21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

b.Masadukayo, Hawa jina lao lilitoka kwa Sadoki kuhani mkuu wa wakati wa Daudi toka

uzao wa Haruni Kuhani Mkuu. Hivyo walikuwa ni uzao wa kikuhani.Wao hawakuamini

ufufuo wa wafu wala uwepo wa malaika.

2. Dola ya Kirumi,. Mwaka 63KK. mfalme wa Rumi Julius Kaizari aliivamia na

kuishinda Palestina na akaanzisha utawala wa kirumi katika nchi ya palestina . Huu

ulikuwa ni ufalme wanne uliokuwa umeishinda na kuitawala Israeli kulingana na unabii wa

Danieli . Israeli ilikuwa chini ya utawala wa dola ya Rumi Yesu Kristo alipozaliwa na

katika kipindi cha maisha yake hapa duniani.

a. Dini ya kipagani(Heathenism), hii ilikuwa ni dini ambayo mianzo yake ni mtawala

Nimrodi katika mnara wa Babeli na dini hii baadae ilisambaa katika maeneo mbalimbali

yaliyoizunguka Babeli mpaka Misri, Ugiriki na Rumi.Waliabudu miungu ya kigeni {Yer

2:25}. Ilikuwa ni miungu ya zamani sana ya Kibabeli, ilikuwa na majina mbalimbali katika

nchi mbalimbali, mfano A=`570rtemi, Diana, Osiris, Jupita Appolo Zeus. N.K

b. Ibada ya mfalme. Hii ilikuwani mojawapo ya tamaduni ya dola ya Rumi. Baadhi ya

wafalme wakirumi walijitangaza kwamba wao ni miungu na wakadai kwamba wananchi

wao wanatakiwa kuwaabudu.hivyo Ibada ya kuwaadudu wafalme {makaisari} ilianzishwa.

Kukataa kumwabudu Kaisari kungepelekea mtu kuhukumiwa adhabu ya kifo. Ibada

ya kumwabudi mfalme ilikuwa imerithiwa toka kipindi cha babeli. Kaisari Domitiani ni

mojawapo wa Makaisari waliosimamisha sanamu zao na kudai ibada zifanywe juu yao.

c. Wanafasalsafa wa Kigiriki. Kulizuka falsafa za kigiriki ambazo zilikuwa zinasisitiza

kwamba lengo la maisha ni furaha na anasa. Walisisitiza kwamba maarifa yanaweza

kupatikana kwa njia ya kufikiri {Logic}.Waliegemea katika vitu vinavyooneka tu

(materialism). Falsafa hizi ndizo ambazo zilikuwa zimeshikiliwa na watu mbalimbali

katika kipindi hiki.

Falsafa hizi zilisisitiza kwamba maisha ni kula na kunywa kwa sababu baada ya kufa

mwanadamu alikuwa anaoza na kwamba hakukuwa na maisha baada ya kufa.

C. KUANZA KWA KANISA.

Kanisa lilianza Yerusalemu siku aliposhuka Roho mtakatifu katika chumba cha juu katika

hekalu la Yerusalem. Baada ya Yesu Kristo kupaa Mbinguni wanafunzi walirudi toka

mlima wa Mizeituni mpaka hekaluni na kukaa katika chumba cha juu. Waliomba na

kusubiri kuvikwa nguvu. Baada ya siku kumi Roho Mtakatifu alishuka na wote

waliokuwemo kwenye chumba cha juu walijazwa Roho Mtakatifu na kuanza

kumwazimisha Mungu kwa Lugha zingine. Kazi ya uinjilisti ilianza papo hapo, mtume

Petro alihubiri na watu 3000 wakaokolewa na kubatizwa. Hii inahesabiwa kwamba ndio

mwanzo wa kanisa la agano jipya.

Matokeo ya kujazwa Roho Mtakaifu

5

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!