You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
mwaka 15012 alipata shahada ya pili ya udaktari katika Theolojia. Baada ya masomo yake
alianza kufundisha Biblia katika Vyuo Vikuu vya Erfurt na Witternberg Mnamo mwaka
1507 alipata ubarikio na kuwa padre.
Mnamo mwaka 1510, Martin Luther na mmonaki mwingine mmoja walisafiri kwenda
Rumi kwaajili ya shughuli za Chama chao cha umonaki. Akiwa Rumi alishangaa kuona
udhalimu uliokuwa ukifanywa na mapdre huko Rumi. Martin akiwa mmonaki alipata
mabishano makubwa moyoni mwake, na alijiuliza namna gani ambavyo angeweza
kupata rehema za Mungu. Alijipiga, Alifunga na kujitesa kwa muda mrefu ili aweze
kusamehewa dhambi zake. Alipata majibu ya maswali yake yote baada ya kusoma Waraka
kwa Warumi 1:16-17. Ukiwa na maneno mwenye haki ataishi kwa imani.
Wakati huo huo papa Leo X aliwatuma wawakilishi wake katika nchi mbalimbali
kukusanya fedha kwajili ya ujenzi wa kanisa la Mt Petro. Walikusanya fedha hivyo kwa
njia ya kuuza vyeti vya msamaha. Wakristo waliweza kununua vyeti kwajili yao wenyewe
na kwaajili ya ndugu zao waliokwisha kufariki ili waweze kupata msamaha.
Luther alipinga vikali jambo hili pamoja na mambo mengine ambayo yalikuwa kinyume
na Maandiko matakatifu kwa kuandika hoja 95 na kuzibandika katika mlango wa kanisa
Huko Wittenberg. Rafiki zake Luther walipiga kopi hoja hizo na kuzisambaza katika
maeneo mbalimbali ya nchi ya ujerumani ili ziweze kusomwa na watu wote. Kwa muda
mfupi nakala hizo ziliweza kuenea na mafundisho ya Luther yakaenea katika maeneo
mbalimbali.
Baada ya hoja hizo kuenea Luther aliitwa na Kardinali, Cajetan katika mji wa Dusgbarg (
1518). Kardinari huyo alimtaka Luther kukiri makosa yake lakini Luther alipinga swala
hilo.
Papa Leo X alimwandikia Luther barua ya kumtishia kumtenga na kanisa iwapo hangekiri
makosa yake. Baada ya Luther kuipata barua hii aliichoma moto hadharani mbele ya
kadamnasi
Mnamo mwaka 1521. Luther alitengwa rasmi na kanisa Katoliki. Luther aliitwa katika
mkutano uliofanyika katika mji wa worms ulioitishwa na kaisari Charles V, ili aweze
kusikilizwa na kumaliza mgogoro. Katika mkutano huo Luther alitakwa kukiri makosa
yake kuhusu vitabu alivyokuwa ameviandika na kuvisambaza. Luther alikataa kubadili
msimamo wake, kuyakana maandishi yake, na hatimaye kaisari na wafalme wake
walitangaza hukumu ya kifo dhidi ya Luther. Katika mkutano huo kulitokea fujo na
hatimae Luther alitoroka na kuokolewa na mfalme Fredrick wa Saksoni na kupelekwa
katika boma lake la Wartburg. Akiwa huko alijificha kama mfungwa na alibadilishwa jina
na kuitwa Jorg na kupelekewa nguo zingine. Alibadili sura yake kwa kufuga ndevu.
Akiwa katika boma hilo alianza kazi ya kutafsiri Biblia katika lugha ya kijerumani.
Katika muda huu wa kukaa mafichoni Luther alifanya kazi kubwa ya matengenzo kuliko
wakati mwingine wote kwake.
Mnamo mwaka 1529 Wafalme walibadili msimamo wao wakaamua kupigana dhidi ya
wanamatengenezo. Wafalme 19 walipinga uamuzi huu, na hivyo wakaitwa waprotestanti.
48