21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

‣ Misa kwa lugha ya kilatini kuliondolewa

‣ Siku kuu za kikatoliki zilifutwa

‣ Maombi ya wafu yalipigwa marufuku

‣ Imani ya kwamba wafu wapo toharani ilikataliwa

‣ Misalaba ilikataliwa

‣ Sherehe za misa zilikataliwa

‣ Ilidhibitishwa kwamba mkate kuwa mwili wa Yesu ni mfano tu na sio kwamba mkate ni

mwili wake halisi.

Pamoja na hayo, bunge liliwaagiza Knox na wachungaji wengine kuandaa kuundwa upya

kwa kanisa la matengenezo nchini Scotland na taratibu mpya za ibada zilihamisha

msisitizo kutoka kweye kutazama makuhani na kuuweka kwenye kushirikiana kwa

waumini wote, na masomo ya Biblia, mahubiri, maombi, kusoma Zaburi na kuimba kwa

kusanyiko lote.

Magumu mapya

Disemba 1560, Knox alipokea pigo kubwa pale mke wake Margery alipofariki, akiachwa

na watoto wawili wadogo wakuwatunza, Muda usio mrefu sana baada ya hapo, Agosti 19,

1561, sauti ya mabomu ilisikika kwenye bandari ya Leith, ikitambulisha ujio wa Malkia

mdogo Maria, mtoto wa Maria Gise, aliyekuwa amekimbilia Ufaransa. Ilitangazwa

kwamba hakutakuwa na mabadiriko yoyote juu ya maswala ya dini na hakuna

kinachopaswa kusumbua wafanyakazi wake wakikatoliki.

Baadhi ya waheshimiwa, waliopendelea siasa, waliamua kumuunga mkono malkia mpya,

na si John Knox. Knox alipaza suti, akihubiri kupinga msimamo wa malkia kuhusu

mambo ya dini. Malkia Mary alimuita Knox wiki mbili baada ya kufika Scotland,

akimtuhumu kwa uasi wake na kuandika kupinga mamlaka yake.

"Baada yakuletwa uso kwa uso na malkia wa Scotland, mahali ambapo udhahiri wa

viongozi wakiprotestanti ulikosa nguvu, John knox alisimama bila kutikisika kushuhudia

ukweli. Hakukubali kununuliwa na maneno matamu, hakuwa na hofu kwa kutishwa.

Malkia alimshtaki kwa mafundisho potofu. Alikuwa amefundisha watu kupokea dini

iliokataliwa na taifa, alisema, hiyo ni kuvunja amri ya Mungu kwamba watu watii walio

juu yao.

Knox aliitwa Mara kadhaa na malkia kujibu mashtaka, lakini mwanamatengenezo huyu

alijibu kila wakati kwa msimamo na kuweza kubaki huru kutokana na ushawishi wake

mkubwa na kuungwa mkono na waheshimiwa wakiprotestanti. Malkia alimkumbusha

kwamba anapaswa kuishi kulingana na sheria za Scotland na kwamba misa ilikatazwa.

Mwezi Machi 26, 1564, Knox, akiwa hana mke, akiwa na miaka 50, aliamua kuoa tena, na

alimuoa Margaret wa Stewart, ambae alizaa nae watoto wakike watatu ambao ni Martha,

Margaret, na Elizabeth.

Knox hakunyamaza, Mwaka 1565, alihubiri, kama siku zote, kwa ujasiri, akipinga ndoa ya

malkia na Henry Stuart. Ndoa hiyo haikudumu, Stuart aliuwawa. Malkia Maria aliolewa

tena, . Kutokana na hayo, mamlaka ya Scotland ilimlazimisha Malkia Maria ajiuzuru

56

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!