You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
akakubali. Kule Frankfurt tatizo lingine liliibuka: Taratibu za ibada. Mawazo
yaligawanyika na ujio wa wakimbizi wapya. Wengine waliunga utaratibu mpya uliokuwa
ukipendekezwa na Knox na wengine kuzitingatia kwa umakini sana kama ilivyo kwenye
kitabu cha taratibu za ibada za kanisa la katoliki. Kupitia ushauri wa Calvin, Knox
alifanikiwa kufikia makubaliano; ila na ujio wa wakimbizi wengi zaidi, msukumo ulizidi
kiasi ya kwamba waliokuwa wakipinga walishitaki kwa utawala wa Frankfurt, na
akaombwa aondoke. Hata hivo Knox alirudi Geneva.
Jaribio Jipya Scotland
Ndani ya Scotland, pamoja na nguvu ya kirumi, baadhi ya waheshimiwa waliamua
kusimamisha neno la Mungu kama msingi wa makanisa yao, walipinga mafundisho potofu
yaliyokuwa yakitolewa na kanisa. Baadhi yao walimwalika Knox kurudi Scotland ili
kusimamia maengenezo ya Kanisa. Kwa miezi tisa Knox alijitoa sana kuhubiri
mafundisho ya matengenezo na taratibu mpya za ibada katika makanisa mbali mbali ya
Scotland.
Kurudi kwake Scotland na umarufu wake kulishangaza makuhani wa Katoliki, waliomuita
ajitokeze mjini Ediburg mwezi Mei 15, 1556, wakimchukulia kuwa tishio kwa mamlaka ya
kanisa. Alisindikizwa kwenye hicho kikao na waheshimiwa wengi wenye ushawishi, na
maaskofu waliomshitaki waliamua kufuta mashtaka. Knox alikuwa huru kuhubiri wazi
misingi ya uprotestanti.
Kazi ya tatu Geneva
Gafla Knox aliamua kurudi Uswisi, na alifika Uswisi mwezi Septemba 13, 1556, pamoja
na mke wake, Margery Bowes, na mama mkwe wake, Elizabeth Bowes. Hii ilikuwa miaka
ya Knox ya furaha zaidi, licha ya kazi yake ngumu kama mchunganji katika kanisa la
kiingereza la Geneva, ambalo lilikusanyika kwenye Eglise de Notre Dame la Neuve,
ambalo kwa sasa linajulikana kama Ukumbi wa Calvin. Akiwa Geneva, watoto wake
wawili wakiume walizaliwa, Nathaniel na Eleazar.
Knox alishauri Geneva kwa marafiki zake wote Uingereza kuwa sehemu bora zaidi ya
kimbilio. Katika moja wa barua zake aliandika: “Sina hofu wala aibu kusema, (Geneva) ni
shule ya kristo iliyokamilika zaidi kutokea duniani tangu siku za mitume. Katika baadhi ya
sehemu na shuhudia Kristo kuhubiriwa kiukweli; ila tabia na dini yenye matengenezo ya
dhati sijawahi kuona katika sehemu nyingine.
Mwaka 1558 Knox aliandika akiwa Geneva mmoja wa vipeperushi vyake maarufu
kiitwacho “Sauti ya kwanza ya tarumbeta dhidi ya utawala wa kinyama wa wanawake.”
Knox alimaanisha Maria I wa Uingereza na Maria wa Gise wa Scotland kwa kutesa wa
protestanti na kusema wanapaswa kuondolewa katika utawala. Jarida hilo lilichapishwa
kisiri bila ushauri wa Calvin. Lilipigwa marufuku nchini Uingereza na hata Geneva na
Calvin, alilikataa kabisa. Knox mwenyewe alikubali kwamba jarida hili lilikamilisha
kufarakana kwake na marafiki zake wa Uingereza. Elizabeth Tudour, aliyekuja kuwa
malkia miezi michache baadae, alikwazika sana na jarida hilo na hakumsamehe Knox.
54