21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

maandiko ya John Wikrif na hivyo alianza kuhubiri mafundisho ya mtangulizi wake

Wikrif.

Alipinga mafundisho mbalimbali yasiyo ya ki-Biblia ya kanisa la Romani katoliki na

akasisitiza watu kuishi maisha matakatifu. Alisisitiza kwamba Biblia ndiyo mamlaka ya

mwisho kwa mwamini na katika huduma za kanisa.

Katika kitabu chake alichoandika juu ya kanisa, alifasili kwamba kanisa ni mwili wa

Kristo, na Yesu Kristo pekee akiwa kiongozi wake mkuu. Alitetea nafasi ya ukuhani na

kudai kwamba Mungu pekee ndiye aliyekuwa na uwezo wa kusamehe dhambi. Alieleza

kwamba hakuna mamlaka ya kanisa inayoruhusiwa kuanzisha mafundisho (doctrine)

yaliyo kinyume na Biblia na kwamba Waamini hawatakiwi kutii maagizo yasiyo ya

kimaandiko.

John Hus Alipinga baadhi ya mambo yafuatayo,

Udhalimu wa mapadre

kuuzwa kwa vyeti vya msamaha,

kuondolewa kikombe cha divai kwa walei.

Kanisa kuwa na mamlaka juu ya Biblia

Uwezo wa Makuhani kusamehe dhambi

Ukuhani wa wachache (crerism)

Baada ya mashambulizi hayo mazito dhidi ya mafundisho ya kanisa Hus alifukuzwa

upadre na akaambiwa abadilishe msimamo wake kwa kufuta kauli, jambo ambalo Hus

hakukubaliana nalo. Hatimae Hus alihukumiwa kifo na akachomwa moto. Hus akiwa

anachomwa moto alitoa unabii kwa kusema “leo mnaniua mimi lakini miaka miamoja

ijayo Mungu atamwinua mtu mwingine ambaye matengenezo yake hayataweza

kuzimwa” Kweli baada ya kipindi hicho Mungu alimwinua Martin Luther mwana

matengenezo mkuu kama tutakavyoona hapo baadae.

4. JEROME SAVANAROLA.

Alizaliwa Ferrara Italia mnamo mwaka 1452, alikuwa ni mtawa wa shiriki la wadominico.

Mtu huyu alijaribu kuleta matengenezo katika kanisa na serikali. Alipinga uovu uliokuwa

unafanywa na mapapa. Alisomea mambo ya ubinadamu na utabibu. Kufikia mwaka 1491

alikuwa mhubiri maarufu kule Frolence.

Alitabiri kwamba papa na mfalme wa Naples wangekufa siku moja, jambo ambalo

lilitokea kama alivyotabiri. Katika mahubiri yake alitabiri hukumu kubwa ambayo

ingekuja juu ya mji ikifuatiwa na kipindi chema ambapo Frolence ingewaunganisha watu

wote wa Itali. Utimilizo wa unabii huu ulionekana kuwa ni kuvamiwa kwa Itali na mfalme

Charles VIII. Ambaye mwaka 1494 aliuondoa utawala dhalimu wa Frolence.

Baada ya kuanzishwa kwa serikali mpya Saravano alipata umaarufu sana pale Frolence

kupitia mahubiri yake na alileta mabadiliko mengi katika jamii. Alianzisha matengenezo

ya kodi, Kusaidia maskini na matengenezo katika mahakama. Aliubadilisha mji kutoka

katika maisha ya kimwili na kuishi maisha ya kiroho.

Kutokana na mabadiliko hayo kila mtu katika mji alikwenda kanisani na matajiri waliwapa

misaada masikini.Wafanya biashara walirudisha vitu walivyokuwa wamewatapeli wateja

wao. Waimbaji waliacha kuimba nyimbo za kidunia na kuanza kuimba nyimbo za kumsifu

Mungu. Waliachana na maisha maovu, walichoma moto mawigi, vinyago, vitabu vya

43

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!