21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

nyaraka hizo ziliandikwa na wahusika walioandikwa kumbe sivyo. Zifuatazo ni baadhi ya

nyaraka hizo

Waraka wa mfalme Kostantino kwa askofu Silvesta (314-335 BK). Huu ulikuwa ni waraka

uliogushiwa na viongozi wa kanisa kwamba uliandikwa na Kostantino kumpa askofu wa

Rumi (Silvesta) mamlaka ya kiutawala juu ya wafalme wote wa Ulaya na Ulaya nzima.

Tamko la uongo la Isodore(850 BK). Kulikuwa na maandiko yaliyokuwa yanadai

kwamba askofu wa Rumi alikuwa amepokea waraka toka kwa mitume uliokuwa

unamtangaza askofu wa Rumi kuwa askofu wa kanisa dunia nzima na kwamba kanisa

lilitangazwa kuwa huru (yaani kanisa kutokuwa chini ya serikali).

2 KUSITAWI KWA UPAPA (1073- 1216 )

Nguvu ya upapa ilifikia kilele chake katika utawala wa Gegori VII ambaye pia alijulikana

kama Hildebrand. Katika kipindi hiki upapa ulikuwa na nguvu kamili kikanisa na

kiserikali katika mataifa yote ya kule Ulaya.

i. Papa Gregori VII alifanya matengenezo ya ukreli na kukataza ndoa kwa wakreli.

ii. Aliliondoa kanisa chini ya utawala wa serikali, kanisa likaanza kujitawala, alifuta suala

la maaskofu kuteuliwa na watawala wa serikali (wafalme).

iii. Alilifanya kanisa kuwa juu ya selikali.

Papa Innocent III (1198 -1216).

Huyu alikuwa ni papa mwingine mwenye nguvu kubwa. Katika siku yake ya kutawazwa

kuwa papa alitoa usemi wenye maneno yafuatayo.

“ Mahalifa wa mtakatifu Petro wako katikati ya Mungu na watu; wadogo kuliko

Mungu lakini wakubwa kuliko watu, wenye uwezo wa kuwahukumu watu wote lakini

wasioweza kuhukumiwa na yeyote”

Katika barua yake ya kiofisi aliandika

“ papa hajapewa mamlaka kwa kanisa pekee bali kwa ulimwengu mzima. Akiwa na

haki ya kuwaondoa na kuwaweka watawala katika uongozi”

Papa innocent III alijitwalia mamlaka ya serikali ya mji wa Rumi akijifanya yeye

mwenyewe kuwa bwana kwa kuanzisha nchi ndani ya nchi ijulikanayo kama nchi ya

Vatikani. Hivyo papa akawa kiongozi wa kidini na kiserikali.

3 KUANGUKA KWA UPAPA.

Kuanguka kwa upapa kulianza wakati wa papa Bonifasi VIII katika mwaka 1303. Jambo

hili lilisababishwa na kuanza kuibuka kwa roho ya utaifa miongoni mwa nchi mbalimbali.

Jambo hili lilileta mtikisiko dhidi ya Bonifasi VIII. Watu walianza kuwaheshimu viongozi

wa nchi zao kuliko kumheshimu papa. Amri na maagizo mbalimbali ya papa yalipuuzwa

na viongozi wa nchi. Baada ya mfalme wa ufaransa kukata kutii maagizo ya papa, papa

39

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!