Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
MADA YA PILI
KIPINDI CHA EFESO.
{Kanisa la Mtume}
A. UTANGULIZI.
Kanisa la Efeso (ufunuo wa Yohana 2:1-7)
MUDA; Tangu kupaa kwa Yesu Kristo kama mwaka 30.AD.Mpaka kifo cha mtume
Yohana kama mwaka wa 100. B.K.
Efeso ulikuwa mji muhimu katika pwani ya Asia ndogo na ulipewa jina la heshima la
Nuru ya Asia. Waefeso waliabudu miungu ya kiasia ambayo ni Artemi, ambae pia aliitwa
Diana. Hekalu la artemi lilihesabiwa kuwa mojawapo ya maajabu ya dunia ya wakati ule.
Mahali pengine walipoabudia paliitwa Augusteum. Mahali hapo walitumia kumwabudu
mfalme . kiwango cha kiburudani za kidunia zilikuwa nyingi na inakadiliwa kuwa ukumbi
wa Efeso ulikuwa na uwezo wa kuchukua watu 25,000.
Kipindi hiki kinaitwa kipindi cha mitume kwa sababu karibia mitume wote12 wa
mwanakondoo {Yesu} waliishi katika kipndi hiki. Kipndi hiki kiliishia na kifo cha Mtume
Yohana ambae alikufa kifo cha kawaida akiwa mzee mwenye umri wa kama miaka 100.
Kuna walimu wa theologia wanaofundisha kwamba mitume na manabii waliishia katika
kipindi hiki. Jambo ambalo si kweli kabisa kwani huduma hizi zimekuwepo katika vipindi
vyote vya kanisa japokuwa katika vipindi fulani zilififia, lakini zimekuwepo katika zama
zote za kanisa.
B.ULIMWENGU WA WAKATI WA MITUME
Kanisa lilikutana na upinzani mara tu lilipoanza.Upinzani huo ulitokana na makundi
mbalimbali
1. Dini ya kiyahudi. Wayahudi walikuwa ni adui namba moja wa kanisa .walilivamia
kanisa wakati lingali changa kwa kushirikiana na mfalme wa kirumi walimsulibisha Yesu
Kristo. Ndani y dini ya kiyahudi kulikuwa na makundi/madhehebu mbalimbali ambayo
yalishiriki katika kulitesa kanisa. Baadhi ya makundi hayo ni:-
a).Mafarisayo. Hawa walianza katika kipindi cha Ezra na Nehemia waliporudi toka
uhamishoni Babeli wakati ukuhani mpya ulipoanzishwa. Mafarisayo Waliamini juu ya
‣ Ufufuo wa wafu
‣ adhabu kwa wenye dhambi
‣ Kutokufa kwa nafsi
‣ Uwepo wa malaika na huduma zao
‣ Kila kitu kinamtegemea Mungu.
‣ Mtazamo wao wa kisiasa ulikuwa ni wa kiyahudi na waliogopa kushirikiana na watu
wasiokuwa mafarisayo. Mfano Wasamaria, na Wamataifa na kwa namna zote
walizishika sheria za Musa na walifanya tohara.
4