21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Cemetri ambalo halikuwekwa alama yoyote. Hadi sasa kaburi la John Calvin halijulikani

lilipo.

4. JOHN KNOX

John Knox alizaliwa katika miaka ya 1513 katika Haddington, mji mdogo kaskazini mwa

Edinburg, Scotland. Maisha yake ya awali yalimwezesha kukutana na watu wengi, na

elimu yake ya juu ilimwezesha kuwafikia watu wa hali ya juu katika jamii. Alipoteza

wazazi wake akiwa bado mtoto. Knox alijifunza kilatini shuleni Haddington. Mwaka 1529,

alianza masomo ya Theolojia katika chuo cha mtakatifu Andrews. Aliwekewa mikono ya

ukuhani mwaka 1536 ila hakuajiriwa katika nafasi hiyo kutokana na Scotland kuwa na

makuhani wengi.

Mwaka 1540, utawala wa Scotland ulianza kuwatesa wahubiri wa Neno la Mungu. George

Wishart hakuogopa muda wa majaribu na akasafiri kutoka kijiji kimoja hadi kijiji kingine

kuhubiri ukweli wa Biblia. Knox, kwa kushawishika na ujumbe wa Wishart, aliamua

kumsindikiza kama mlinzi wake, akiwa na mapanga mawili kumkinga mhubiri huyu dhidi

ya vitisho vya watesi. Kwa wiki tano, alimsindikiza Wishart katika kuhubiri kwake mpaka

mamlaka yaliamua kunyamazisha sauti ya mheshimiwa huyu kwa kumfunga gerezani.

John Knox Aliamua kujiunga nae na kumuunga mkono, lakini Wishart alimsihi arudi

nyumbani, akisema: “Hapana, rudi kwa watoto wako, na Mungu akubariki. Mmoja

anatosha kuwa kafara. Knox alirudi.

Henry Balnaves, mmoja ya waheshimiwa, alifurahishwa na kipaji chaa ufundishaji wa

wanamatengenezo na kuungana na mhubiri John Rough kwa kumwalika Knox kuwa mkuu

wa kanisa na mchungaji wa kanisa la nyumba ya mtakatifu Andrews. Knox alikataa

mwaliko huo, nakusema hawakuwa na mamlaka ya kutoa wito huo na kurudi chumbani

mwake

. Wiki chache baade, alihudhuria ibada ambayo mhudumu alitetea kanisa la kikatoliki

kuwa mke wa Kristo. Knox alishindwa kunyamaza na kuzungumza kwamba kanisa la

kikatoliki sio mke wa Kristo bali ni kahaba. Kanisa waliomba maneno yake yachunguzwe

jumapili iliyofuata. Baada ya siku saba, alihubiri Danieli 7, akilinganisha upapa na mpinga

Kristo, Knox alitambua maandiko kuwa mamlaka pekee kwa kutunga mafundisho ya dini

na kuthibitisha umhimu wa haki kwa imani pekee, mambo yaliounda msingi wa mahubiri

yake hadi mwisho wa uhai wake.

Siku kadhaa baadae, John Knox alitoa maandishi ya mafundisho yanayopinga utaratibu wa

misa, pugatori, na maombi kwa wafu. Ndipo palianza kazi ya John Knox, aliyetokea kuwa

mmoja wa wahubiri wa kupinga mafundisho potofu ya kanisa.

Kutoka utumwani kuwa mkuu wa Kanisa katika huduma kwa mfalme

Kundi la waheshimiwa kumi na sita, wafuasi wa mfia dini Wishart, waliokuwa

wamekasirishwa na padre David Beaton kwa kuuwa mhubiri huyo, waliuwa padre huo

52

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!