21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Baada ya kukaa Basel kwa mwaka mmoja john Calvin alimaua kwenda Straburg. Lakini

ilikuwa vigumu kwa yeye kuendelea kuwepo kule kutokana na vita ilyokuwepo kati ya

mfalme Francis I na Mfalme Charles V. hivyo basi John Calvin aliamua kuelekea kusini

na akaamua kutumia usiku mmoja pale Jiniva. Baada ya taarifa za ujio wa John Calvin

kumfikia William ferali mwanamatengenezo ya kanisa wa ufaransa pale Jiniva

alimkaribisha john Calvin na kumuomba kukaa pamoja nae na kuendeleza kazi ya

matengenzo ya kanisa pamoja. Hivi ndivyo john Calvin alivyoingia rasmi katika kazi ya

matengenezo ya Kanisa. Inasadikiwa kuwa john Calvin aliokoka mnamo mwaka 1530.

Ferali aliandika rasimu ya ukiri wa Imani na Calvin aliandika andiko lake la Uhuisho wa

Muundo wa Kanisa jiniva (Reorganization). Mnamo Januari, 16, 1537 Waliwasilisha

Rasimu yao mbele ya baraza la mji. Mwaka huohuo baraza lilikubali na kupitisha rasimu

hiyo.

Kadli miaka ivyozidi kwenda uhusiano baina ya baraza na wanamatengenzo hao ulianza

kuteteleka.Baraza lilisita kusimamia mapendekezo ya rasimu yao kwasababu wananchi

wengi walionekana kutokukubaliana na mapendekezo ya rasimu hiyo. Novemba 26

mwaka hu huo wanamatengenezo hao walifanya mdahalo na baraza kuhusu rasimu yao.

Kulitokea kutokuelewana katika mdahalo huo.

Mgongano mkubwa ulitokea pale ambapo viongozi wa mji wa Bern uliokuwa umeungana

na Jiniva katika matengenezo ya makanisa ya Uswisi ulipotoa mapendekezo ya

kuanzishwa kwa mfumo mmoja unaofanana (unifoymity) wa uendeshaji wa misa. Moja

ya mapendekezo hayo ilikuwa ni kutumika kwa mkate usiotiwa chachu katika sakramenti

ya Ekaristi Takatifu. Wanamatengenezo hao hawakuwa tayari kufuata wala kutekeleza.

Hawakuendesha misa ya sakramenti ya ekaristi wakisubiri mkutano wa sinodi kule Zurich

ambao ndio ungepaswa kutoa maamuzi ya mwisho Baraza liliwaamuru wanamatengenezo

hao kuendesha misa ya sakramenti ya ekaristi wakati wa pasaka. Wanamatengenezo hao

walikataa kuongoza misa wakati wa ibada ya pasaka. Jambo hili lilisababisha vurugu

katika ibada na siku iliyofuata baraza liliwaamuru Wanamatengenezo hao kuondoka mjini

hapo.

Wanamatengenezo hao wawili walipeleka kesi yao kule Zurich na Bern. Sinodi ilipoketi

iliwalaumu sana wanamatengenezo kwa kutokuwa watii kwaajili ya watu wa jiniva. Sinodi

iliwaomba Bern kufanya suruhu kwa lengo la kuwarudisha wanamatengenezo hao.

Baraza la Jiniva lilikataa kuwarudisha wanamatengenezo.

Ferali alipata mwaliko wa kwenda kuongoza kanisa Neuchâtel, John Calvin alipata

mwaliko wa kwenda Strasburg kuongoza kanisa la wakimbizi (refugees) John Calvin

alikutana na wanamatengenezo wa kanisa katika mji huu ambao ni Martin Bucer,

Wolfgang Capito. Miezi michache baadae John Calvin alipewa uraia katika mji huu.

Katika kipindi hiki John Calvin hakuambatana na kanisa moja tu bali bali alifanya kazi

katika makanisa kadhaa yakiwemo St. Nicholas na Kanisa la Dominika. Aliwahudumua

waamini 400-500 katika ibada moja.

50

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!