You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
maandiko ya John Wikrif na hivyo alianza kuhubiri mafundisho ya mtangulizi wake
Wikrif.
Alipinga mafundisho mbalimbali yasiyo ya ki-Biblia ya kanisa la Romani katoliki na
akasisitiza watu kuishi maisha matakatifu. Alisisitiza kwamba Biblia ndiyo mamlaka ya
mwisho kwa mwamini na katika huduma za kanisa.
Katika kitabu chake alichoandika juu ya kanisa, alifasili kwamba kanisa ni mwili wa
Kristo, na Yesu Kristo pekee akiwa kiongozi wake mkuu. Alitetea nafasi ya ukuhani na
kudai kwamba Mungu pekee ndiye aliyekuwa na uwezo wa kusamehe dhambi. Alieleza
kwamba hakuna mamlaka ya kanisa inayoruhusiwa kuanzisha mafundisho (doctrine)
yaliyo kinyume na Biblia na kwamba Waamini hawatakiwi kutii maagizo yasiyo ya
kimaandiko.
John Hus Alipinga baadhi ya mambo yafuatayo,
Udhalimu wa mapadre
kuuzwa kwa vyeti vya msamaha,
kuondolewa kikombe cha divai kwa walei.
Kanisa kuwa na mamlaka juu ya Biblia
Uwezo wa Makuhani kusamehe dhambi
Ukuhani wa wachache (crerism)
Baada ya mashambulizi hayo mazito dhidi ya mafundisho ya kanisa Hus alifukuzwa
upadre na akaambiwa abadilishe msimamo wake kwa kufuta kauli, jambo ambalo Hus
hakukubaliana nalo. Hatimae Hus alihukumiwa kifo na akachomwa moto. Hus akiwa
anachomwa moto alitoa unabii kwa kusema “leo mnaniua mimi lakini miaka miamoja
ijayo Mungu atamwinua mtu mwingine ambaye matengenezo yake hayataweza
kuzimwa” Kweli baada ya kipindi hicho Mungu alimwinua Martin Luther mwana
matengenezo mkuu kama tutakavyoona hapo baadae.
4. JEROME SAVANAROLA.
Alizaliwa Ferrara Italia mnamo mwaka 1452, alikuwa ni mtawa wa shiriki la wadominico.
Mtu huyu alijaribu kuleta matengenezo katika kanisa na serikali. Alipinga uovu uliokuwa
unafanywa na mapapa. Alisomea mambo ya ubinadamu na utabibu. Kufikia mwaka 1491
alikuwa mhubiri maarufu kule Frolence.
Alitabiri kwamba papa na mfalme wa Naples wangekufa siku moja, jambo ambalo
lilitokea kama alivyotabiri. Katika mahubiri yake alitabiri hukumu kubwa ambayo
ingekuja juu ya mji ikifuatiwa na kipindi chema ambapo Frolence ingewaunganisha watu
wote wa Itali. Utimilizo wa unabii huu ulionekana kuwa ni kuvamiwa kwa Itali na mfalme
Charles VIII. Ambaye mwaka 1494 aliuondoa utawala dhalimu wa Frolence.
Baada ya kuanzishwa kwa serikali mpya Saravano alipata umaarufu sana pale Frolence
kupitia mahubiri yake na alileta mabadiliko mengi katika jamii. Alianzisha matengenezo
ya kodi, Kusaidia maskini na matengenezo katika mahakama. Aliubadilisha mji kutoka
katika maisha ya kimwili na kuishi maisha ya kiroho.
Kutokana na mabadiliko hayo kila mtu katika mji alikwenda kanisani na matajiri waliwapa
misaada masikini.Wafanya biashara walirudisha vitu walivyokuwa wamewatapeli wateja
wao. Waimbaji waliacha kuimba nyimbo za kidunia na kuanza kuimba nyimbo za kumsifu
Mungu. Waliachana na maisha maovu, walichoma moto mawigi, vinyago, vitabu vya
43