You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
matengenezo na mengine mengi kulipeleka kuanza kwa nguvu wimbi kubwa la
matengenezo.
Hadi kufikia miaka 1500 misingi ya jamii ya kipindi cha giza ilikuwa inabadilika
kutokana na mabadiliko ya kielimu, kisiasa, kidini na kiuchumi. Kanisa la ulimwengu
lilianza kupoteza nguvu na kanisa la kitaifa likaanza kuchukua nafasi
Kupanuka kijiografia kulileta mabadiliko mengi katika kufikiri. Kwa kifupi kulikuwa na
sababu mbalimbali zilizopelekea wimbi la matengenezo ya kanisa kutokea, baadhi ya
sababu hizo ni;
1. Kukua kwa utaifa(nationalism).
Kila nchi ilianza kuweka mkazo kujijenga yenyewe, hivyo nchi mbalimbali zilianza
kujitenga na ushirikiano wa kimataifa, Hii ilipelekea kanisa la ulimwengu kokosa nguvu
kwani utaifa ulisababisha kuanza kwa kanisa la kitaifa kila mahali.
Mgogoro wa kanisa katika karne ya 14 na 15.(Utumwa wa Babeli. Kugombania madaraka
yaupapa.)(Great Schism)
2. Kuvumbuliwa kwa mashine za uchapishaji.
Johann Guthenberg alivumbua mashine ya uchapaji mwaka 1456. Mpaka wakati huu
vitabu vyote viliandkwa na kunakiliwa kwa mkono. Kuvumbuliwa kwa mashine hii
kulisababisha Biblia na maandiko mengine kuchapwa na kusambazwa katika maeneo
mbalimbali. Kusambazwa kwa maandiko hayo kulipelekea kuamsha akili za watu na
kutambua hitaji la kuwepo kwa mabadiliko katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kanisa.
3. Kuzuka kwa mwamko wa kujifunza. (Renaissence)
Hiki kilikuwa ni kipindi ambacho ulizuka mwamko mkubwa
wa kujifunza . Kipindi hiki kilianza huko Ulaya Italia karne ya 14 na kuendelea hadi
karne ya 17. Wasomi wengi waliibuka katika kipindi hiki. Watu walianza kufikiri mambo
kwa upya kutokana na elimu waliyokuwa wamepata. Kutokana na elimu hiyo watu
walihitaji mabadiliko katika maeneo mbalimbali ili kuweza kuleta maendeleo. Hivyo
kanisa nalo likajikuta linahitaji mabadiliko japo kuwa halikuwa tayari kwaajili ya
mabadiliko hayo. Tunaweza kufupisha sababu zilizopelekea matengenezo ya kanisa kwa
kuziorodhesha hapa chini kama ifuatavyo:-
Mgogoro wa kanisa katika karne ya 14 na 15.( Great Schism)
Rushwa.
Kanisa kutojali maisha ya kiroho ya watu na kujikita katika mambo ya kiuchumi.
Kuuzwa kwa vyeti vya msamaha
Upendeleo. (Mtu mmoja kuwa na vyeo vingi kwa wakati mmoja)
Mapapa kukosa maadili.
Mapadri kuwa na elimu duni.
Kuzuka kwa falsafa ya Mantiki.
45