21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kujihusisha na shughuli za kijamii, Mitume walianza kujihusisha na mambo ya kijamii

{kiutawala} kwani shughuli zote za kanisa za kila siku zilifanywa na wao.Tunaona Petro

aliyekuwa mhubiri anaanza kujihusiha na mambo ya kiutwala.

Mitume walifika mahali wakagundua tatizo hilo na wakachagua wahudumu saba

waliotakiwa kushughulikia mambo ya kiutawala ili wao wadumu katika kulihubiri Neno

na Kuomba.

Bwana alilionya kanisa lake “Tubu na ukafanye mambo ya kwanza la sivyo nitakiondoa

kinara chako mahli pake. Mungu alitimiza Neno lake kama Tutakavyo ona hapo baadae.

H. KUENEA KWA KANISA LA KWANZA. Kupanuka kwa kanisa tangu mahubiri ya

Stefano {mwaka 35. AD} hadi mkutano wa Yerusalemu {mwka 48. AD}.Mambo ya

msingi katika kipindi hiki yalikuwa ni upandaji wa makanisa. Kipindi hiki kifupi kilikuwa

na umuhimu mkubwa kwa kanisa. Japokuwa kanisa mwanzo lilikuwa Yerusalemu tu sasa

lilipandwa katika maeneo mengine kama vile Siria na Asia ndogo na kuelekea Ulaya.

Waamini wa kwanza walikuwa ni Wayahudi lakini baada ya kipindi hiki kifupi waamini

wengi walikuwa ni wamataifa .

Mwanzoni Injili ilihubiriwa kwa kiebrani na kwa kiaramu lakini baadae iligundulika

kwamba ulimwengu mzima ungefikiwa na Injili kupitia lugha ya Kigiriki kwa sababu

kigiriki wakati huo kilikuwa ni lugha ya mawasiliano ya kimataifa kama ilivyo

kiingereza kwa dunia ya sasa.

I KUTESWA KWA KANISA NA VIONGOZI WA KIYAHUDI.

Yesu aliwaagiza mitume kwenda kuhubiri Injili duniani kote lakini wao walipenda kukaa

Yerusalemu .Mungu alikasirika na akaamua kuruhusu mateso katika kanisa .{Mdo 9}

1. Mahubiri ya Stefano {.Mdo 6:1-4, 7} Kwa sababu ya imani yake kwa Mungu Stefano

alihukumiwa kuuawa na kuwa mfia dini wa kwanza katika imani ya kikristo. Kijana

mmoja mfarisayo wa Tarso Sauli alishuhudia mauaji ya Stefano na Baadae kijana huyo

akawa kiongozi mkuu wa mauaji ya wakristo katika taifa la wayahudi.

Kutokana na tukio hili waamini wote walikimbia Yerusaelimu isipokuwa mitume {Mdo

8:1-4}.Waamini hao walisambaa maeneo mbalimbali na kila mahali walipokwenda

walilihubiri Neno . Kwa njia hii kwa muda mfupi Injili ilipata kuenea kwa haraka katika

maeneo yote yaliyoizunguka Yerusalemu.

2. Kanisa Linakwenda Samaria,{ Mdo 8}.Wasamaria walikuwa ni chotara ambao asili

yao ilikuwa ni Ashuru ambpo walihamishiwa katika eneo la Kaskazini mwa Israeli. Pale

waisraeli walipochukuliwa kwenda utumwani Ashuru {Irani}. Mchanganyiko wa wageni

hao na mabaki ya waisraeli ambao hawakwenda utumwani Ashuru yaliunda jamii ya

Wasamaria kwa njia ya kuzaliana, kutokana na kuoana kati ya wageni na mabaki ya

waisraeli. Watoto waliozaliwa walikuwa chotara na ndio kizazi cha Wasamaria .

Wasamaria Walikuwa na hekalu lao katika mlima Gelzimu na walivitumia vitabu vitano

vya Musa pekee kama Biblia yao. Kwahiyo Wayahudi hawakuchangamana nao.

Roho Mtakatifu alimwambia Shemasi Filipo kwenda kuhubiri Neno Samaria. Mungu

alimtumia kufanya ishara na maajabu kwa jina la Yesu huko Samaria. Uamsho mkuu

7

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!