You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
kwamba mtu hawezi kuokolewa kwa uchaguzi wake mwenyewe, bali ni kwa mapenzi ya
Mungu na kwamba neema ya Mungu haiwezi kukataliwa na wanadamu.
Mafundisho ya pelegio yalipingwa vikali na kanisa na kuonekana ni uzushi. Kanisa
lilikubali mafundisho ya Agustino mkuu ambayo pia yalijengewa hoja na
wanamatengenzo ya kanisa katika kipindi cha matengenezo katika karne ya 16 1
I. KUZUKA KWA UMONAKI.
Utawa au umonaki ulianza katika karne ya tatu BK. Kabla ya kipindi hicho wakristo
waliishi katika jamii na familia. Mara baada ya ukristo kushamiri mambo ya dunia yalianza
kuingia kanisani, baadhi ya wacha Mungu hawakuridhika na hali hiyo hivyo waliamua
kujitenga na kukaa peke yao nje ya mji katika mapango au katika nyumba walizokuwa
wamejenga. Nyumba hizo zilijulikana kama nyumba za watawa maarufu kama Monastery.
Baadhi ya mambo yaliyochochea kuanzishwa kwa utawa ni
i. Mvuto wa Injili, Injili ya Yesu alipomwambia Yule kijana tajiri kuuza kila kitu na
kuwapa maskini kasha kumfuata Yesu.
ii. Maovu kukithirikatika kanisa. Kutokana na mmonyoko wa maadili na kuhalalishwa
kwa dhambi ndani ya kanisa.s
iii. Falsafa ya uovu wa mwili. Imani ya kuwa mwili ni muovu na hivyo unapaswa
kuteswa vikali ili kuudhibiti.
Kutokana na mikazo juu ya mambo yaliyotajwa hapo juu, kulikuwa na watu ambao
waliuza kila kitu walichokuwanacho wakawagawia maskini na kisha wakajitenga na
kuamua kuishi maisha ya kimasikini mbali na jamii yao. Baadhi ya watu hao ni;
Antoni Mtawa Wa Kwanza.
Mtu huyu alikuwa ni mwenyeji wa Misri na ndiye mwanzilishi wa utawa. Antoni aliuza
kila kitu alichokuwa nacho na kuwagawia maskini mali zake na kisha akaishi nje ya mji
akilima na kuwapatia maskini chakula alicholima. Baada ya muda alijitenga na kuishi
peke yake pangoni mlimani. Watu mbalimbali walimwendea huko pangoni ili kujifunza na
kisha alifanikiwa kupata wafuasi ambao nao waliamua kuungana nae kuishi maisha ya
utawa. Alipat wafuasi karibuni 2000
Pokomeo Mwanzilishi Wa Nyumba Za Utawa.
Huyu alikuwa mdogo wa Antoni na ndie aliyeanzisha nyumba za utawa. Yeye alijenga
boma kubwa ambalo wafuasi wake waliishi ndani wakijitenga na mambo ya ulimwengu.
Watawa hawa walijishughulisha na ibada na kazi, utawa huu ulikaza ushirika na
ulipendwa na watu wengi.
Jerome (Hironimo)
34