21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Hivyo neno hilo wakapewa watu wale waliokubali matengenezo ya kanisa. Martin Luther

alifariki dunia mnamo mwaka 17, Februari, 1546.

3. JOHN CALVIN

John Calvin Kwa kifarnsa Jean Cauvin alizaliwa mnamo Julai 10, 1509 katika mji wa

Nayoni jimbo la Picard Ufaransa. Baba yake aliitwa Gerard Cauvin, Mama yake aliitwa

Jeahn Lefrenc. Katika familia yao walizaliwa watoto watano, wakiume watatu na wakike

wawili ambapo mtoto wa kiume wa tatu alifariki angali mchanga siku chache tu baada ya

kuzaliwa. John Calvin alikuwa mtoto wa pili kuzaliwa katika familia ya baba yake. Gerard

Cauvin alikuwa Mwanasheria na msajiri katika ofisi ya Askofu wa Nayon.Gerard Cauvini

alitaka watoto wake wapate elimu bora kulingana na nafasi yake aliyokuwa nayo katika

kanisa. John alikuwa mtoto mwenye akili sana, akiwa na umri wa miaka 12 alipata kazi

katika ofisi ya askofu wa mji. Baba yake alipenda mtoto wake awe kuhani (padre) hivyo

basi John alijiunga na chuo kikuu cha Paris kusomea clasics.

Kabla ya kendelea na masomo zaidi kulitokea mgongano kati ya baba yake na askofu wa

Nayon, jambo ambalo lilimfanya baba yake kumsitisha John kuendelea na masomo katika

chuo kikuu cha Parisi ili asiendelee na matayarisho ya upadri badala yake John Calvin

alijiunga na chuo cha Orleans kusomea sheria.

Katika mwaka wa 1531 Gerard Cauvin alifariki dunia na hapo John Calvin akawa huru

kuchagua kusomea taaluma aliyoihitaji mwenyewe. John Calvin alirudi Paris tena

japokuwa baadae kidogo tena alirejea katika chuo ch Orleans kumalizia masomo yake ya

sheria.

Akiwa Paris alichapisha kitabu chake kimoja alichokiita Ufafanuzi wa kitabu na Seneka

(A commentary of a book by Seneca) mwandishi aliyeishi wakati wa dola ya zamani ya

Rumi.

Kwa wakati huu John Calvin alivutiwa sana na mafundisho ya wanamatenegenzo wa

Ujerumani. Moyo wake ulijazwa na upendo kwa Mungu na kwa watu wake. Inaamininka

kuwa kati ya wanamatengenezo wote wa Kanisa hakuna aliyetoa mchango mkubwa

katika kanisa kama John Calvin. Kwa kuwa hakuna kati yao aliyechunguza Neno la

Mungu kwa kina zaidi na kwa maombi zaidi kama John Calvin.

Wakati Waprotestanti wakiwindwa na kuteswa, john Calvin kwa wazi kabisa aliamua

kuwa upande wao. Aliwatembelea na kuwa tia moyo kwa kadli alivyoweza. Rafiki yake

aliyeitwa Nicholas Cop aliteuliwa kuwa mkuu wa chuo (rector ) chuo kikuu cha mji na

ilionekana kuwa john Calvin alimsaidia kuandaa hotuba yake ya Ufunguzi ambayo katika

hotuba hiyo Nicholas alilishambulia sana kanisa la Roman katoliki na kusisitiza

kufanyika kwa matengenezo. Baada ya hotuba hiyo Nicholas alishambuliwa na wanazuoni

wenzake na viongozi wengine na kuitwa mzushi na akalazimika kukimbia na kwenda

kuishi na wakimbizi kule Uswis Basel ili kuokoa uhai wake.

Baadae john Calvin alihusishwa kwamba alishirikiana na Nicholas Cop hivyo mwaka

uliofuta nayeye alilazimika kukimbia kwaajili ya usalama wake na kwenda Basel Uswisi

Mji wa Basel ulielezwa kuwa mji wa Uhuru na wa makimbilio kwa miaka mingi.

49

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!