You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
kipagani, picha za ngono na kila kitu walichodhani kuwa ni kiovu. Hakika uamsho mkuu
ulitokea kama alivyokuwa ametabiri.
Jerome alitabiri kwamba angehubiri kwa miaka nane tu pale Florence na kisha angeuawa.
Katika mwaka 1498 Jerome alimshutumu papa Alexander VI kwa kutangaza hadharani
maovu aliyokuwa anayafanya yeye na wasaidizi wake. Baada ya mkasa huo Alexander VI
aliamua kumwekea vikwazo na kisha baadaye akamnyonga na kuuchoma moto mwili
wake mnamo mwaka huohuo wa 1498. Maneno yake ya mwisho akiwa anauawa alisema
“ Bwana Aliteseka sana kwaajili yangu”. Mapambano yake dhidi ya papa yalimfanya
kuwa shujaa na kuwa mtangulizi wa matengenezo ya kanisa. Alikuwa tayari kuitetea
imani kwa gharama yoyote.
Wanamatengenzo watangulizi walionyesha ushujaa katika kuitetea imani. Hawakukubali
kusalimu amri kwa uongozi wa kanisa au serikali na hawakuwa tayari kunyamaza kimya
na kuacha hali mbaya kuendelea kulitafuna kanisa, walikubali kulipa gharama katika
kuitetea imani na kupinga uovu. Walitengeneza njia ambayo ilifuatwa na
wanamatengenezo wakuu baadae kidogo katika kipindi cha kanisa la Sardi yaani kanisa la
matengezo.
Kuna mengi ambayo twaweza kujifunza kwa watu hao kutokana na vile kila mmoja
alivyosimamia kusudi lake kwa ujasiri na imani kuu. Kama tutajifunza na kutetea imani kama
wao tunaweza kuleta matengenezo katika kanisa vuguvugu la wakati huu wa mwisho
F. KUANGUKA KWA KOSTANTINOPALI.
Wanahistoria wengi wana tazama kuanguka kwa Kostantinopali kama mpaka wa kipindi
cha karne za katikati na nyakati hizi zetu. Waislamu toka Uturuki waliivamia
Kostantinopali na kuishinda mnamo mwaka 1453. Hekalu zuri liliojengwa na mfalme
Kostantino lililojulikana kama Saint Sophia liligeuzwa na kuwa msikiti. Huu ndio
uliokuwa mwisho wa kipindi cha giza au mediaval Period.
MADA YA SITA
KIPINDI CHA SARDI KANISA LA MATENGENEZO
KIPINDI : Tangu kuanguka kwa Kostantinopali hadi Patano la Amani la Westpharia.
A. SABABU ZA KUZUKA KWA MATENGENEZO YA KANISA.
Kitendo cha Kanisa la Rumi kutokuwa tayari kupokea mabadiliko yaliyokuwa
yanapendekezwa na watu wema kama vile, Wikrif na Hus, viongozi wa baraza la
44