Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
wadhifa wake, alifungwa jela kwenye nyumba ya kifalme ya Loch Leven lakini alifanikiwa
kutoroka Mei 2, 1568.
Miaka ya mwisho ya John Knox
Scotland ilijikuta ikiwa kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya wale waliomuunga
mkono malkia aliyeondolewa na waprotestanti.1571, msimamizi wa nyumba ya kifalme ya
Edinburgh, nae alimuunga mkono malkia, alifukuza waprotestanti wote kwenye jiji hilo.
Knox alistaafu kwenye nyumba ya kifalme ya mtakatifu Andrew lakini akarudi tena
mwaka 1572, tayari akiwa dhaifu kimwili kutokana na umri wake lakini, kama siku zote,
akiwa imara katika misingi yake ya kusambaza neno kwenye kanisa la mtakatifu Gilles,
akimtambulisha mrithi wake, mchungaji Lawson Aberdeen. Knox alirudi nyumbani kwake
kwa mara ya mwisho na kufariki Novemba 24, 1572, mke wake akimfariji na akiwa
amezungukwa na waprotestanti wenye vyeo vya heshima. Ombi lake la mwisho
lilikuwa kusomewa neno la Mungu. Mwili wake ulizikwa ndani ya kanisa la mtakatifu
Gilles
Mwanamatengenezo huyu hakuogopa sura ya mwanadamu. Moto wa Injili ya kweli
uliwaka ndani yake daima na alikuwa tayari kuitetea kweli ya Neno kwa gharama yoyote
ile.
Knox aliishi kwa imani. Alibaki kuwa mkweli kwa kazi yake na kwa ukweli wa Mungu,
akipigania vita ya Bwana hadi Scotland ilipata wa uhuru. Kanisa la Presbyterian lina
mtambua Knox kuwa mmoja wa waanzilishi wake.
Hitimisho
" Tunapaswa kuwa na shauku kama aliyokuwa nayo John Knox alipoomba mbele ya
Mungu kwa ajili ya Scotland. Alilia, "Nipe Scotland, Bwana, au nitakufa. Hakika shujaa
huyu alipewa Scotland kama alivyoomba na akawa tayari kufa kupona kuhakikisha nuru ya
matengenezo inang’aa Scotland.
Kwa hakika Wanamatengenezo walisimama kidete kuitetea kweli ya Mungu. Bado leo
Mungu anahitaji na anainua wanamatengezo katika kanisa la sasa. Kazi ya matengenezo
ya kanisa haijamalizika. Mungu analiandaa kanisa lake kwaajili ya unyakuo . Kazi ya
matengenezo ya kanisa itakwisha pale kanisa litakapokuwa limenyakuliwa kwenda
mbinguni.
Kanisa la leo limekengeuka. Ulimwengu umeingia kanisani na karibu kila mtu katika
dunia ya sasa anajiita ameokoka. Wanahitajika wanamatengenezo wa kizazi hiki
watakaosimama na kupaza sauti zao ili kulirudisha kanisa katika nafasi yake.
Kama mtumishi wa Mungu unapaswa kusimama katika zamu yako. Usimezwe na dunia
na anasa zake. Hubiri kweli ya neno la Mungu. Usikubali kuhalalisha baadhi ya mambo ili
kujipatia kundi kubwa au kujijengea umaarufu. Simama na Bwana katika utumishi
aliokwitia bila kuyumbishwa na mtu yeyote.
57