21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

ambao ulipaswa kutumiwa na makanisa yote. Ukiri huo uliweka mkazo katika uungu wa

Yesu kuwa Yesu ni sawa na baba.

Mkutano wa Naikea haukuweza kumaliza majadiliano na badala yake uliyachochea

kwani majadiliano hayo yaliendelea kwa muda wa miaka 35 baada ya mkutano wa Naikea.

Baadhi ya viongozi wa kanisa walitilia mashaka ukiri wa Naikea kwasababu hawakuuzoea.

Mkutano Wa Kostantinopali

Kutokana na majadiliano hayo ya muda mrefu na makali kulikuwepo na haja ya kuitisha

mkutano mwingine wa kanisa zima. Mkutano hu uliitishwa katika mji wa Kostantinopali

mnamo mwaka wa 381 BK. Katika mkutano huu walifanya marekebisho kidogo ya

ukiri wa imani wa Naikea.

Mkutano Wa Efeso. (Mabishano kati ya Sirilo na Nestori)

Baada ya Apolinari kuhukumiwa uzushi, kuliendelea mabishano makali katika kanisa.

Baadhi ya mabishano hayo yalikuwa baina ya askofu Sirilo wa Iskandelia na askofu

Nestori wa Kostantinopali.

Sirio alipinga fundisho la Apolinari. Aliona kwamba uungu na ubinadamu wa Yesu

kuwa ni hali mbili zisizoweza kutenganishwa . Alipokuwa anataka kueleza uungu wa

Yesu alianza kwa kumwita bikira Maria ‘Theotokos’ yaani mama wa Mungu.

Askofu Nestori alibaini uzushi katika maelezo ya Sirilo, yeye alipendekeza Mariamu aitwe

mama wa Kristo. Maaskofu hao walishambuliana vikali sana kwa maandishi. Shauli hilo

lilipelekwa kwa askofu wa Rumi ili aweze kutoa uamuzi. Askofu wa Rumi alimpa ushindi

Sirilo na kumtangaza Nestori kuwa mzushi.Hayo yalifanyika katika mkutano wa tatu wa

kanisa uliofanyika katika mji wa Efeso mnamo mwaka 433 BK.

2. Majadiliano Ya Apolinari.

Apolinari alikuwa ni askofu wa Laodikia. Askofu huyu alijaribu kueleza uhusiano uliopo

baina ya hali mbili tofauti alizo nazo Yesu. Yaani hali ya uungu na hali ya ubinadamu.

Yeye alikuwa na mtazamo wa kwamba mwili wa Yesu ni ubinadamu na akili na roho

yake ni Logosi aliyefanyika mwili. Katika kueleza fundisho hilo askofu huyu alikaza

uugu wa Yesu uliokana ubinadamu wake. Kutokana na fundisho hili Apolinari

alitangazwa kuwa mzushi katika mkutano wa Kostantinopali mnamo mwaka 381BK.

3. Mabishano Ya Pelegio.

Pelegio alikuwa ni mmonaki, mwingereza aliyekuja Afrika Kaskazini kwajili ya kuhubiri

Neno la Mungu katika kanisa la Afrika ya Kaskazini.

Peregio alifundisha kwamba mtu harithi dhambi toka kwa Adamu, lakini kila mtu ni

lazima afanye uchaguzi yeye mwenyewe.

Pelegio alipingwa vikali na Agustino mkuu kwa mafundisho yake. Agustino alifundisha

kwamba Adamu alipotenda dhambi alikiwakilisha kizazi chote cha binadamu na

33

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!