You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Katika kipindi cha Pergamo tuliona jinsi Patriaki wa Rumi alivyochukua mamlaka ya
uongozi wa kanisa na kuinuka kwa Rumi kuwa makao makuu ya kanisa. Tuliona jinsi
mafundisho potofu pamoja mambo ya kipagani yalivyoingia kanisani
Haikutosha kwa Patriaki wa Rumi kuwa Askofu mkuu wa kanisa lote duniani na kuwa na
mji wa Rumi kama makao makuu ya kanisa lote duniani, baada ya hapo alijitangaza kuwa
kiongozi wa mataifa kwa njia ya kukuza upapa katika karne kumi za kipindi cha giza.
Kipindi cha giza kilikuwa na hatua tatu ambazo ni, kukua, kusitawi na kuanguka.
1. Kukua.
Gregori I alipokuwa kijana aliteuliwa kuwa msimamizi wa majengo na vyakula katika Mji
wa Rumi. Baada ya kifo cha baba yake aliamua kutoa kwa kanisa mirathi ya babaye.
Mnamo mwaka 578 BK Gregori I aliteuliwa na papa kuwa balozi wake katika mji wa
Kostantinopali. Mwaka 585 hadi 590 BK alikuwa msaidizi wa papa huko Rumi na
kiongozi mkuu wa Monastery(nyumba za utawa). Baada ya papa Pelegio II kufariki dunia
kwa ugonjwa wa tauni mwaka 590 BK, Grogori I aliteuliwa na umati wa watu huko Rumi
kuwa Askofu badala ya Peregio II.
Kukua kwa nguvu ya upapa kulianza baada ya Gregori I kushika wadhifa wa upapa
katika mwaka wa 590 BK. Mfumo wa kubadilisha majina mtu alipokuwa anaingia
katika nafasi ya upapa ulianza katika kipindi hiki. Gregori aliitwa mkuu kwa sababu ya
mafanikio yake ambayo baadhi ni,
i. Alitumia uwezo wa kikanisa katika kuwasaidia watu, (kuwapa chakula na nguo).
ii. Serikali ilipolega aliimarisha ulinzi katika mji wa Rumi.
iii. Alimtambua papa wa Rumi kuwa na mamlaka juu ya viongozi wengine wote wa
kanisa.
iv. Alilipatia kanisa nguvu ya kisiasa na kidini.
v. Alitengeneza dogma ya kanisa.
vi. Kutokana na misaada ya kijamii iliyokuwa ikitolewa na papa Gregori I wananchi wa
Rumi walianza kumheshimu na kumhesabu kama kiongozi wao. Hivyo basi Gregori
Mkuu aliimarisha nguvu ya upapa katika mambo ya kidini na kisiasa pia.
Sababu za kukua kwa upapa
Mbali na mchango wa Gregori Mkuu katika kukuza nguvu ya upapa kulikuwa mambo
mengine kadhaa yaliyopelekea kukua kwa upapa katika kipindi hiki. Baadhi ya sababu
hizo ni:
1. Nguvu ya haki, kanisa liliwatetea raia dhidi ya watawala dhalimu hivyo likapendwa na
watu wengi.
Kuzolota kwa serikali, Wakati serikali inazolota kanisa lilizidi kujiimarisha, kiuchumi na
kijeshi hivyo viongozi dhaifu walihitaji msaada wa kanisa katika kupambana na adui zao
hivyo kanisa likazidi kuwa na mamlaka na nguvu ya ushawishi.
2. Ulaghai, Kanisa lilitumia kigezo cha ujinga wa watu kujipatia mamlaka. Kanisa
lilitengeneza nyaraka mbalimbali zenye kulipa mamlaka ya kiutawala na kudai kwamba
38