You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
3. Upendeleo na anasa. Baada ya utawa kupata umaarufu, walianza kuishi maisha ya
anasa na kukwepa kulipa kodi.
4. Utawa haukuwa na msingi ki-Biblia
5. Watawa waliielewa visivyo Injili ya Yesu kristo waliyoitumia kuhalalisha utawa.
J. KUANGUKA KWA DOLA YA RUMI
Mfalme Kostantino mara baada ya kuingia katika utawala alihamishia makao makuu ya
dola ya Rumi katika mji wa Kostantinopali. Tutatazama namna Rumi ilivyokuwa makao
makuu ya kanisa. Wakati kanisa la Orthodox la mashariki lilikuwa likitawaliwa na serikali,
Patriaki wa Rumi alidai kuwa na mamlaka katika kanisa lote la ulimwengu wa magharibi,
ambao ulikuwa kupitia kanisa la Katoliki la Rumi. Hii iliwezekana kwa sababu kadhaa,
badhi zikiwa ni;
Kufanana kiutawala. Kulikuwa na mazoea kuongoza kanisa kwa mfumo wa kiserikali
ambapo kunakuwa na kiongozi mkuu mmoja anaetakiwa kusikilizwa . wakati huu
kulikuwa na maaskofu karibu kila mji, ambao katika miji mikubwa waliitwa Patriaki
(patriarch) yaani baba mkubwa. Kulikuwa na mapatriaki katika miji ya Yerusalemu,
Antiokia, Iskanderia, Rumi na Kostantinopali.
Kulikuwa na mashindano ya kugombea ukuu miongoni mwa mapatriaki. Swali lilikuwa
nani angekuwa kiongozi mkuu wa kanisa lote ulimwenguni. Rumi ikiwa imetengeneza njia
ya kuwa makao makuu ya kanisa ilikuwa na viongozi bora.
Kwa muda mrefu kanisa la Rumi lilikuwa imara. Lilisimama kidete kupinga mafundisho
potofu. Kanisa la Rumi liliihudumia Jamii kiroho na kimwili kwa kuanzisha kazi za kijamii
dunia nzima. Nyumba za utawa, shule na hospitali zilianzishwa katika maeneo
mbalimbali, jambo hili lililipa umaarufu kanisa la Rumi. Wamishenari walitumwa katika
ulimwengu mzima wa wakati ule kueneza Neno la Mungu.
Wakati nguvu ya kanisa ilikuwa inakua, nguvu ya dola iliendelea kuzorota, nguvu ya
kisiasa ya Rumi ilizidi kuporomoka.
Kwa muda mrefu wa utawala wake dola ya Rumi ilikuwa imetajirika sana. Maadui zake
waliokuwa wanaishi jirani nae waliutamani utajiri wake. Maadui hao waliivamia Rumi
ambayo sasa haikuwa na uzoefu wa kivita. Baadhi ya maadui walioivamia Rumi na
kuishambulia ni wavisigothi, wasaksoni, wavandali, , wahuni, wabarigandiana na
wafranka. Uvamizi wa mataifa haya ulipunguza nguvu ya dola ya Rumi.
Janga lingine lilikuwa ni vita ya wenyewe kwa wenyewe, baina ya wanachama wa seneti
kugombania kiti cha utawala. Kabila la kijerumani lililojulikana kama Herulisi liliivamia
na kuishinda dola ya Rumi mnamo mwaka 476 BK.
36