21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

matengenezo na mengine mengi kulipeleka kuanza kwa nguvu wimbi kubwa la

matengenezo.

Hadi kufikia miaka 1500 misingi ya jamii ya kipindi cha giza ilikuwa inabadilika

kutokana na mabadiliko ya kielimu, kisiasa, kidini na kiuchumi. Kanisa la ulimwengu

lilianza kupoteza nguvu na kanisa la kitaifa likaanza kuchukua nafasi

Kupanuka kijiografia kulileta mabadiliko mengi katika kufikiri. Kwa kifupi kulikuwa na

sababu mbalimbali zilizopelekea wimbi la matengenezo ya kanisa kutokea, baadhi ya

sababu hizo ni;

1. Kukua kwa utaifa(nationalism).

Kila nchi ilianza kuweka mkazo kujijenga yenyewe, hivyo nchi mbalimbali zilianza

kujitenga na ushirikiano wa kimataifa, Hii ilipelekea kanisa la ulimwengu kokosa nguvu

kwani utaifa ulisababisha kuanza kwa kanisa la kitaifa kila mahali.

Mgogoro wa kanisa katika karne ya 14 na 15.(Utumwa wa Babeli. Kugombania madaraka

yaupapa.)(Great Schism)

2. Kuvumbuliwa kwa mashine za uchapishaji.

Johann Guthenberg alivumbua mashine ya uchapaji mwaka 1456. Mpaka wakati huu

vitabu vyote viliandkwa na kunakiliwa kwa mkono. Kuvumbuliwa kwa mashine hii

kulisababisha Biblia na maandiko mengine kuchapwa na kusambazwa katika maeneo

mbalimbali. Kusambazwa kwa maandiko hayo kulipelekea kuamsha akili za watu na

kutambua hitaji la kuwepo kwa mabadiliko katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kanisa.

3. Kuzuka kwa mwamko wa kujifunza. (Renaissence)

Hiki kilikuwa ni kipindi ambacho ulizuka mwamko mkubwa

wa kujifunza . Kipindi hiki kilianza huko Ulaya Italia karne ya 14 na kuendelea hadi

karne ya 17. Wasomi wengi waliibuka katika kipindi hiki. Watu walianza kufikiri mambo

kwa upya kutokana na elimu waliyokuwa wamepata. Kutokana na elimu hiyo watu

walihitaji mabadiliko katika maeneo mbalimbali ili kuweza kuleta maendeleo. Hivyo

kanisa nalo likajikuta linahitaji mabadiliko japo kuwa halikuwa tayari kwaajili ya

mabadiliko hayo. Tunaweza kufupisha sababu zilizopelekea matengenezo ya kanisa kwa

kuziorodhesha hapa chini kama ifuatavyo:-

Mgogoro wa kanisa katika karne ya 14 na 15.( Great Schism)

Rushwa.

Kanisa kutojali maisha ya kiroho ya watu na kujikita katika mambo ya kiuchumi.

Kuuzwa kwa vyeti vya msamaha

Upendeleo. (Mtu mmoja kuwa na vyeo vingi kwa wakati mmoja)

Mapapa kukosa maadili.

Mapadri kuwa na elimu duni.

Kuzuka kwa falsafa ya Mantiki.

45

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!