21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

hao waliona kwamba dhana ya utatu wa Mungu ilielekea kuwa ni uzushi wa kuwa na

miumngu mingi.

Wamonarchianism waligawanyika katika makundi mawili ambayo ni;

1. Wamonarchianism wa kimabadiliko, hawa walikuwa na mtazamo wenye kumwona

Yesu kama mwanadamu pekee tu, ambae hakuwa Mungu aliyefanyika mwili. Kundi hili

liliongozwa na Askofu Paulo Samosota wa Antiokia.

2. Wamonarchianism wa kimfano. Hawa waliona kuwa hakuna tofauti kati ya baba na

mwana. Baba ndiye aliyevaa mwili. Kwa hiyo majina haya baba, mwana na Roho

mtakatifu yalitumika kuonesha kwetu njia au hali tatu Mungu alizotumia

kujidhihirisha. Hivyo hakuna nafsi tatu bali ni nafsi moja. Kundi hili liliongozwa na

Sabelio.

Baada ya mateso kukoma katika kanisa kulitokea mgogoro mwingine ndani ya kanisa

uliohusisha mgongano wa kimafundisho (doctrinal controversals).

Baadhi ya viongozi wa kanisa walianza kuibuka na mafundisho yaliyoonekana kuwa

mageni katika kanisa na hivyo walihukumiwa uzushi na kutengwa na kanisa.

Wakristo walitumia muda mwingi kujadiliana wao kwa wao badala ya kuipeleka

Injili mbele. Katika moduli hii tutajadili badhi tu ya mabishano ya kithiolojia yaliyotokea

ndani ya kanisa.

1. Mabishano Baina Ya Mchungaji Ario Na Askofu Alexander.

Ario alimshutumu askofu wake kuwa alikuwa anaweka mkazo sana juu ya uungu wa Yesu

katika mafundisho yake. Alexander alifundisha kwamba mwana ni wa milele sawa na

baba. Ario alipinga fundisho hilo yeye alidai kwamba baba ni wa milele lakini mwana

alikuwa na mwanzo wake. Kuna kipindi ambapo mwana hakuwapo. Askofu Alexander

aliitisha mkutano wa sinodi huko Iskanderia ili kujadili suala hilo na hatimae Ario

alitangazwa kuwa mzushi na alitengwa na kanisa.

Ario aliungana na Askofu Euzebio wa Nikomedia na wakaandika nyaraka mbalimbli

ambazo zilitetea fundisho lao na wakazisambaza maeneo mbalimbali ili ziendelee

kusomwa na wakristo mbalimbali.

Mkutano Wa Naikea.

Baada ya nyaraka hizo kusomwa majadiliano miongoni wa viongozi wa kanisa yalipamba

moto na kuleta mgawanyiko ndani ya kanisa. Mfalme Kostantino hakupendezwa na

mgogoro huo ulioleta mgawanyiko miongoni mwa wakristo hivyo aliwaomba viongozi hao

wapatane na iliposhindikana kupatana kwa viongozi hao, mfalme akitumia nguvu ya dola

aliamua kuitisha mkutano wa viongozi wote wa kanisa toka sehemu mbalimbali ili aweze

kuwapatanisha. Mkutano huo ulifanyika mwaka 325BK katika mji wa Naikea na

kutambulikana kama mkutano wa kwanza wa kanisa zima, kwa sababu ulihusisha viongozi

mbalimbali toka sehehemu mbalimbali.

Katika mkutano huo Askofu alexender alishinda kwa hoja na hatimae Ario alitangazwa

kuwa mzushi na akatengwa na kanisa. Katika kipindi hiki kanisa lilitunga ukiri wa imani

32

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!