You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
b.Masadukayo, Hawa jina lao lilitoka kwa Sadoki kuhani mkuu wa wakati wa Daudi toka
uzao wa Haruni Kuhani Mkuu. Hivyo walikuwa ni uzao wa kikuhani.Wao hawakuamini
ufufuo wa wafu wala uwepo wa malaika.
2. Dola ya Kirumi,. Mwaka 63KK. mfalme wa Rumi Julius Kaizari aliivamia na
kuishinda Palestina na akaanzisha utawala wa kirumi katika nchi ya palestina . Huu
ulikuwa ni ufalme wanne uliokuwa umeishinda na kuitawala Israeli kulingana na unabii wa
Danieli . Israeli ilikuwa chini ya utawala wa dola ya Rumi Yesu Kristo alipozaliwa na
katika kipindi cha maisha yake hapa duniani.
a. Dini ya kipagani(Heathenism), hii ilikuwa ni dini ambayo mianzo yake ni mtawala
Nimrodi katika mnara wa Babeli na dini hii baadae ilisambaa katika maeneo mbalimbali
yaliyoizunguka Babeli mpaka Misri, Ugiriki na Rumi.Waliabudu miungu ya kigeni {Yer
2:25}. Ilikuwa ni miungu ya zamani sana ya Kibabeli, ilikuwa na majina mbalimbali katika
nchi mbalimbali, mfano A=`570rtemi, Diana, Osiris, Jupita Appolo Zeus. N.K
b. Ibada ya mfalme. Hii ilikuwani mojawapo ya tamaduni ya dola ya Rumi. Baadhi ya
wafalme wakirumi walijitangaza kwamba wao ni miungu na wakadai kwamba wananchi
wao wanatakiwa kuwaabudu.hivyo Ibada ya kuwaadudu wafalme {makaisari} ilianzishwa.
Kukataa kumwabudu Kaisari kungepelekea mtu kuhukumiwa adhabu ya kifo. Ibada
ya kumwabudi mfalme ilikuwa imerithiwa toka kipindi cha babeli. Kaisari Domitiani ni
mojawapo wa Makaisari waliosimamisha sanamu zao na kudai ibada zifanywe juu yao.
c. Wanafasalsafa wa Kigiriki. Kulizuka falsafa za kigiriki ambazo zilikuwa zinasisitiza
kwamba lengo la maisha ni furaha na anasa. Walisisitiza kwamba maarifa yanaweza
kupatikana kwa njia ya kufikiri {Logic}.Waliegemea katika vitu vinavyooneka tu
(materialism). Falsafa hizi ndizo ambazo zilikuwa zimeshikiliwa na watu mbalimbali
katika kipindi hiki.
Falsafa hizi zilisisitiza kwamba maisha ni kula na kunywa kwa sababu baada ya kufa
mwanadamu alikuwa anaoza na kwamba hakukuwa na maisha baada ya kufa.
C. KUANZA KWA KANISA.
Kanisa lilianza Yerusalemu siku aliposhuka Roho mtakatifu katika chumba cha juu katika
hekalu la Yerusalem. Baada ya Yesu Kristo kupaa Mbinguni wanafunzi walirudi toka
mlima wa Mizeituni mpaka hekaluni na kukaa katika chumba cha juu. Waliomba na
kusubiri kuvikwa nguvu. Baada ya siku kumi Roho Mtakatifu alishuka na wote
waliokuwemo kwenye chumba cha juu walijazwa Roho Mtakatifu na kuanza
kumwazimisha Mungu kwa Lugha zingine. Kazi ya uinjilisti ilianza papo hapo, mtume
Petro alihubiri na watu 3000 wakaokolewa na kubatizwa. Hii inahesabiwa kwamba ndio
mwanzo wa kanisa la agano jipya.
Matokeo ya kujazwa Roho Mtakaifu
5