21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Kufunguka kwa matengenezo ya kiprotestanti Scotland

Pale malkia aliependelea uprotestanti, Elizabeth Tudor, alipoingia madarakani Uingereza,

wakambizi waliokuwa Ujerimani waliamua kurudi nchini kwao. Knox aliamua kurudi

Scotland. Kabla hajaondoka, utawala wa Geneva ulimtaja kwa heshima kwa mchango

wake kwa uprotestanti. Nchini Scotland, hali ilikuwa tete kati ya malkia Maria wa Gise na

kuandamana kwa waprotestanti.

Baada ya siku chache kufika Scotland, Knox alihubiri mahubiri ya kuvutia katika mji wa

Perth kupinga kuabudu sanamu kwa wa katoliki. Mara baada ya kumaliza tu, maandamano

yaliibuka dhidi ya kanisa la Katoliki, na kusababisha kuharibiwa kwa sanamu,

madhabahu, na hekalu na mji wa Perth uliozungushwa na ukuta kuchimbwa chimbwa.

Maria wa Gise alituma jeshi kuzingira huo mji. Mazungumzo yalifikia makubaliano na

jeshi la waprotestanti ili kusitokee vita na jeshi la Ufaransa waliounganika na Malkia Maria

wa Gise. Lakini baada ya kuingia kwenye huo mji, malkia aliujaza na jeshi la wa Scot kwa

kudhaminiwa na Ufaransa. Jambo hili lilichukuliwa kama usaliti kwa upande wa baadhi ya

waheshimiwa waliounga mkono makubaliano kati ya waprotestanti na wanaomuunga

mkono Mary wa Gise, hivo waliamua kubadili msimamo wao na kuunga mkono

matengenezo ya uprotestanti

Kutokana na matatizo ya Perth, Knox alienda katika kanisa la mtakatifu Andrews, huko

alihubiri ujumbe wa moto uliosababisha athari kama kule Perth - maandamano na

kuvunjwa kwa mali ya kanisa. Jeshi la waprotestanti waliweza kuvamia miji kadhaa

Scotland, wakiungwa mkono na mahubiri ya Knox yenye nguvu. Waheshimiwa wa

kiprotestant, wakisaidiwa na jeshi, pia walivamia Edinburgh, mji mkuu wa Scotland.

Mwezi Julai 25, 1559, baada ya viongozi wa kiprotestant, waitwao mabwana wa

kusanyiko, kujitoa katika mji Edinburgh, na malkia waScotland, Maria wa Gise, kuahidi

uhuru wa dhamira.

Ila malkia alikuwa na mpango mwingine. Aliomba msaada kutoka jeshi la ufaransa.

Walipotua Leith, waprotestanti waliuvamia na kuuchukua tena mji Edinburgh na kumvua

cheo Maria wa Gise kwenye kuongoza Scotland. Baadhi ya waheshimiwa waliweza

kushawishi Uingereza kutuma wanajeshi kusaidia waprotestanti.

Kifo cha malkia kiongozi Maria wa Gise mwezi Juni 10, 1560, kilitengeneza njia ya

muafaka wenye amani. Julai 6 mwaka huo, makubaliano ya Edinburgh yalitiwa sahihi,

ambapo jeshi la majini la Ufaransa na jeshi la Uingereza walipaswa kuondoka Scotland,

hivyo kuimarisha mwendelezo wa kiprotestant. Julai 19, Knox aliongoza ibada ya shukrani

kwa ngazi ya taifa kwenye kanisa la mtakatifu Gilles mjini Edinburgh. Kuanzia Agosti, 1,

1560, bunge lilikutana kutoa mwongozo mpya juu ya dini inayotambulika kitaifa. Knox,

pamoja na wachungaji wengine, waliandaa mwongozo mpya wa imani ambao bunge

lilipitisha na rasmi kuanzisha matengenezo ya kiprotestant nchini humo. Baadhi ya mambo

yaliyokataliwa na waprotestanti ni:-

‣ Mamlaka ya papa nchini Scotland yaliondolewa

‣ Mafundisho na matendo yote yalio kinyume na uprotestanti yalikataliwa

‣ Kuabudu Maria kulikataliwa

55

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!