Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Baada ya kukaa Basel kwa mwaka mmoja john Calvin alimaua kwenda Straburg. Lakini
ilikuwa vigumu kwa yeye kuendelea kuwepo kule kutokana na vita ilyokuwepo kati ya
mfalme Francis I na Mfalme Charles V. hivyo basi John Calvin aliamua kuelekea kusini
na akaamua kutumia usiku mmoja pale Jiniva. Baada ya taarifa za ujio wa John Calvin
kumfikia William ferali mwanamatengenezo ya kanisa wa ufaransa pale Jiniva
alimkaribisha john Calvin na kumuomba kukaa pamoja nae na kuendeleza kazi ya
matengenzo ya kanisa pamoja. Hivi ndivyo john Calvin alivyoingia rasmi katika kazi ya
matengenezo ya Kanisa. Inasadikiwa kuwa john Calvin aliokoka mnamo mwaka 1530.
Ferali aliandika rasimu ya ukiri wa Imani na Calvin aliandika andiko lake la Uhuisho wa
Muundo wa Kanisa jiniva (Reorganization). Mnamo Januari, 16, 1537 Waliwasilisha
Rasimu yao mbele ya baraza la mji. Mwaka huohuo baraza lilikubali na kupitisha rasimu
hiyo.
Kadli miaka ivyozidi kwenda uhusiano baina ya baraza na wanamatengenzo hao ulianza
kuteteleka.Baraza lilisita kusimamia mapendekezo ya rasimu yao kwasababu wananchi
wengi walionekana kutokukubaliana na mapendekezo ya rasimu hiyo. Novemba 26
mwaka hu huo wanamatengenezo hao walifanya mdahalo na baraza kuhusu rasimu yao.
Kulitokea kutokuelewana katika mdahalo huo.
Mgongano mkubwa ulitokea pale ambapo viongozi wa mji wa Bern uliokuwa umeungana
na Jiniva katika matengenezo ya makanisa ya Uswisi ulipotoa mapendekezo ya
kuanzishwa kwa mfumo mmoja unaofanana (unifoymity) wa uendeshaji wa misa. Moja
ya mapendekezo hayo ilikuwa ni kutumika kwa mkate usiotiwa chachu katika sakramenti
ya Ekaristi Takatifu. Wanamatengenezo hao hawakuwa tayari kufuata wala kutekeleza.
Hawakuendesha misa ya sakramenti ya ekaristi wakisubiri mkutano wa sinodi kule Zurich
ambao ndio ungepaswa kutoa maamuzi ya mwisho Baraza liliwaamuru wanamatengenezo
hao kuendesha misa ya sakramenti ya ekaristi wakati wa pasaka. Wanamatengenezo hao
walikataa kuongoza misa wakati wa ibada ya pasaka. Jambo hili lilisababisha vurugu
katika ibada na siku iliyofuata baraza liliwaamuru Wanamatengenezo hao kuondoka mjini
hapo.
Wanamatengenezo hao wawili walipeleka kesi yao kule Zurich na Bern. Sinodi ilipoketi
iliwalaumu sana wanamatengenezo kwa kutokuwa watii kwaajili ya watu wa jiniva. Sinodi
iliwaomba Bern kufanya suruhu kwa lengo la kuwarudisha wanamatengenezo hao.
Baraza la Jiniva lilikataa kuwarudisha wanamatengenezo.
Ferali alipata mwaliko wa kwenda kuongoza kanisa Neuchâtel, John Calvin alipata
mwaliko wa kwenda Strasburg kuongoza kanisa la wakimbizi (refugees) John Calvin
alikutana na wanamatengenezo wa kanisa katika mji huu ambao ni Martin Bucer,
Wolfgang Capito. Miezi michache baadae John Calvin alipewa uraia katika mji huu.
Katika kipindi hiki John Calvin hakuambatana na kanisa moja tu bali bali alifanya kazi
katika makanisa kadhaa yakiwemo St. Nicholas na Kanisa la Dominika. Aliwahudumua
waamini 400-500 katika ibada moja.
50