21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

waliongoza kikundi cha watu katika kujifunza kikamilifu mafundisho ya Biblia juu ya

ubatizo.

Mwaka 1524 walihitimisha kwamba ubatizo usifanywe kwa watoto wadogo. Walifundisha

kwamba watu waliompokea Yesu kama Bwana na mwokozi wao ndio wanaostahili

kubatizwa. Pia walitengeneza mawazo mapya kuhusu kanisa wakiamini kwamba kanisa la

kweli lilikuwa linahusisha watu wale walibatizwa baada ya kukiri.

Vijana hawa walijaribu kumshawishi mlezi wao wa zamani akubaliane na mawazo haya,

kwa kiasi fulani Zwingli alikubaliana na mawazo haya, japo shauku yake ya kuwapendeza

watawala ilisababisha kuwakataa na kupinga mawazo ya hawa wanafunzi wake wa

zamani.

Katika mdahalo wa Januari 18-19 – 1525 vijana hawa walibishana na Zwingli kuhusu

suala la ubatizo wa watoto, Kiongozi wa mji alimtangaza Zwingly kuwa mshindi wa

mdahalo huo na akatangaza ya kwamba yeyote ambaye hangefanya ubatizo wa watoto

wadogo au angebatiza ubatizo wa waamini alitakiwa ama kutubu au kuondoka Zurich

ndani ya siku nane.

Kuanzishwa kwa kanisa huru la kwanza.

Katika nyumba ya Conrad Grebel walikusanyika watu wachache ili kujadili nini

walitakiwa kufanya. Baada ya majadiliano hayo walifikia uamuzi wa kwamba wanatakiwa

kubatizwa upya kwa kwa sababu wote walibatizwa wakiwa watoto katika kanisa Katoliki.

Conrad alimbatiza George Blaurock kwa sababu mtu huyu alikuwa ni padre. Hivyo baada

ya kubatizwa kwake alipewa jukumu la kuwabatiza wengine. Kwa sababu hii walianza

kuitwa wanabatisti, maana yake ikiwa ni wabatizwa upya.

Hii ilikuwa ni moja ya mapinduzi ya matengenezo. Mapinduzi haya yalianzisha kanisa

jipya. Watu hawa walianza kukutana kwaajili ya ibada na wakaanza kueneza kanisa lao

katika maeneo mbalimbali.Kikundi hiki pia kiliitwa undugu wa uswisi.

Baada ya mlengo huu kukua na kuenea, ulishambuliwa na kupingwa sana karibu katika

Ulaya nzima. Kanisa la Romani Katoliki, pamoja na wanamatengenezo yaani Martin

Luther pamoja na John Calvin walihusika katika kuwaua Wanabatisti. Zaidi ya wanabatisti

4000 walinyongwa.

Mnamo mwaka 1529 wanamatengenezo walikutana katika mji wa Marbag ili kuweza

kuimarisha umoja wao. Wanamatengezo hao walikubaliana katika mambo kadhaa, lakini

kulitokea kutokukubaliana katika jambo moja ambalo ni meza ya Bwana. Zwingli alisema

kwamba mkate na divai ni kielelezo tu cha ukumbusho wa mauti ya Yesu, wakati Luther

alikaza kwamba kwa namna fulani Yesu alikuwa katika mkate na divai kwa njia ya fumbo.

Jambo hili lilileta utengano mkubwa baina ya wanamatengenezo hawa.

Kulizuka vita baina ya Kanisa la Romani katoliki na Waprotestant, katika vita hiyo

Zwingly aliuawa, hii ilikuwa mwaka 1531.

2. MARTIN LUTHER.

Martin Luther alizaliwa mnamo mwaka 1483. Baba yake aliitwa Hans na mama yake

aliitwa magareth. Alizaliwa katika familia ya kimsikini, baba yake alikuwa mfanyakazi

katika mgodi wa madini. Martin Luther alisoma Theolojia katika vyuo vikuu vya Erfurt

na Edburg. Mnamo mwaka 1505 alitunukiwa shahada ya kwanza katika falsafa na katika

47

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!