You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
hao waliona kwamba dhana ya utatu wa Mungu ilielekea kuwa ni uzushi wa kuwa na
miumngu mingi.
Wamonarchianism waligawanyika katika makundi mawili ambayo ni;
1. Wamonarchianism wa kimabadiliko, hawa walikuwa na mtazamo wenye kumwona
Yesu kama mwanadamu pekee tu, ambae hakuwa Mungu aliyefanyika mwili. Kundi hili
liliongozwa na Askofu Paulo Samosota wa Antiokia.
2. Wamonarchianism wa kimfano. Hawa waliona kuwa hakuna tofauti kati ya baba na
mwana. Baba ndiye aliyevaa mwili. Kwa hiyo majina haya baba, mwana na Roho
mtakatifu yalitumika kuonesha kwetu njia au hali tatu Mungu alizotumia
kujidhihirisha. Hivyo hakuna nafsi tatu bali ni nafsi moja. Kundi hili liliongozwa na
Sabelio.
Baada ya mateso kukoma katika kanisa kulitokea mgogoro mwingine ndani ya kanisa
uliohusisha mgongano wa kimafundisho (doctrinal controversals).
Baadhi ya viongozi wa kanisa walianza kuibuka na mafundisho yaliyoonekana kuwa
mageni katika kanisa na hivyo walihukumiwa uzushi na kutengwa na kanisa.
Wakristo walitumia muda mwingi kujadiliana wao kwa wao badala ya kuipeleka
Injili mbele. Katika moduli hii tutajadili badhi tu ya mabishano ya kithiolojia yaliyotokea
ndani ya kanisa.
1. Mabishano Baina Ya Mchungaji Ario Na Askofu Alexander.
Ario alimshutumu askofu wake kuwa alikuwa anaweka mkazo sana juu ya uungu wa Yesu
katika mafundisho yake. Alexander alifundisha kwamba mwana ni wa milele sawa na
baba. Ario alipinga fundisho hilo yeye alidai kwamba baba ni wa milele lakini mwana
alikuwa na mwanzo wake. Kuna kipindi ambapo mwana hakuwapo. Askofu Alexander
aliitisha mkutano wa sinodi huko Iskanderia ili kujadili suala hilo na hatimae Ario
alitangazwa kuwa mzushi na alitengwa na kanisa.
Ario aliungana na Askofu Euzebio wa Nikomedia na wakaandika nyaraka mbalimbli
ambazo zilitetea fundisho lao na wakazisambaza maeneo mbalimbali ili ziendelee
kusomwa na wakristo mbalimbali.
Mkutano Wa Naikea.
Baada ya nyaraka hizo kusomwa majadiliano miongoni wa viongozi wa kanisa yalipamba
moto na kuleta mgawanyiko ndani ya kanisa. Mfalme Kostantino hakupendezwa na
mgogoro huo ulioleta mgawanyiko miongoni mwa wakristo hivyo aliwaomba viongozi hao
wapatane na iliposhindikana kupatana kwa viongozi hao, mfalme akitumia nguvu ya dola
aliamua kuitisha mkutano wa viongozi wote wa kanisa toka sehemu mbalimbali ili aweze
kuwapatanisha. Mkutano huo ulifanyika mwaka 325BK katika mji wa Naikea na
kutambulikana kama mkutano wa kwanza wa kanisa zima, kwa sababu ulihusisha viongozi
mbalimbali toka sehehemu mbalimbali.
Katika mkutano huo Askofu alexender alishinda kwa hoja na hatimae Ario alitangazwa
kuwa mzushi na akatengwa na kanisa. Katika kipindi hiki kanisa lilitunga ukiri wa imani
32