Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
ambao ulipaswa kutumiwa na makanisa yote. Ukiri huo uliweka mkazo katika uungu wa
Yesu kuwa Yesu ni sawa na baba.
Mkutano wa Naikea haukuweza kumaliza majadiliano na badala yake uliyachochea
kwani majadiliano hayo yaliendelea kwa muda wa miaka 35 baada ya mkutano wa Naikea.
Baadhi ya viongozi wa kanisa walitilia mashaka ukiri wa Naikea kwasababu hawakuuzoea.
Mkutano Wa Kostantinopali
Kutokana na majadiliano hayo ya muda mrefu na makali kulikuwepo na haja ya kuitisha
mkutano mwingine wa kanisa zima. Mkutano hu uliitishwa katika mji wa Kostantinopali
mnamo mwaka wa 381 BK. Katika mkutano huu walifanya marekebisho kidogo ya
ukiri wa imani wa Naikea.
Mkutano Wa Efeso. (Mabishano kati ya Sirilo na Nestori)
Baada ya Apolinari kuhukumiwa uzushi, kuliendelea mabishano makali katika kanisa.
Baadhi ya mabishano hayo yalikuwa baina ya askofu Sirilo wa Iskandelia na askofu
Nestori wa Kostantinopali.
Sirio alipinga fundisho la Apolinari. Aliona kwamba uungu na ubinadamu wa Yesu
kuwa ni hali mbili zisizoweza kutenganishwa . Alipokuwa anataka kueleza uungu wa
Yesu alianza kwa kumwita bikira Maria ‘Theotokos’ yaani mama wa Mungu.
Askofu Nestori alibaini uzushi katika maelezo ya Sirilo, yeye alipendekeza Mariamu aitwe
mama wa Kristo. Maaskofu hao walishambuliana vikali sana kwa maandishi. Shauli hilo
lilipelekwa kwa askofu wa Rumi ili aweze kutoa uamuzi. Askofu wa Rumi alimpa ushindi
Sirilo na kumtangaza Nestori kuwa mzushi.Hayo yalifanyika katika mkutano wa tatu wa
kanisa uliofanyika katika mji wa Efeso mnamo mwaka 433 BK.
2. Majadiliano Ya Apolinari.
Apolinari alikuwa ni askofu wa Laodikia. Askofu huyu alijaribu kueleza uhusiano uliopo
baina ya hali mbili tofauti alizo nazo Yesu. Yaani hali ya uungu na hali ya ubinadamu.
Yeye alikuwa na mtazamo wa kwamba mwili wa Yesu ni ubinadamu na akili na roho
yake ni Logosi aliyefanyika mwili. Katika kueleza fundisho hilo askofu huyu alikaza
uugu wa Yesu uliokana ubinadamu wake. Kutokana na fundisho hili Apolinari
alitangazwa kuwa mzushi katika mkutano wa Kostantinopali mnamo mwaka 381BK.
3. Mabishano Ya Pelegio.
Pelegio alikuwa ni mmonaki, mwingereza aliyekuja Afrika Kaskazini kwajili ya kuhubiri
Neno la Mungu katika kanisa la Afrika ya Kaskazini.
Peregio alifundisha kwamba mtu harithi dhambi toka kwa Adamu, lakini kila mtu ni
lazima afanye uchaguzi yeye mwenyewe.
Pelegio alipingwa vikali na Agustino mkuu kwa mafundisho yake. Agustino alifundisha
kwamba Adamu alipotenda dhambi alikiwakilisha kizazi chote cha binadamu na
33