You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Cemetri ambalo halikuwekwa alama yoyote. Hadi sasa kaburi la John Calvin halijulikani
lilipo.
4. JOHN KNOX
John Knox alizaliwa katika miaka ya 1513 katika Haddington, mji mdogo kaskazini mwa
Edinburg, Scotland. Maisha yake ya awali yalimwezesha kukutana na watu wengi, na
elimu yake ya juu ilimwezesha kuwafikia watu wa hali ya juu katika jamii. Alipoteza
wazazi wake akiwa bado mtoto. Knox alijifunza kilatini shuleni Haddington. Mwaka 1529,
alianza masomo ya Theolojia katika chuo cha mtakatifu Andrews. Aliwekewa mikono ya
ukuhani mwaka 1536 ila hakuajiriwa katika nafasi hiyo kutokana na Scotland kuwa na
makuhani wengi.
Mwaka 1540, utawala wa Scotland ulianza kuwatesa wahubiri wa Neno la Mungu. George
Wishart hakuogopa muda wa majaribu na akasafiri kutoka kijiji kimoja hadi kijiji kingine
kuhubiri ukweli wa Biblia. Knox, kwa kushawishika na ujumbe wa Wishart, aliamua
kumsindikiza kama mlinzi wake, akiwa na mapanga mawili kumkinga mhubiri huyu dhidi
ya vitisho vya watesi. Kwa wiki tano, alimsindikiza Wishart katika kuhubiri kwake mpaka
mamlaka yaliamua kunyamazisha sauti ya mheshimiwa huyu kwa kumfunga gerezani.
John Knox Aliamua kujiunga nae na kumuunga mkono, lakini Wishart alimsihi arudi
nyumbani, akisema: “Hapana, rudi kwa watoto wako, na Mungu akubariki. Mmoja
anatosha kuwa kafara. Knox alirudi.
Henry Balnaves, mmoja ya waheshimiwa, alifurahishwa na kipaji chaa ufundishaji wa
wanamatengenezo na kuungana na mhubiri John Rough kwa kumwalika Knox kuwa mkuu
wa kanisa na mchungaji wa kanisa la nyumba ya mtakatifu Andrews. Knox alikataa
mwaliko huo, nakusema hawakuwa na mamlaka ya kutoa wito huo na kurudi chumbani
mwake
. Wiki chache baade, alihudhuria ibada ambayo mhudumu alitetea kanisa la kikatoliki
kuwa mke wa Kristo. Knox alishindwa kunyamaza na kuzungumza kwamba kanisa la
kikatoliki sio mke wa Kristo bali ni kahaba. Kanisa waliomba maneno yake yachunguzwe
jumapili iliyofuata. Baada ya siku saba, alihubiri Danieli 7, akilinganisha upapa na mpinga
Kristo, Knox alitambua maandiko kuwa mamlaka pekee kwa kutunga mafundisho ya dini
na kuthibitisha umhimu wa haki kwa imani pekee, mambo yaliounda msingi wa mahubiri
yake hadi mwisho wa uhai wake.
Siku kadhaa baadae, John Knox alitoa maandishi ya mafundisho yanayopinga utaratibu wa
misa, pugatori, na maombi kwa wafu. Ndipo palianza kazi ya John Knox, aliyetokea kuwa
mmoja wa wahubiri wa kupinga mafundisho potofu ya kanisa.
Kutoka utumwani kuwa mkuu wa Kanisa katika huduma kwa mfalme
Kundi la waheshimiwa kumi na sita, wafuasi wa mfia dini Wishart, waliokuwa
wamekasirishwa na padre David Beaton kwa kuuwa mhubiri huyo, waliuwa padre huo
52