21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Utawa ulienea sana sehemu ya magharibi kwa njia ya Jerome. Mtu huyu alikuwa na uwezo

mkubwa wa kufasiri Maandiko na alifanywa kuwa katibu wa Papa wa Rumi kwa kipindi

kirefu. Aliishi maisha ya kujikana. Alisema “ Mtu asieoa hujipatia sifa ya pekee mbele ya

Mungu. Alikiri kwa wazi kabisa kwamba “ Maisha ya utawa hayawezi kuondoa majaribu

yote” Alidai kwamba alipokaa katika boma la utawa huko mlimani bado aliwaza juu ya

wasichana wa Rumi.

Jerome alikuwa fundi wa Maandiko na elimu. Alitafsiri Biblia kwa lugha ya Kilatini

iliyojulikana kwa jina la Vulgate. Tafsiri inayopendwa sana na wakatoliki wa Rumi mpaka

sasa.

Yeye alishirikiana na wanawake watawa kutunza yatima Huko Bethrehemu na Palestina.

Walikuwa na nyumba mbili za watawa, moja ikiwa ya watawa wa kiume na nyingine ya

watawa wa kike.

Benedikto Mwanzilishi wa Kanuni Za Utawa.

Benedikto wa Nusia alianzisha shirika la utawa huko Monte Kasino Italia. Yeye aliweka

mkazo katika umoja. Aliweka uongozi uliosimamia nyumba zote za utawa. Aliona kuwa

kila nyumba ya utawa ni jeshi la Yesu waliotayari kumtumikia wakati wowote.

Kiongozi wa kila nyumba ya utawa aliitwa Aboot, na watawa wote walipaswa kumtii.

Aliweka mpangilio mzuri wa saa za ibada, sala na kusoma. Nyumba za kanuni za

Benedikto zilikuwa mahali pakuu pa elimu na kilimo.

Umonaki katika nchi za Ulaya

Umonaki uienea taratibu katika nchi za Ulaya ikilinganishwa na Afrika na Asia. Badala ya

kila mtu kuishi peke yake, umonaki wa ulaya ulipangiliwa na kusimamiwa vizuri. Kazi na

sala ziliunganishwa pamoja.

Faida Za Utawa.

1. Ulifanyika kuwa vituo vya wakimbizi.

2. Walitoa msaada kwa watu wenye mahitaji , mfano kusaidia maskini na wasiojiweza.

3. Walileta mchango mkubwa katika kuinua kilimo.

4. Walikuza elimu kwani watawa walitumia muda mwingi katika kusoma na kuandika

maandiko mbalimbali.

5. Walipeleka wamishenari katika mataifa mbalimbali kueneza Injili.

6. Walitoa viongozi bora katika jamii na katika kanisa.

7. Walitafsiri Maandiko katika lugha mbalimbali.

Madhaifu Ya Utawa.

1. Mkazo wa juu ya kuishi maisha ya useja.waliwakataza wafuasi wao wasioe wala

kuolewa.

2. Walikuwa omba omba kwa watu waliowatembelea

35

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!