katika kukabiliana

na mabadiliko ya tabianchi

ni uhifadhi wa misitu ya asili.

Misitu ya asili ina uwezo

mkubwa wa kutumia hewa ya ukaa

na hewa sumu kama chakula chake.

Misitu ya asili iliyopo katika

Halmashauri ya Tanganyika ni

miongoni mwa misiti iliyo na

uwezo wa kuchangia katika suala

la kabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Wananchi mkoani Katavi,

watanzania na Waafrika kwa ujumla

hatuna budi kuhifadhi misitu

na kutunza mazingira yetu kwa

manufaa yetu na vizazi vilivyo.

Tuendelee kutunza mazingira yetu

kwa kupanda miti mbali ikiwemo

ya matunda kwa ajili matumizi

mbambali sambamba na kufyonza

hewa ukaa kwa manufaa yetu.

Mwandishi wa makala haya ni

Ofisa Habari Mkuu, Ofisi ya Mkuu

wa Mkoa wa Katavi.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!