21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Rafiki zake walimshauri John Calvin kuoa lakini yeye alikataa lakini baada ya muda kupita

alikubali na akamuoa mjane mmoja wa watoto wawili aliyeitwa Idelete Burry Walizaa

mtoto mmoja wa kiume aliefariki siku chache tu baada ya kuzaliwa kwake. Mkewe John

Calvin alifariki baada ya miaka tisa tu tangu kuoana kwao.

John Calvin alikaa kwa muda wa miaka mitatu hivi Strasburgy, wakati huu kanisa Katoliki

lilitaka kuurudisha mji wa Jiniva mikononi mwao. Kwa bahati rafiki zake Calvin

walifanikiwa kuchukua nafasi za uongozi katika baraza la mji wa Jiniva na wakaamua

kumwita John Calvin kurejea tena Jiniva. Mwanzoni Calvin hakuwa tayari kurejea Jiniva

kwa sababu hakuwa na uhakika kama alikuwa mtu sahihi kwa kazi ile. Hatimae mwaka

1541 aliamua kurudi Jiniva.

John Calvin alipokelewa kwa furaha mno pale jiniva na akapewa jukumu la kurejesha

mfumo wa maisha ya kijamii na kidini kulingana na neno la Mungu. Calvin alianza kazi

ya kuhuburi Neno la Mungu kwa mara ya pili pale Jiniva. Kutokana na kanuni

zilizowekwa watu wote kwa pamoja walikuja kusikiliza neno la Mungu. Jiniva

iligawanywa katika sharika (parish) tano zikiwa na wahudumu watatu na wahudumu

wasaidizi wawili. Ilikuwa ni lazima kuhudhuria ibada, faini iliwekwa kwa yeyote

asiyehudhuria

Kufikia katikati ya karne ya 16 John Calvin alikuwa kiongozi maarufu sana wa

matengenezo ya kanisa. Baada ya kifo cha Martin Luther mwaka 1546 watu wengi

waliotilia mashaka mafundisho ya Kanisa Katoliki walimwendea John Calvin kwaajili ya

ushauri na maelekezo.

Afya ya John Calvin ilianza kuzorota, mwili wake ulianza kuwa dhaifu kutokana na

kusoma na mifungo (Fasting). Calvin aliweza kupitisha siku kadhaa bila kula wala kupata

usingizi. Miaka mitatu kabla ya kifo chake afya yake ilizidi kuwa mbaya zaidi. Rafiki zake

walimshauri kupunguza kazi lakini yeye alikataa akawajibu mnataka Bwana anikute

sijamaliza kazi yake ?

Watu wengi waliokimbia mateso kutoka maeneo mbalimbali walipokelewa Jiniva. Mmoja

wa wakimbizi hao alikuwa ni John Knox wa Skotilandi. Vijana wengi walikwenda Jiniva

kuandaliwa kwaajili ya kazi ya huduma ya Injili Ulaya ya kati na ulaya Magharibi.

Mvuto mkubwa wa Calvin ulitokana na mafundisho na mihadhara yake. Vijana wengi

waliokuja kuandaliwa kwaajili ya huduma waliporudi kwao walibeba Kweli ya Neno la

Mungu katika mioyo na akili zao. Walieneza Nuru ya Injili katika maeneo yote.

John Calvin alikuwa anabebwa na kupelekwa kwenye mikutano aliyokuwa anahitaji

kuhudhuria. Mwaka 1564 alipelekwa kwenye ukumbi wa mji kuhudhuria mkutano wa

baraza na aliwashukuru sana kwa yote waliyofanya kwaajili yake. Siku chache viongozi

wa kanisa walimtenbelea akiwa kitandani, Calvin alisalimiana nao na kuwaaga.

Mwanamatengenezo huyu alifariki mnamo Mei 27, 1564 na alizikwa katika kaburi la

51

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!