21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

kipagani, picha za ngono na kila kitu walichodhani kuwa ni kiovu. Hakika uamsho mkuu

ulitokea kama alivyokuwa ametabiri.

Jerome alitabiri kwamba angehubiri kwa miaka nane tu pale Florence na kisha angeuawa.

Katika mwaka 1498 Jerome alimshutumu papa Alexander VI kwa kutangaza hadharani

maovu aliyokuwa anayafanya yeye na wasaidizi wake. Baada ya mkasa huo Alexander VI

aliamua kumwekea vikwazo na kisha baadaye akamnyonga na kuuchoma moto mwili

wake mnamo mwaka huohuo wa 1498. Maneno yake ya mwisho akiwa anauawa alisema

“ Bwana Aliteseka sana kwaajili yangu”. Mapambano yake dhidi ya papa yalimfanya

kuwa shujaa na kuwa mtangulizi wa matengenezo ya kanisa. Alikuwa tayari kuitetea

imani kwa gharama yoyote.

Wanamatengenzo watangulizi walionyesha ushujaa katika kuitetea imani. Hawakukubali

kusalimu amri kwa uongozi wa kanisa au serikali na hawakuwa tayari kunyamaza kimya

na kuacha hali mbaya kuendelea kulitafuna kanisa, walikubali kulipa gharama katika

kuitetea imani na kupinga uovu. Walitengeneza njia ambayo ilifuatwa na

wanamatengenezo wakuu baadae kidogo katika kipindi cha kanisa la Sardi yaani kanisa la

matengezo.

Kuna mengi ambayo twaweza kujifunza kwa watu hao kutokana na vile kila mmoja

alivyosimamia kusudi lake kwa ujasiri na imani kuu. Kama tutajifunza na kutetea imani kama

wao tunaweza kuleta matengenezo katika kanisa vuguvugu la wakati huu wa mwisho

F. KUANGUKA KWA KOSTANTINOPALI.

Wanahistoria wengi wana tazama kuanguka kwa Kostantinopali kama mpaka wa kipindi

cha karne za katikati na nyakati hizi zetu. Waislamu toka Uturuki waliivamia

Kostantinopali na kuishinda mnamo mwaka 1453. Hekalu zuri liliojengwa na mfalme

Kostantino lililojulikana kama Saint Sophia liligeuzwa na kuwa msikiti. Huu ndio

uliokuwa mwisho wa kipindi cha giza au mediaval Period.

MADA YA SITA

KIPINDI CHA SARDI KANISA LA MATENGENEZO

KIPINDI : Tangu kuanguka kwa Kostantinopali hadi Patano la Amani la Westpharia.

A. SABABU ZA KUZUKA KWA MATENGENEZO YA KANISA.

Kitendo cha Kanisa la Rumi kutokuwa tayari kupokea mabadiliko yaliyokuwa

yanapendekezwa na watu wema kama vile, Wikrif na Hus, viongozi wa baraza la

44

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!