You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Kujihusisha na shughuli za kijamii, Mitume walianza kujihusisha na mambo ya kijamii
{kiutawala} kwani shughuli zote za kanisa za kila siku zilifanywa na wao.Tunaona Petro
aliyekuwa mhubiri anaanza kujihusiha na mambo ya kiutwala.
Mitume walifika mahali wakagundua tatizo hilo na wakachagua wahudumu saba
waliotakiwa kushughulikia mambo ya kiutawala ili wao wadumu katika kulihubiri Neno
na Kuomba.
Bwana alilionya kanisa lake “Tubu na ukafanye mambo ya kwanza la sivyo nitakiondoa
kinara chako mahli pake. Mungu alitimiza Neno lake kama Tutakavyo ona hapo baadae.
H. KUENEA KWA KANISA LA KWANZA. Kupanuka kwa kanisa tangu mahubiri ya
Stefano {mwaka 35. AD} hadi mkutano wa Yerusalemu {mwka 48. AD}.Mambo ya
msingi katika kipindi hiki yalikuwa ni upandaji wa makanisa. Kipindi hiki kifupi kilikuwa
na umuhimu mkubwa kwa kanisa. Japokuwa kanisa mwanzo lilikuwa Yerusalemu tu sasa
lilipandwa katika maeneo mengine kama vile Siria na Asia ndogo na kuelekea Ulaya.
Waamini wa kwanza walikuwa ni Wayahudi lakini baada ya kipindi hiki kifupi waamini
wengi walikuwa ni wamataifa .
Mwanzoni Injili ilihubiriwa kwa kiebrani na kwa kiaramu lakini baadae iligundulika
kwamba ulimwengu mzima ungefikiwa na Injili kupitia lugha ya Kigiriki kwa sababu
kigiriki wakati huo kilikuwa ni lugha ya mawasiliano ya kimataifa kama ilivyo
kiingereza kwa dunia ya sasa.
I KUTESWA KWA KANISA NA VIONGOZI WA KIYAHUDI.
Yesu aliwaagiza mitume kwenda kuhubiri Injili duniani kote lakini wao walipenda kukaa
Yerusalemu .Mungu alikasirika na akaamua kuruhusu mateso katika kanisa .{Mdo 9}
1. Mahubiri ya Stefano {.Mdo 6:1-4, 7} Kwa sababu ya imani yake kwa Mungu Stefano
alihukumiwa kuuawa na kuwa mfia dini wa kwanza katika imani ya kikristo. Kijana
mmoja mfarisayo wa Tarso Sauli alishuhudia mauaji ya Stefano na Baadae kijana huyo
akawa kiongozi mkuu wa mauaji ya wakristo katika taifa la wayahudi.
Kutokana na tukio hili waamini wote walikimbia Yerusaelimu isipokuwa mitume {Mdo
8:1-4}.Waamini hao walisambaa maeneo mbalimbali na kila mahali walipokwenda
walilihubiri Neno . Kwa njia hii kwa muda mfupi Injili ilipata kuenea kwa haraka katika
maeneo yote yaliyoizunguka Yerusalemu.
2. Kanisa Linakwenda Samaria,{ Mdo 8}.Wasamaria walikuwa ni chotara ambao asili
yao ilikuwa ni Ashuru ambpo walihamishiwa katika eneo la Kaskazini mwa Israeli. Pale
waisraeli walipochukuliwa kwenda utumwani Ashuru {Irani}. Mchanganyiko wa wageni
hao na mabaki ya waisraeli ambao hawakwenda utumwani Ashuru yaliunda jamii ya
Wasamaria kwa njia ya kuzaliana, kutokana na kuoana kati ya wageni na mabaki ya
waisraeli. Watoto waliozaliwa walikuwa chotara na ndio kizazi cha Wasamaria .
Wasamaria Walikuwa na hekalu lao katika mlima Gelzimu na walivitumia vitabu vitano
vya Musa pekee kama Biblia yao. Kwahiyo Wayahudi hawakuchangamana nao.
Roho Mtakatifu alimwambia Shemasi Filipo kwenda kuhubiri Neno Samaria. Mungu
alimtumia kufanya ishara na maajabu kwa jina la Yesu huko Samaria. Uamsho mkuu
7