Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Utawa ulienea sana sehemu ya magharibi kwa njia ya Jerome. Mtu huyu alikuwa na uwezo
mkubwa wa kufasiri Maandiko na alifanywa kuwa katibu wa Papa wa Rumi kwa kipindi
kirefu. Aliishi maisha ya kujikana. Alisema “ Mtu asieoa hujipatia sifa ya pekee mbele ya
Mungu. Alikiri kwa wazi kabisa kwamba “ Maisha ya utawa hayawezi kuondoa majaribu
yote” Alidai kwamba alipokaa katika boma la utawa huko mlimani bado aliwaza juu ya
wasichana wa Rumi.
Jerome alikuwa fundi wa Maandiko na elimu. Alitafsiri Biblia kwa lugha ya Kilatini
iliyojulikana kwa jina la Vulgate. Tafsiri inayopendwa sana na wakatoliki wa Rumi mpaka
sasa.
Yeye alishirikiana na wanawake watawa kutunza yatima Huko Bethrehemu na Palestina.
Walikuwa na nyumba mbili za watawa, moja ikiwa ya watawa wa kiume na nyingine ya
watawa wa kike.
Benedikto Mwanzilishi wa Kanuni Za Utawa.
Benedikto wa Nusia alianzisha shirika la utawa huko Monte Kasino Italia. Yeye aliweka
mkazo katika umoja. Aliweka uongozi uliosimamia nyumba zote za utawa. Aliona kuwa
kila nyumba ya utawa ni jeshi la Yesu waliotayari kumtumikia wakati wowote.
Kiongozi wa kila nyumba ya utawa aliitwa Aboot, na watawa wote walipaswa kumtii.
Aliweka mpangilio mzuri wa saa za ibada, sala na kusoma. Nyumba za kanuni za
Benedikto zilikuwa mahali pakuu pa elimu na kilimo.
Umonaki katika nchi za Ulaya
Umonaki uienea taratibu katika nchi za Ulaya ikilinganishwa na Afrika na Asia. Badala ya
kila mtu kuishi peke yake, umonaki wa ulaya ulipangiliwa na kusimamiwa vizuri. Kazi na
sala ziliunganishwa pamoja.
Faida Za Utawa.
1. Ulifanyika kuwa vituo vya wakimbizi.
2. Walitoa msaada kwa watu wenye mahitaji , mfano kusaidia maskini na wasiojiweza.
3. Walileta mchango mkubwa katika kuinua kilimo.
4. Walikuza elimu kwani watawa walitumia muda mwingi katika kusoma na kuandika
maandiko mbalimbali.
5. Walipeleka wamishenari katika mataifa mbalimbali kueneza Injili.
6. Walitoa viongozi bora katika jamii na katika kanisa.
7. Walitafsiri Maandiko katika lugha mbalimbali.
Madhaifu Ya Utawa.
1. Mkazo wa juu ya kuishi maisha ya useja.waliwakataza wafuasi wao wasioe wala
kuolewa.
2. Walikuwa omba omba kwa watu waliowatembelea
35