21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

wadhifa wake, alifungwa jela kwenye nyumba ya kifalme ya Loch Leven lakini alifanikiwa

kutoroka Mei 2, 1568.

Miaka ya mwisho ya John Knox

Scotland ilijikuta ikiwa kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya wale waliomuunga

mkono malkia aliyeondolewa na waprotestanti.1571, msimamizi wa nyumba ya kifalme ya

Edinburgh, nae alimuunga mkono malkia, alifukuza waprotestanti wote kwenye jiji hilo.

Knox alistaafu kwenye nyumba ya kifalme ya mtakatifu Andrew lakini akarudi tena

mwaka 1572, tayari akiwa dhaifu kimwili kutokana na umri wake lakini, kama siku zote,

akiwa imara katika misingi yake ya kusambaza neno kwenye kanisa la mtakatifu Gilles,

akimtambulisha mrithi wake, mchungaji Lawson Aberdeen. Knox alirudi nyumbani kwake

kwa mara ya mwisho na kufariki Novemba 24, 1572, mke wake akimfariji na akiwa

amezungukwa na waprotestanti wenye vyeo vya heshima. Ombi lake la mwisho

lilikuwa kusomewa neno la Mungu. Mwili wake ulizikwa ndani ya kanisa la mtakatifu

Gilles

Mwanamatengenezo huyu hakuogopa sura ya mwanadamu. Moto wa Injili ya kweli

uliwaka ndani yake daima na alikuwa tayari kuitetea kweli ya Neno kwa gharama yoyote

ile.

Knox aliishi kwa imani. Alibaki kuwa mkweli kwa kazi yake na kwa ukweli wa Mungu,

akipigania vita ya Bwana hadi Scotland ilipata wa uhuru. Kanisa la Presbyterian lina

mtambua Knox kuwa mmoja wa waanzilishi wake.

Hitimisho

" Tunapaswa kuwa na shauku kama aliyokuwa nayo John Knox alipoomba mbele ya

Mungu kwa ajili ya Scotland. Alilia, "Nipe Scotland, Bwana, au nitakufa. Hakika shujaa

huyu alipewa Scotland kama alivyoomba na akawa tayari kufa kupona kuhakikisha nuru ya

matengenezo inang’aa Scotland.

Kwa hakika Wanamatengenezo walisimama kidete kuitetea kweli ya Mungu. Bado leo

Mungu anahitaji na anainua wanamatengezo katika kanisa la sasa. Kazi ya matengenezo

ya kanisa haijamalizika. Mungu analiandaa kanisa lake kwaajili ya unyakuo . Kazi ya

matengenezo ya kanisa itakwisha pale kanisa litakapokuwa limenyakuliwa kwenda

mbinguni.

Kanisa la leo limekengeuka. Ulimwengu umeingia kanisani na karibu kila mtu katika

dunia ya sasa anajiita ameokoka. Wanahitajika wanamatengenezo wa kizazi hiki

watakaosimama na kupaza sauti zao ili kulirudisha kanisa katika nafasi yake.

Kama mtumishi wa Mungu unapaswa kusimama katika zamu yako. Usimezwe na dunia

na anasa zake. Hubiri kweli ya neno la Mungu. Usikubali kuhalalisha baadhi ya mambo ili

kujipatia kundi kubwa au kujijengea umaarufu. Simama na Bwana katika utumishi

aliokwitia bila kuyumbishwa na mtu yeyote.

57

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!