Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
waliongoza kikundi cha watu katika kujifunza kikamilifu mafundisho ya Biblia juu ya
ubatizo.
Mwaka 1524 walihitimisha kwamba ubatizo usifanywe kwa watoto wadogo. Walifundisha
kwamba watu waliompokea Yesu kama Bwana na mwokozi wao ndio wanaostahili
kubatizwa. Pia walitengeneza mawazo mapya kuhusu kanisa wakiamini kwamba kanisa la
kweli lilikuwa linahusisha watu wale walibatizwa baada ya kukiri.
Vijana hawa walijaribu kumshawishi mlezi wao wa zamani akubaliane na mawazo haya,
kwa kiasi fulani Zwingli alikubaliana na mawazo haya, japo shauku yake ya kuwapendeza
watawala ilisababisha kuwakataa na kupinga mawazo ya hawa wanafunzi wake wa
zamani.
Katika mdahalo wa Januari 18-19 – 1525 vijana hawa walibishana na Zwingli kuhusu
suala la ubatizo wa watoto, Kiongozi wa mji alimtangaza Zwingly kuwa mshindi wa
mdahalo huo na akatangaza ya kwamba yeyote ambaye hangefanya ubatizo wa watoto
wadogo au angebatiza ubatizo wa waamini alitakiwa ama kutubu au kuondoka Zurich
ndani ya siku nane.
Kuanzishwa kwa kanisa huru la kwanza.
Katika nyumba ya Conrad Grebel walikusanyika watu wachache ili kujadili nini
walitakiwa kufanya. Baada ya majadiliano hayo walifikia uamuzi wa kwamba wanatakiwa
kubatizwa upya kwa kwa sababu wote walibatizwa wakiwa watoto katika kanisa Katoliki.
Conrad alimbatiza George Blaurock kwa sababu mtu huyu alikuwa ni padre. Hivyo baada
ya kubatizwa kwake alipewa jukumu la kuwabatiza wengine. Kwa sababu hii walianza
kuitwa wanabatisti, maana yake ikiwa ni wabatizwa upya.
Hii ilikuwa ni moja ya mapinduzi ya matengenezo. Mapinduzi haya yalianzisha kanisa
jipya. Watu hawa walianza kukutana kwaajili ya ibada na wakaanza kueneza kanisa lao
katika maeneo mbalimbali.Kikundi hiki pia kiliitwa undugu wa uswisi.
Baada ya mlengo huu kukua na kuenea, ulishambuliwa na kupingwa sana karibu katika
Ulaya nzima. Kanisa la Romani Katoliki, pamoja na wanamatengenezo yaani Martin
Luther pamoja na John Calvin walihusika katika kuwaua Wanabatisti. Zaidi ya wanabatisti
4000 walinyongwa.
Mnamo mwaka 1529 wanamatengenezo walikutana katika mji wa Marbag ili kuweza
kuimarisha umoja wao. Wanamatengezo hao walikubaliana katika mambo kadhaa, lakini
kulitokea kutokukubaliana katika jambo moja ambalo ni meza ya Bwana. Zwingli alisema
kwamba mkate na divai ni kielelezo tu cha ukumbusho wa mauti ya Yesu, wakati Luther
alikaza kwamba kwa namna fulani Yesu alikuwa katika mkate na divai kwa njia ya fumbo.
Jambo hili lilileta utengano mkubwa baina ya wanamatengenezo hawa.
Kulizuka vita baina ya Kanisa la Romani katoliki na Waprotestant, katika vita hiyo
Zwingly aliuawa, hii ilikuwa mwaka 1531.
2. MARTIN LUTHER.
Martin Luther alizaliwa mnamo mwaka 1483. Baba yake aliitwa Hans na mama yake
aliitwa magareth. Alizaliwa katika familia ya kimsikini, baba yake alikuwa mfanyakazi
katika mgodi wa madini. Martin Luther alisoma Theolojia katika vyuo vikuu vya Erfurt
na Edburg. Mnamo mwaka 1505 alitunukiwa shahada ya kwanza katika falsafa na katika
47