21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Kugombea ukuu, Madai ya kanisa la mashariki ya kuwa ni kanisa la kitawala.

D. KUSITAWI KWA UTAWA.

Mashirika mbalimbali ya kitawa yalisitawi katika kipindi hiki na yakajitolea kusaidia jamii

katika maeneo mbalimbali. Baadhi ya mashrika hayo ni :

Wabenedectino walianza mwaka 529 BK

Wasisteri mwaka 1098.

Wafransiska mwaka 1209.

Wadomenica mwaka 1215.

Kipindi cha karne za katikati kilichangia sana katika ustaarabu wa ulimwengu, hasa katika

mambo ya elimu, maandiko, na mambo ya ufundi, katika kipindi hiki zilijengwa kathedro

kubwa . kuna baadhi ya vyuo vikuu vikubwa vilivyojengwa wakati huu, mfano wa vyuo

vikuu hivyo ni Chuo kikuu cha Parisi huko Ufarasnsa, Chuo Kikuu cha Kambridge,

Chuo Kikuu cha Oxford, na vyote viwili vikiwa huko Uingereza. Kuanzishwa kwa vyuo

vikuu hivi kulipelekea elimu kukua na kuleta mtazamo mpya katika jamii kama

tutakavyoangalia baadae katika kipindi kitakachofuata.

E. WATANGULIZI WA MATENGENEZO YA KANISA.

Katika mwaka wa 1229 kanisa la Rumi lilikataza waumini wa kawaida wasisiome Biblia

isipokuwa makuhani tu. Lugha ya kilatini iliteuliwa kuwa lugha takatifu na hivyo mtu

yeyote asiyejua kilatini alizuiliwa kuhubiri.

1. PITA WALDO.

Katika miaka ya 1170 alitokea mfanya biashara mmoja aliyeitwa Pita waldo mwenyeji

wa Loyona Ufaransa. Mtu huyu alipenda kujua mambo yaliyo katka Biblia lakini

hakuweza kwa sababu hakufahamu kilatini hivyo aliwaajiri mapadri wawili wamtafsirie

Biblia katika lugha ya kifaransa. Baada ya kusoma neno la Mungu alivutiwa nalo sana

hivyo akauza kila kitu alichokuwa nacho na akala kiapo cha umaskini, akajitoa kikamilifu

kuhubiri neno la Mungu.

Pita Waldo Alianzisha timu iliyoitwa watu maskini. walianza kuhubiri, lakni walipingwa

na papa. Mwaka 1184 walijitenga na kanisa kwa sababu hawakukubali kitendo cha wao

kuzuiwa kuhubiri,

Waldo alipinga baadhi ya mafundisho ya kanisa Katoliki. Baadhi ya mambo aliyoyapinga

ni

Mafundisho kuhusu toharani,

Misa kwaajili ya wafu

Kumwabudu Mariamu mama wa Yesu.

Kanisa kuwa na mamlaka juu ya Biblia

Kuifanya lugha ya kilatini kuwa lugha takatifu

41

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!