Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
nyaraka hizo ziliandikwa na wahusika walioandikwa kumbe sivyo. Zifuatazo ni baadhi ya
nyaraka hizo
Waraka wa mfalme Kostantino kwa askofu Silvesta (314-335 BK). Huu ulikuwa ni waraka
uliogushiwa na viongozi wa kanisa kwamba uliandikwa na Kostantino kumpa askofu wa
Rumi (Silvesta) mamlaka ya kiutawala juu ya wafalme wote wa Ulaya na Ulaya nzima.
Tamko la uongo la Isodore(850 BK). Kulikuwa na maandiko yaliyokuwa yanadai
kwamba askofu wa Rumi alikuwa amepokea waraka toka kwa mitume uliokuwa
unamtangaza askofu wa Rumi kuwa askofu wa kanisa dunia nzima na kwamba kanisa
lilitangazwa kuwa huru (yaani kanisa kutokuwa chini ya serikali).
2 KUSITAWI KWA UPAPA (1073- 1216 )
Nguvu ya upapa ilifikia kilele chake katika utawala wa Gegori VII ambaye pia alijulikana
kama Hildebrand. Katika kipindi hiki upapa ulikuwa na nguvu kamili kikanisa na
kiserikali katika mataifa yote ya kule Ulaya.
i. Papa Gregori VII alifanya matengenezo ya ukreli na kukataza ndoa kwa wakreli.
ii. Aliliondoa kanisa chini ya utawala wa serikali, kanisa likaanza kujitawala, alifuta suala
la maaskofu kuteuliwa na watawala wa serikali (wafalme).
iii. Alilifanya kanisa kuwa juu ya selikali.
Papa Innocent III (1198 -1216).
Huyu alikuwa ni papa mwingine mwenye nguvu kubwa. Katika siku yake ya kutawazwa
kuwa papa alitoa usemi wenye maneno yafuatayo.
“ Mahalifa wa mtakatifu Petro wako katikati ya Mungu na watu; wadogo kuliko
Mungu lakini wakubwa kuliko watu, wenye uwezo wa kuwahukumu watu wote lakini
wasioweza kuhukumiwa na yeyote”
Katika barua yake ya kiofisi aliandika
“ papa hajapewa mamlaka kwa kanisa pekee bali kwa ulimwengu mzima. Akiwa na
haki ya kuwaondoa na kuwaweka watawala katika uongozi”
Papa innocent III alijitwalia mamlaka ya serikali ya mji wa Rumi akijifanya yeye
mwenyewe kuwa bwana kwa kuanzisha nchi ndani ya nchi ijulikanayo kama nchi ya
Vatikani. Hivyo papa akawa kiongozi wa kidini na kiserikali.
3 KUANGUKA KWA UPAPA.
Kuanguka kwa upapa kulianza wakati wa papa Bonifasi VIII katika mwaka 1303. Jambo
hili lilisababishwa na kuanza kuibuka kwa roho ya utaifa miongoni mwa nchi mbalimbali.
Jambo hili lilileta mtikisiko dhidi ya Bonifasi VIII. Watu walianza kuwaheshimu viongozi
wa nchi zao kuliko kumheshimu papa. Amri na maagizo mbalimbali ya papa yalipuuzwa
na viongozi wa nchi. Baada ya mfalme wa ufaransa kukata kutii maagizo ya papa, papa
39