21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

akakubali. Kule Frankfurt tatizo lingine liliibuka: Taratibu za ibada. Mawazo

yaligawanyika na ujio wa wakimbizi wapya. Wengine waliunga utaratibu mpya uliokuwa

ukipendekezwa na Knox na wengine kuzitingatia kwa umakini sana kama ilivyo kwenye

kitabu cha taratibu za ibada za kanisa la katoliki. Kupitia ushauri wa Calvin, Knox

alifanikiwa kufikia makubaliano; ila na ujio wa wakimbizi wengi zaidi, msukumo ulizidi

kiasi ya kwamba waliokuwa wakipinga walishitaki kwa utawala wa Frankfurt, na

akaombwa aondoke. Hata hivo Knox alirudi Geneva.

Jaribio Jipya Scotland

Ndani ya Scotland, pamoja na nguvu ya kirumi, baadhi ya waheshimiwa waliamua

kusimamisha neno la Mungu kama msingi wa makanisa yao, walipinga mafundisho potofu

yaliyokuwa yakitolewa na kanisa. Baadhi yao walimwalika Knox kurudi Scotland ili

kusimamia maengenezo ya Kanisa. Kwa miezi tisa Knox alijitoa sana kuhubiri

mafundisho ya matengenezo na taratibu mpya za ibada katika makanisa mbali mbali ya

Scotland.

Kurudi kwake Scotland na umarufu wake kulishangaza makuhani wa Katoliki, waliomuita

ajitokeze mjini Ediburg mwezi Mei 15, 1556, wakimchukulia kuwa tishio kwa mamlaka ya

kanisa. Alisindikizwa kwenye hicho kikao na waheshimiwa wengi wenye ushawishi, na

maaskofu waliomshitaki waliamua kufuta mashtaka. Knox alikuwa huru kuhubiri wazi

misingi ya uprotestanti.

Kazi ya tatu Geneva

Gafla Knox aliamua kurudi Uswisi, na alifika Uswisi mwezi Septemba 13, 1556, pamoja

na mke wake, Margery Bowes, na mama mkwe wake, Elizabeth Bowes. Hii ilikuwa miaka

ya Knox ya furaha zaidi, licha ya kazi yake ngumu kama mchunganji katika kanisa la

kiingereza la Geneva, ambalo lilikusanyika kwenye Eglise de Notre Dame la Neuve,

ambalo kwa sasa linajulikana kama Ukumbi wa Calvin. Akiwa Geneva, watoto wake

wawili wakiume walizaliwa, Nathaniel na Eleazar.

Knox alishauri Geneva kwa marafiki zake wote Uingereza kuwa sehemu bora zaidi ya

kimbilio. Katika moja wa barua zake aliandika: “Sina hofu wala aibu kusema, (Geneva) ni

shule ya kristo iliyokamilika zaidi kutokea duniani tangu siku za mitume. Katika baadhi ya

sehemu na shuhudia Kristo kuhubiriwa kiukweli; ila tabia na dini yenye matengenezo ya

dhati sijawahi kuona katika sehemu nyingine.

Mwaka 1558 Knox aliandika akiwa Geneva mmoja wa vipeperushi vyake maarufu

kiitwacho “Sauti ya kwanza ya tarumbeta dhidi ya utawala wa kinyama wa wanawake.”

Knox alimaanisha Maria I wa Uingereza na Maria wa Gise wa Scotland kwa kutesa wa

protestanti na kusema wanapaswa kuondolewa katika utawala. Jarida hilo lilichapishwa

kisiri bila ushauri wa Calvin. Lilipigwa marufuku nchini Uingereza na hata Geneva na

Calvin, alilikataa kabisa. Knox mwenyewe alikubali kwamba jarida hili lilikamilisha

kufarakana kwake na marafiki zake wa Uingereza. Elizabeth Tudour, aliyekuja kuwa

malkia miezi michache baadae, alikwazika sana na jarida hilo na hakumsamehe Knox.

54

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!