21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

B. VIONGOZI WA MATENGENEZO YA KANISA.

Katika kipengele hiki tutawatalii baadhi ya wanamatengenezo ya kanisa, yaani

tutawachunguza watu ambao Mungu aliwatumia kuleta kweli ya neno la Mungu katika

kanisa lililokuwa limepotoka na lisilokubali matengenezo kwa hiali. Tutawatalii

wanamatengenezo wafuatao, Martn Luther, John Calvin, Ulrich Zwingli na John

Knox.

1. ULRICH ZWINGLY

Alikuwa ni mwanamatengenezo wa kanisa wa kiswisi asiyejulikana sana kama Martn

Luther na John Calvin lakini aliye na mchango mkubwa katika mategenezo ya kanisa.

Alizaliwa mwaka 1484, na kuelimishwa katika Chuo kikuu cha Basel na Vienna

akisomea fani ya ubinadamu (humanism). Alifanya kazi kama Padre wa Parish Huko

Glarus Uswisi mwaka 1512. Katika mwaka wa 1515 Ulrich alianza kuyatilia shaka

mafundisho ya Kanisa Katoliki na alianzisha kile kilichoitwa matengenezo ya Zurich.

Alihubiri jumbe za ki-Biblia na kufanikiwa kulibadilisha baraza la mji kuwa na mtazamo

kama wa kwake.

Baraza hili liliufanya mji kuwa ngome ya Uprotestant. Hoja 67 za Zwingli

ziliasiliwa(adopted) na kufanywa Mafundisho rasmi ya mji na mji uliweza kubadilika kwa

haraka sana. Mahubiri na mafundisho yalifanywa mara kwa mara, sanamu ziliondolewa ,

mapadre waliruhusiwa kuoa, Watawa walihamasishwa kutoka katika makao yao

yaliyowatenga na jamii na kuja kuishi na jamii. Nyumba za kitawa zilivunjika na

wakatumia mali zao katika kufadhili elimu na misaada kwa maskini.

Mwaka 1525 Zwingly alijitenga na kanisa katoliki, na akaanzisha mlengo wake. Mnamo

mwaka 1450 baada ya kuongoka Zwingly alianza kuwakusanya wanafunzi waliopenda

kujifunza kigiriki, baadhi ya wanafunzi hawa waliongoka na wakavutiwa sana na Biblia.

Katika mdahalo wa mji uliofanyika katika ukumbi wa mji, Zwingly aliwasilisha hoja 67

Mnamo Februari1523 ambamo aliambatisha mamlaka ya Kanisa la Romani Katoliki.

Mamlaka ya papa, kuwabudu watakatifu, wokovu kwa matendo mema, mifungo, sikukuu,

hija, vikundi (order) vya watawa, useja kwa mapadre, Uuuzaji wa vyeti vya msamaha,

adhabu na toharani. Viongozi wa mji walivutiwa sana na hoja za Zwingli.

Katika mdahalo mwingine wa Oktoba 1523 Zwingli alishambulia matumizi ya sanamu na

akataka kuiondoa Krismas. Viongozi wa mji hawakukubaliana na jambo hili na hivyo

zwingly alikaa kimya. Zwingry aliwaogopa watawala. Kulitokea kutoridhishwa kwa

wanafunzi wake Zwinngry

Baadhi ya wanafunzi wake waliokuwa wamemsaidia katika kuhitimisha hoja zake zote

mbili walijisikia kwamba wamesalitiwa na Zwingli. Kwa kuacha kushughulikia swala la

Sakramenti, kwa kuwapendeza watawala. Walikuwa wamefundishwa na yeye mwenyewe

kufuata mafundisho ya Biblia hivyo wakatambua kwamba Zwingly hakuwa anawaongoza

katika mwelekeo sahihi. Hivyo wakaamua kuanza kujisimamia wenyewe.

Vijana hawa walikuwa ni Conrad Grebel na Felix Manz. Conrad alikuwa ni mwanazuoni

wa kigiriki na Felix alikuwa ni mwanazuoni wa kiebrania. Kwa pamoja vijana hawa

46

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!