Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Hivyo neno hilo wakapewa watu wale waliokubali matengenezo ya kanisa. Martin Luther
alifariki dunia mnamo mwaka 17, Februari, 1546.
3. JOHN CALVIN
John Calvin Kwa kifarnsa Jean Cauvin alizaliwa mnamo Julai 10, 1509 katika mji wa
Nayoni jimbo la Picard Ufaransa. Baba yake aliitwa Gerard Cauvin, Mama yake aliitwa
Jeahn Lefrenc. Katika familia yao walizaliwa watoto watano, wakiume watatu na wakike
wawili ambapo mtoto wa kiume wa tatu alifariki angali mchanga siku chache tu baada ya
kuzaliwa. John Calvin alikuwa mtoto wa pili kuzaliwa katika familia ya baba yake. Gerard
Cauvin alikuwa Mwanasheria na msajiri katika ofisi ya Askofu wa Nayon.Gerard Cauvini
alitaka watoto wake wapate elimu bora kulingana na nafasi yake aliyokuwa nayo katika
kanisa. John alikuwa mtoto mwenye akili sana, akiwa na umri wa miaka 12 alipata kazi
katika ofisi ya askofu wa mji. Baba yake alipenda mtoto wake awe kuhani (padre) hivyo
basi John alijiunga na chuo kikuu cha Paris kusomea clasics.
Kabla ya kendelea na masomo zaidi kulitokea mgongano kati ya baba yake na askofu wa
Nayon, jambo ambalo lilimfanya baba yake kumsitisha John kuendelea na masomo katika
chuo kikuu cha Parisi ili asiendelee na matayarisho ya upadri badala yake John Calvin
alijiunga na chuo cha Orleans kusomea sheria.
Katika mwaka wa 1531 Gerard Cauvin alifariki dunia na hapo John Calvin akawa huru
kuchagua kusomea taaluma aliyoihitaji mwenyewe. John Calvin alirudi Paris tena
japokuwa baadae kidogo tena alirejea katika chuo ch Orleans kumalizia masomo yake ya
sheria.
Akiwa Paris alichapisha kitabu chake kimoja alichokiita Ufafanuzi wa kitabu na Seneka
(A commentary of a book by Seneca) mwandishi aliyeishi wakati wa dola ya zamani ya
Rumi.
Kwa wakati huu John Calvin alivutiwa sana na mafundisho ya wanamatenegenzo wa
Ujerumani. Moyo wake ulijazwa na upendo kwa Mungu na kwa watu wake. Inaamininka
kuwa kati ya wanamatengenezo wote wa Kanisa hakuna aliyetoa mchango mkubwa
katika kanisa kama John Calvin. Kwa kuwa hakuna kati yao aliyechunguza Neno la
Mungu kwa kina zaidi na kwa maombi zaidi kama John Calvin.
Wakati Waprotestanti wakiwindwa na kuteswa, john Calvin kwa wazi kabisa aliamua
kuwa upande wao. Aliwatembelea na kuwa tia moyo kwa kadli alivyoweza. Rafiki yake
aliyeitwa Nicholas Cop aliteuliwa kuwa mkuu wa chuo (rector ) chuo kikuu cha mji na
ilionekana kuwa john Calvin alimsaidia kuandaa hotuba yake ya Ufunguzi ambayo katika
hotuba hiyo Nicholas alilishambulia sana kanisa la Roman katoliki na kusisitiza
kufanyika kwa matengenezo. Baada ya hotuba hiyo Nicholas alishambuliwa na wanazuoni
wenzake na viongozi wengine na kuitwa mzushi na akalazimika kukimbia na kwenda
kuishi na wakimbizi kule Uswis Basel ili kuokoa uhai wake.
Baadae john Calvin alihusishwa kwamba alishirikiana na Nicholas Cop hivyo mwaka
uliofuta nayeye alilazimika kukimbia kwaajili ya usalama wake na kwenda Basel Uswisi
Mji wa Basel ulielezwa kuwa mji wa Uhuru na wa makimbilio kwa miaka mingi.
49